Jaji mstaafu Warioba unayakana maneno yako mwenyewe au ndiyo agenda ya kuvunja Muungano?

Jaji mstaafu Warioba unayakana maneno yako mwenyewe au ndiyo agenda ya kuvunja Muungano?

Jabirimakame

Member
Joined
Jan 15, 2014
Posts
71
Reaction score
37
Mwenyekiti wa Tume ya Katiba, Jaji Mstaafu Joseph Warioba, katika mahojiano yake na gazeti la Raia Mwema, toleo la 209 la Agosti 26,2011, alinukuliwa akisema

““Suala la Muungano pia liwe katika Katiba. Tusipokuwa makini kwa maneno yanayozungumzwa sasa tutavunja Muungano. Muungano huu una misingi yake na upo kwa manufaa ya wananchi. Tufafanue manufaa hayo ni nini kwa mwananchi wa kawaida.Wakati wote kwa mwananchi wa kawaida, kumekuwa hakuna matatizo ya Muungano. Matatizo yanatoka kwenye midomo ya viongozi. Shughuli za wananchi wa kawaida haziangalii orodha ya mambo ya Muungano, bali haki yao kama raia. Wanajiona ni raia katika shughuli zao za kibiashara au nyingine. Mwananchi wa kawaida anaona anayo haki ya kufanya biashara mahali popote. Wananchi wamezoa hivyo. Msiwafikishe mahali wakajiona kuwa kwenda Zanzibar au kuja Bara inabidi wafuate taratibu za kwenda Kenya au Uganda” .

Jaji Joseph Warioba aliendelea kusema “Tunayo matatizo ya madaraka, kwamba unazo Serikali mbili kwa hiyo yale yaliyomo kwenye orodha ya Muungano ni kuonyesha Serikali hii ina madaraka gani. Wanagombania madaraka. Kama suala ni mafuta au mengine tuzungumze. Inategemea mnavyokubaliana, tusije kuongeza au kupunguza kwenye orodha mambo ambayo yatakuja kuwatenganisha wananchi. Kama kwa mfano, kuna watu wanafikiri kuimarisha Muungano ni kuwa na serikali tatu, unaimarishaje?

Sasa hivi kiini ni ugomvi wa madaraka kati ya Serikali ya Muungano na Serikali ya Zanzibar. Hivi ukileta serikali tatu, ugomvi huu hautakuwapo? Ukileta Serikali ya Tanganyika yenyewe haitadai madaraka? Mwisho wataomba madaraka hadi Serikali ya Muungano isiwe na chochote. Hivi Serikali ya Tanganyika kwa mfano ikawapo, ikataka iwe na wimbo wake wa Taifa, bendera yake, nembo yake, kisha inadai ifanye biashara ya nje, unafikiri tutakuwa tumefika wapi? Ni kwamba tutakuwa tunaondoa Muungano na kurudisha Tanganyika na Zanzibar. Lakini kama wananchi wanataka hivyo, sawa. Lakini tukivunja Muungano madhara yake ni makubwa sana kwa pande zote mbili. Mimi naamini wale wanaotaka serikali tatu wanajua nia yao ni kuvunja Muungano na huu ndio ukweli. Ukianzisha serikali tatu, maana yake unavunja Muungano”.


UKIANZISHA SERIKALI TATU MAANA YAKE UNAVUNJA MUUNGANO.
 
Kwa upande mmoja siwezi kuwalaumu wazanzibar kwani waonavyo wao nchi yao ni ndogo na wanafikiri au kuwaza watakapokuwa peke yao ni rahisi sana kupata maendeleo ya haraka,ukilinganisha na bara nchi yetu ni kubwa na watu ni wengi,tukijumuishwa nao basi maendeleo yanakuwa ya polepole mno na mpaka kuona kwamba tunawaibia haki zao za msingi za kuendelea.Na bila kuangalia tatizo siyo ukbwa wa nchi au wingi wa watu bali ni ULAFI uliopitiliza wa viongozi wetu wa pande zote mbili bila kujali imani za za dini,makabila yao wala vyama watokavyo,na hawa wanaona bado hawafaidi ipasavyo wanafikiria kuongeza MADARAKA yao zaidi na hili ndilo tatizo.

Tunachotakiwa kukipigia kelele wala si serikali tatu,mbili au moja bali MALIASILI za nchi kutumika vyema ipasavyo,viongozi wala rushwa ,mafisadi na wale waliotumia nafasi zao vibaya wachukuliwe hatua na kweli iwe hivyo kwenye mioyo yetu sisi wananchi na kwenye mioyo ya viongozi wachache waadilifi waliobaki.Vinginevyo naweza kukubaliana na kauli ya Jaji Warioba tunacheza muziki wa wanasiasa na tunawasaidia kupiga ngoma na kuimba.
 
Hayo maneno siyo yangu. Nimefanya quotation.

Jaji Waroba alisema na amekuwa akirudia kila mara kuwa walipokaa kama Tume kila mjumbe alitakiwa kuacha itikadi yake ya chama au msimamo binafsi hivyo makubaliano ya wote ndani ya Tume ndio yaliyofuatwa, zinduka.
 
Toa hoja unautaka muungano wa aina gani na uwe na mfumo gani sio Jaji alisema nini, bado un nafasi ya kutwambia kwa nini muungano na sio serikali moja.
 
Seriali moja , bendera moja, ikulu moja bunge moja nchi moja mbali ya hiyo muungano utakuwa fix tu. WARIOBA HAWEZI KULISEMA HILO ILA ANAPUGIA DEBE JAMBO GUMU LA SERIKALI TATU ULI MUUNGANO UFE. UTAPASHWA KUFA KWA SABABU HAUJUWEPO ULISHAKUFA KITAMBO.
 
Hili ndio gumu zaidi/fix
seriali moja , bendera moja, ikulu moja bunge moja nchi moja mbali ya hiyo muungano utakuwa fix tu. Warioba hawezi kulisema hilo ila anapugia debe jambo gumu la serikali tatu uli muungano ufe. Utapashwa kufa kwa sababu haujuwepo ulishakufa kitambo.
 
labda mtanisaidia kunielewesha, ni hivi...tunaongea sana kuhusu suala la muungano utafikiri ndio essence ya katiba mpya tunayoitaka, mosi. Pili, kiuhalisia watz sasa hatupendani yaan tunu zetu za udugu au tunu za taifa kama sage warioba alivyozitaja zimekufa, juzi juzi tu hapa tumeonesha kufyatuka akili zetu kwa kuuana coz ya udini na mpaka sasa hatujaja na mwarobain wa hiyo kansa. Gap kat ya pobre na rich z at climax..Alafu urafi, rushwa na rasilimali za nchi kuwaneemesha tu viongozi halitatuliwi tu ktk ideal katiba, but from our hearts but til now we hv not proved such conversion. Niandikie..+255759376213
 
Back
Top Bottom