Jaji Mustapha Siyani ataanza upya kusikiliza mapingamizi yaliyomfanya Jaji Elinaza kujitoa au anaendeleaje na kesi?

Jaji Mustapha Siyani ataanza upya kusikiliza mapingamizi yaliyomfanya Jaji Elinaza kujitoa au anaendeleaje na kesi?

Beatrice Kamugisha

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2019
Posts
762
Reaction score
6,984
Upande wa mlalamikaji ulieleza mahakama kwa ushahidi na facts kwamba mashtaka yaliyowasilishwa na Jamuhuri hayapo au hayana nguvu na msingi wa kisheria. Jaji alinaza baada ya kusikiliza pande zote mbili alikubali kuwa hati ya mashtaka ina makosa lakini pamoja na kubaini makosa kwenye hati ya mashtaka hakutaka kuifuta kesi.

Kitendo Cha kukubali kwamba mashtaka yamekosewa lakini hapohapo akaielekeza Jamhuri ikaandae mashtaka upya kilileta picha kwamba yeye Jaji anajua mashtaka sahihi ya mtuhumiwa kitu ambacho nikinyume kabisa na sheria. Jaji apaswi kuelekeza jamhuri ikatafute makosa maana kama Jamhuri ingelikuwa na makosa sahihi walipoletewa pingamizi walipaswa kukubali kwamba hati ina mapungufu na waje na chaji nyingine.

Kama katika kipindi chote Cha uendeshaji mashtaka Jamhuri haikuwahi kuomba ikabadilishe hati ya mashtaka, jaji Elinaza aliielekeza Jamhuri ikarekebishe vipi hati ya mashtaka? Mazingira haya ya Jaji kujielekeza kutoa maamuzi ya hoja kinyume na utaratibu ndiyo yaliyopelekea Mtuhumiwa Mbowe kumwomba ajiondoe.

Je, jaji mpya anakuja kutolea maamuzi hoja za ubovu wa hati ya mashtaka au anakuja kufanya kazi gani? Kama anakuja kuendelea na ushauri wa jaji aliyepita kwa Jamhuri nini nafasi ya Malalamiko ya Mbowe kuhusu maamuzi mabovu yaliyotolewa na Jaji Elinaza?

Ni sahihi kwa mahakama kuelekeza Jamhuri namna yakuandaa mashtaka? Endapo Jamhuri itaelekezwa na Mahakama namna yakurekebisha hati ya mashtaka, je jaji atakapofika hatua ya kutoa hukumu atapingana na ushauri alioutoa?

Maana kitendo Cha jaji kuielekeza Jamhuru ikarekebishe hati ya mashtaka kinaashiria kwamba mahakama tayari inayajua makosa ya mtuhumiwa na imeshajiridhisha kuwa makosa yalitendwa ila tu Jamhuri ilikosea kuyaandaa mashtaka hayo kwa ukakasi huu tutegemee mahakama kutoa Haki wakati imejipa kazi yakushauri mashtaka yaweje?
 
Ni vigumu sana kumkataa Jaji kwenye kesi yako, halafu ukategemea kuwa huyo jaji mwingine atakayeichukua atakuwa tofauti sana na uliyemkataa; wana fraternity yao.

Wakati fatma karume akiwa wakili akueambie kuwa alimkataa hakimu Mingi ni nini kilichofuatia kwa mahakimu wengine waliochukua kesi yake akiwemo Mahai, Lyamuya na wengine waliiendesha vipi. Wakaili nzuri huwa hashambulii credibility ya mahakimu, hilo hufanywa na mawakili wa harakati tu ambao kwa kiasi kikubwa interests zao kubwa ni kumtangaza mteja kwenye umma badala ya kumnasua mteja kutoka kwenye kibano cha sheria.
 
Line ya Kwanza ulipaswa kusema mlalamikiwa maana kesi ya jinai mlalamikaji Ni Jamhuri

Lakini umeuliza maswali mazito Sana, Jaji Elinaza katika uamuzi wake aliwachana Jamhuri wazi kwamba haiwezekani wao wakaelewa au kusoma fikra za wanadamu hasa pale Jamhuri ilipokiri kwamba watuhumiwa awakukaa kikao chochote kile lakini eti wakatuhumiwa kuwa na common intention ya kutenda Ugaidi. Hasa Kama Jamhuri inakiri watuhumiwa awajawahi kukaa kikao chochote Cha pamoja face to face au kupitia njia ya mtandao je, leo wanapoambiwa wakaandae upya charge watakuja kuieleza mahakama watuhumiwa walikaa kikao?

Jaji mpya anapaswa kuyapitia upya mapingazi yaliyopelekea Jaji kujitoa maana mapingamizi Yale yalilenga kuiomba mahakama ifute kesi hii. Naamini hata Kama yataandaliwa mashtaka upya Upande wa mlalamikiwa wataweka pingamizi na kuiomba mahakama irejee utetezi uliotolewa na Jamhuri awali.

