JAJI Mkuu Mohamed Othman Chande, amekosoa mfumo wa kamati za maadili za mahakimu za mikoa na wilaya kuongozwa na wakuu wa mikoa, akisema kitendo hicho kinakwaza uhuru wa Mahakama.
Akizungumza katika majadiliano na ujumbe wa Mpango wa Hiari wa Kujitathmini Kiutawala Bora Afrika (APRM) jijini Dar es Salaam jana, Jaji Chande, alisema licha ya kuwepo kwa uhuru wa Mahakama, bado kitendo cha kamati za maadili za mahakimu kuwa chini ya viongozi wa Serikali, kinakwaza uhuru wa muhimili huo wa dola.
Uhuru wa Mahakama ni suala muhimu katika kutekeleza kazi zake, nchi nyingi za Afrika zimeshafikia uhuru huo, hata hapa kwetu lakini kuna suala moja tu ambalo linatukwaza.
Aliongeza; Kuwepo kwa viongozi wa mikoa na wilaya kwenye kamati za maadili za mahakimu, inapunguza uhuru wa Mahakama. Ingefaa kamati hizo ziwe chini ya Tume ya Huduma za Mahakama.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Utawala Bora, Mathias Chikawe alipotafutwa kwa simu, ili kuzungumzia hoja hiyo ya Jaji Chande, hakupatikana licha ya simu yake kuita kwa muda mrefu.
Kwa upandeb wake Waziri wa Sheria na Katiba, Celina Kombani alipoulizwa kuhusu kauli hiyo ya Jaji Mkuu alisema; Kamuulize mwenyewe (Jaji Mkuu Chande) yeye si ndiyo amesema hivyo? Basi kamuulize yeye ndiyo anajibu, alisema Kombani na kukata simu.
Kwa mujibu wa Jaji Chande, kamati hizo ngazi ya mkoa huwa chini ya Mkuu wa Mkoa na kati yake huwa Ofisa Tawala wa Mkoa huku mahakimu wakiwa wajumbe, huku katika wilaya pia Mkuu wa Wilaya huwa mwenyekiti na Ofisa Tawala akiwa katibu.
Kila fani ina namna ya kuwajibishana. madaktari wana kamati zao, wanasheria wana kamati zao, basi hata sisi tuwe na chombo chetu, aliongeza Jaji Chande.
Source: Mwananchi
Maoni yangu: Mh. Lissu alilisema sana hili bungeni. Lakini Mh Celina Kombani na mwanasheria mkuu Werema wakagoma kubadilisha. Wabunge wa ccm nao walipohijiwa na speaker walikataa hoja ya Lissu. Sasa Jaji mkuu amelisema, tena anawaambia watu wa nje ya nchi! Ni aibu kwa Tanzania!
Lakini jambo linalonistua ni majibu aliyotoa Celina Kombani alipopigiwa simu na mwandishi wa mwananchi! Kombani anasema " Kamuulize mwenyewe (Jaji Mkuu Chande) yeye si ndiyo amesema hivyo? Basi kamuulize yeye ndiyo anajibu" . Ingekuwa kwa nchi za wenzetu huyu mama angekuwa hana kazi kesho. Majibu gani hayo? Yeye ndiye aliyesimamia hii sheria mbovu, leo anataka jaji mkuu aulizwe nini? Na kama Celina Kombani hana majibu ya kwanini aliona inafaa mahakama kusimamiwa na wanasiasa wa ccm kuna sababu gani? Katiba inasema kuhusu separation of powers, Celina Kombani haelewi hilo?
Akizungumza katika majadiliano na ujumbe wa Mpango wa Hiari wa Kujitathmini Kiutawala Bora Afrika (APRM) jijini Dar es Salaam jana, Jaji Chande, alisema licha ya kuwepo kwa uhuru wa Mahakama, bado kitendo cha kamati za maadili za mahakimu kuwa chini ya viongozi wa Serikali, kinakwaza uhuru wa muhimili huo wa dola.
Uhuru wa Mahakama ni suala muhimu katika kutekeleza kazi zake, nchi nyingi za Afrika zimeshafikia uhuru huo, hata hapa kwetu lakini kuna suala moja tu ambalo linatukwaza.
Aliongeza; Kuwepo kwa viongozi wa mikoa na wilaya kwenye kamati za maadili za mahakimu, inapunguza uhuru wa Mahakama. Ingefaa kamati hizo ziwe chini ya Tume ya Huduma za Mahakama.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Utawala Bora, Mathias Chikawe alipotafutwa kwa simu, ili kuzungumzia hoja hiyo ya Jaji Chande, hakupatikana licha ya simu yake kuita kwa muda mrefu.
Kwa upandeb wake Waziri wa Sheria na Katiba, Celina Kombani alipoulizwa kuhusu kauli hiyo ya Jaji Mkuu alisema; Kamuulize mwenyewe (Jaji Mkuu Chande) yeye si ndiyo amesema hivyo? Basi kamuulize yeye ndiyo anajibu, alisema Kombani na kukata simu.
Kwa mujibu wa Jaji Chande, kamati hizo ngazi ya mkoa huwa chini ya Mkuu wa Mkoa na kati yake huwa Ofisa Tawala wa Mkoa huku mahakimu wakiwa wajumbe, huku katika wilaya pia Mkuu wa Wilaya huwa mwenyekiti na Ofisa Tawala akiwa katibu.
Kila fani ina namna ya kuwajibishana. madaktari wana kamati zao, wanasheria wana kamati zao, basi hata sisi tuwe na chombo chetu, aliongeza Jaji Chande.
Source: Mwananchi
Maoni yangu: Mh. Lissu alilisema sana hili bungeni. Lakini Mh Celina Kombani na mwanasheria mkuu Werema wakagoma kubadilisha. Wabunge wa ccm nao walipohijiwa na speaker walikataa hoja ya Lissu. Sasa Jaji mkuu amelisema, tena anawaambia watu wa nje ya nchi! Ni aibu kwa Tanzania!
Lakini jambo linalonistua ni majibu aliyotoa Celina Kombani alipopigiwa simu na mwandishi wa mwananchi! Kombani anasema " Kamuulize mwenyewe (Jaji Mkuu Chande) yeye si ndiyo amesema hivyo? Basi kamuulize yeye ndiyo anajibu" . Ingekuwa kwa nchi za wenzetu huyu mama angekuwa hana kazi kesho. Majibu gani hayo? Yeye ndiye aliyesimamia hii sheria mbovu, leo anataka jaji mkuu aulizwe nini? Na kama Celina Kombani hana majibu ya kwanini aliona inafaa mahakama kusimamiwa na wanasiasa wa ccm kuna sababu gani? Katiba inasema kuhusu separation of powers, Celina Kombani haelewi hilo?