Cute Wife
JF-Expert Member
- Nov 17, 2023
- 1,906
- 5,000
Wakuu,
Jaji Mkuu Martha Koome ameituhumu serikali, kupitia Wizara ya Mambo ya Ndani, kwa kuondoa walinzi wake, hatua ambayo ameielezea kama shambulio dhidi ya Mahakama na ofisi ya Jaji Mkuu.
Koome alitoa madai hayo katika barua aliyoiandika Alhamisi kwa Waziri wa Mambo ya Ndani Kipchumba Murkomen na Inspekta Jenerali wa Polisi Douglas Kanja, akionyesha wasiwasi mkubwa kuhusu hatua hiyo.
Kwa mujibu wa Koome, uamuzi huo sio tu matusi kwa uhuru wa Idara ya Mahakama, bali pia unahatarisha usalama wa maafisa wa mahakama kote nchini.
"Ninaeleza wasiwasi mkubwa kuhusu kuondolewa kwa walinzi wa Jaji Mkuu—kitendo kinachodhoofisha uhuru wa mahakama, kutishia uadilifu wa taasisi, na kuhatarisha maendeleo ya kidemokrasia," alisema Koome katika barua hiyo iliyoonwa na Citizen Digital.
"Vyombo vya serikali vimepewa jukumu takatifu la kuhudumia umma kwa kutumia rasilimali zinazotolewa na walipa kodi. Wajibu huu unawataka kuhakikisha kuwa hakuna taasisi au mwenye ofisi yeyote anayepaswa kukabiliwa na vitisho, shinikizo, au kuingiliwa kwa namna yoyote isiyo halali na mhimili mwingine wa serikali."
Aidha, Koome alisisitiza kuwa ulinzi kwa ofisi yake si starehe au matumizi binafsi, bali ni hitaji la kimuundo linalohakikisha Idara ya Mahakama inafanya kazi kwa uhuru na bila hofu.
"Ulinzi huu ni kinga ya kitaasisi inayolinda maafisa wa mahakama, majengo, na taratibu dhidi ya vitisho vyovyote vinavyoweza kudhoofisha utoaji wa haki. Kuondolewa kwa walinzi hawa ni dhihaka kubwa kwa kanuni ya mgawanyo wa madaraka," alisema Koome.
"Uhuru wa mahakama ni nguzo muhimu ya demokrasia inayofanya kazi. Inahakikisha kwamba Idara ya Mahakama inaweza kutekeleza majukumu yake bila upendeleo, kutumia sheria kwa usawa, na kuiwajibisha mihimili mingine ya serikali bila kushawishiwa kutoka nje."
Koome alieleza pia kuwa Wizara ya Mambo ya Ndani pia imepunguza idadi ya maafisa walioko katika Kitengo Maalum cha Polisi wa Mahakama, tawi la Huduma ya Polisi ya Kitaifa (NPS) lililoanzishwa mwaka 2021 kwa ajili ya kutoa ulinzi na huduma za usalama kwa maafisa wa mahakama.
Citizen Digital
Jaji Mkuu Martha Koome ameituhumu serikali, kupitia Wizara ya Mambo ya Ndani, kwa kuondoa walinzi wake, hatua ambayo ameielezea kama shambulio dhidi ya Mahakama na ofisi ya Jaji Mkuu.
Koome alitoa madai hayo katika barua aliyoiandika Alhamisi kwa Waziri wa Mambo ya Ndani Kipchumba Murkomen na Inspekta Jenerali wa Polisi Douglas Kanja, akionyesha wasiwasi mkubwa kuhusu hatua hiyo.
Kwa mujibu wa Koome, uamuzi huo sio tu matusi kwa uhuru wa Idara ya Mahakama, bali pia unahatarisha usalama wa maafisa wa mahakama kote nchini.
"Ninaeleza wasiwasi mkubwa kuhusu kuondolewa kwa walinzi wa Jaji Mkuu—kitendo kinachodhoofisha uhuru wa mahakama, kutishia uadilifu wa taasisi, na kuhatarisha maendeleo ya kidemokrasia," alisema Koome katika barua hiyo iliyoonwa na Citizen Digital.
"Vyombo vya serikali vimepewa jukumu takatifu la kuhudumia umma kwa kutumia rasilimali zinazotolewa na walipa kodi. Wajibu huu unawataka kuhakikisha kuwa hakuna taasisi au mwenye ofisi yeyote anayepaswa kukabiliwa na vitisho, shinikizo, au kuingiliwa kwa namna yoyote isiyo halali na mhimili mwingine wa serikali."
Aidha, Koome alisisitiza kuwa ulinzi kwa ofisi yake si starehe au matumizi binafsi, bali ni hitaji la kimuundo linalohakikisha Idara ya Mahakama inafanya kazi kwa uhuru na bila hofu.
"Ulinzi huu ni kinga ya kitaasisi inayolinda maafisa wa mahakama, majengo, na taratibu dhidi ya vitisho vyovyote vinavyoweza kudhoofisha utoaji wa haki. Kuondolewa kwa walinzi hawa ni dhihaka kubwa kwa kanuni ya mgawanyo wa madaraka," alisema Koome.
"Uhuru wa mahakama ni nguzo muhimu ya demokrasia inayofanya kazi. Inahakikisha kwamba Idara ya Mahakama inaweza kutekeleza majukumu yake bila upendeleo, kutumia sheria kwa usawa, na kuiwajibisha mihimili mingine ya serikali bila kushawishiwa kutoka nje."
Koome alieleza pia kuwa Wizara ya Mambo ya Ndani pia imepunguza idadi ya maafisa walioko katika Kitengo Maalum cha Polisi wa Mahakama, tawi la Huduma ya Polisi ya Kitaifa (NPS) lililoanzishwa mwaka 2021 kwa ajili ya kutoa ulinzi na huduma za usalama kwa maafisa wa mahakama.
Citizen Digital