Mfano: Kama Jamhuri ilieleza mahakama kwamba watuhumiwa awakukaa kikao then kesho kutwa wakaja na mashtaka yanayoeleza kwamba watuhumiwa walikaa kikao Basi walalamikiwa wataomba mahakama irejee kauli ya mawakili kwenye ujibuji wa hoja za awali na hapo itathibitika kwamba Jamhuri ilidanganya mahakama.
 
Line ya Kwanza ulipaswa kusema mlalamikiwa maana kesi ya jinai mlalamikaji Ni Jamhuri

Lakini umeuliza maswali mazito Sana, Jaji Elinaza katika uamuzi wake aliwachana Jamhuri wazi kwamba haiwezekani wao wakaelewa au kusoma fikra za wanadamu hasa pale Jamhuri ilipokiri kwamba watuhumiwa awakukaa kikao chochote kile lakini eti wakatuhumiwa kuwa na common intention ya kutenda Ugaidi...
Endeleeni kujitekenya na kucheka wenyewe, yajayo yanafurahisha...
 
Jaji mpya anaendelea kesi ilipoishia, Jamhuri wataleta mashtaka mapya kama yana kasoro Kibatala ataweka pingamizi tena, na hata akishinda hilo pingamizi itaishia Jamhuri kufanya marekebisho tu, hakuna kesi itakayo ondolewa kwa minor mistakes za charge sheet.
 
Ni sahihi kwa mahakama kuelekeza Jamhuri namna yakuandaa mashtaka? Endapo Jamhuri itaelekezwa na Mahakama namna yakurekebisha hati ya mashtaka, je jaji atakapofika hatua ya kutoa hukumu atapingana na ushauri alioutoa? Maana kitendo Cha jaji kuielekeza Jamhuru ikarekebishe hati ya mashtaka kinaashiria kwamba mahakama tayari inayajua makosa ya mtuhumiwa na imeshajiridhisha kuwa makosa yalitendwa ila tu Jamhuri ilikosea kuyaandaa mashtaka hayo........kwa ukakasi huu tutegemee mahakama kutoa Haki wakati imejipa kazi yakushauri mashtaka yaweje?
Mkuu 'Beatrice', hiyo aya uliyoandika hapo ni ngumu sana.

Na pia itakuwa ngumu sana kwa huyu Jaji mpya kuendelea kusikiliza kesi ambayo mtangulizi wake tayari amekwishaona kwamba hati ya mashtaka ina makosa. Ataendelea vipi kusikiliza kesi ambayo tayari hati yake ya mashtaka imekosewa?

Au wewe una maana ya kwamba Jaji mpya hatalazimika kuona hayo mwenzake aliyoyaona?

Kwa hiyo akina Kibatala na wao wataanza upya kabisa, kuleta lile pingamizi lao la mwanzo kuhusu uwezo wa mahakama hiyo kuisikiliza kesi hiyo?

Mbona huu utakuwa mzunguko wa ajabu sana!
 
Upande wa mlalamikaji ulieleza mahakama kwa ushahidi na facts kwamba mashtaka yaliyowasilishwa na Jamuhuri hayapo au hayana nguvu na msingi wa kisheria. Jaji alinaza baada ya kusikiliza pande zote mbili alikubali kuwa hati ya mashtaka ina makosa lakini pamoja na kubaini makosa kwenye hati ya mashtaka hakutaka kuifuta kesi. Kitendo Cha kukubali kwamba mashtaka yamekosewa lakini hapohapo akaielekeza Jamhuri ikaandae mashtaka upya kilileta picha kwamba yeye Jaji anajua mashtaka sahihi ya mtuhumiwa kitu ambacho nikinyume kabisa na sheria. Jaji apaswi kuelekeza jamhuri ikatafute makosa maana kama Jamhuri ingelikuwa na makosa sahihi walipoletewa pingamizi walipaswa kukubali kwamba hati ina mapungufu na waje na chaji nyingine. Kama katika kipindi chote Cha uendeshaji mashtaka Jamhuri haikuwahi kuomba ikabadilishe hati ya mashtaka, jaji Elinaza aliielekeza Jamhuri ikarekebishe vipi hati ya mashtaka? Mazingira haya ya Jaji kujielekeza kutoa maamuzi ya hoja kinyume na utaratibu ndiyo yaliyopelekea Mtuhumiwa Mbowe kumwomba ajiondoe.

Je, jaji mpya anakuja kutolea maamuzi hoja za ubovu wa hati ya mashtaka au anakuja kufanya kazi gani? Kama anakuja kuendelea na ushauri wa jaji aliyepita kwa Jamhuri nini nafasi ya Malalamiko ya Mbowe kuhusu maamuzi mabovu yaliyotolewa na Jaji Elinaza?

Ni sahihi kwa mahakama kuelekeza Jamhuri namna yakuandaa mashtaka? Endapo Jamhuri itaelekezwa na Mahakama namna yakurekebisha hati ya mashtaka, je jaji atakapofika hatua ya kutoa hukumu atapingana na ushauri alioutoa? Maana kitendo Cha jaji kuielekeza Jamhuru ikarekebishe hati ya mashtaka kinaashiria kwamba mahakama tayari inayajua makosa ya mtuhumiwa na imeshajiridhisha kuwa makosa yalitendwa ila tu Jamhuri ilikosea kuyaandaa mashtaka hayo........kwa ukakasi huu tutegemee mahakama kutoa Haki wakati imejipa kazi yakushauri mashtaka yawej
A very good analysis/narration. BRAVO
 
Jaji mpya anaendelea kesi ilipoishia, Jamhuri wataleta mashtaka mapya kama yana kasoro Kibatala ataweka pingamizi tena, na hata akishinda hilo pingamizi itaishia Jamhuri kufanya marekebisho tu, hakuna kesi itakayo ondolewa kwa minor mistakes za charge sheet.
Sijui una maana gani na "minor mistakes" kwenye kesi nzito kama hii ya ughaidi!

"minor mistakes"? ya kuweka vituo kwenye sentensi, au kuosea jia la mtuhumiwa? au ni zipi hizo unazozifikiria wewe?

Kwamba Jamhuri walisahau kutaja vituo vya mafuta vilivyokuwa vimepangwa kulipuliwa?

Kwamba mshtakiwa wa nne ilitakiwa kiasi cha pesa kilichotolewa kiwe zaidi ya hicho kinachodaiwa alitoa?

Kwamba mikutano iliyofanywa na washtakiwa sehemu mbalimbali wakipanga njama za ughaidi inapaswa ieleze kiubagaubaga yaliyozungumzwa kati yao?

Jamhuri ikirekebisha haya, bado utaona ni "monor mistakes"? Ilikuwaje wakasahau kuyanyoosha maelezo awali, hadi walelekezwe ndiyo ionekane kuna kesi nzito!

Unamwambia mtu aliyeko jela na ambaye hatma ya kesi hata kama ni ya kubambikiza hukumu ya maisha yake jela itakuwa miaka kadhaa, halafu umwambie marekebisho ni "minor mistakes"? HAKI hapo iko wapi?
 
Upande wa mlalamikaji ulieleza mahakama kwa ushahidi na facts kwamba mashtaka yaliyowasilishwa na Jamuhuri hayapo au hayana nguvu na msingi wa kisheria. Jaji alinaza baada ya kusikiliza pande zote mbili alikubali kuwa hati ya mashtaka ina makosa lakini pamoja na kubaini makosa kwenye hati ya mashtaka hakutaka kuifuta kesi. Kitendo Cha kukubali kwamba mashtaka yamekosewa lakini hapohapo akaielekeza Jamhuri ikaandae mashtaka upya kilileta picha kwamba yeye Jaji anajua mashtaka sahihi ya mtuhumiwa kitu ambacho nikinyume kabisa na sheria. Jaji apaswi kuelekeza jamhuri ikatafute makosa maana kama Jamhuri ingelikuwa na makosa sahihi walipoletewa pingamizi walipaswa kukubali kwamba hati ina mapungufu na waje na chaji nyingine. Kama katika kipindi chote Cha uendeshaji mashtaka Jamhuri haikuwahi kuomba ikabadilishe hati ya mashtaka, jaji Elinaza aliielekeza Jamhuri ikarekebishe vipi hati ya mashtaka? Mazingira haya ya Jaji kujielekeza kutoa maamuzi ya hoja kinyume na utaratibu ndiyo yaliyopelekea Mtuhumiwa Mbowe kumwomba ajiondoe.

Je, jaji mpya anakuja kutolea maamuzi hoja za ubovu wa hati ya mashtaka au anakuja kufanya kazi gani? Kama anakuja kuendelea na ushauri wa jaji aliyepita kwa Jamhuri nini nafasi ya Malalamiko ya Mbowe kuhusu maamuzi mabovu yaliyotolewa na Jaji Elinaza?

Ni sahihi kwa mahakama kuelekeza Jamhuri namna yakuandaa mashtaka? Endapo Jamhuri itaelekezwa na Mahakama namna yakurekebisha hati ya mashtaka, je jaji atakapofika hatua ya kutoa hukumu atapingana na ushauri alioutoa? Maana kitendo Cha jaji kuielekeza Jamhuru ikarekebishe hati ya mashtaka kinaashiria kwamba mahakama tayari inayajua makosa ya mtuhumiwa na imeshajiridhisha kuwa makosa yalitendwa ila tu Jamhuri ilikosea kuyaandaa mashtaka hayo........kwa ukakasi huu tutegemee mahakama kutoa Haki wakati imejipa kazi yakushauri mashtaka yaweje?
Hakuna mahakama hapo hayo ni matawi ya CCM
 
Back
Top Bottom