Jaji Warioba ambeba JK

Jaji Warioba ambeba JK

abdulahsaf

JF-Expert Member
Joined
Aug 31, 2010
Posts
858
Reaction score
130
MWENYEKITI wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba, ametoa ufafanuzi kuhusu hotuba ya Rais Jakaya Kikwete aliyoitoa usiku wa mwaka mpya na kuzungumzia mchakato wa katiba unaoendelea, na kusema rais hapaswi kulalamikiwa kwani yote aliyosema yamo ndani ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba.

Jaji Warioba alitoa kauli hiyo kujibu kauli ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), iliyomlalamikia Rais Kikwete kuingilia kazi za Tume ya Mabadiliko ya Katiba.

Jaji Warioba alitoa ufafanuzi huo jana katika mkutano wake na waandishi wa habari wakati akizungumzia tathmini ya kazi ya kukusanya maoni binafsi ya wananchi kupitia mikutano iliyomalizika Desemba 19 mwaka jana.

"Kuna kitu gani kipya alichosema rais? Yote aliyosema yapo kwenye Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, na mimi katika mikutano yangu yote nimeyaeleza na hakuna asiyejua," alisema Jaji Warioba ambaye ameshawahi kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Waziri Mkuu na Makamu wa Rais.

"Rais alielezea mchakato wote kuanzia kukusanya maoni, kuandaa rasimu, kufanyika kwa mabaraza ya katiba, Bunge maalum la katiba na kura ya maoni…haya yote yapo kwenye sheria ambayo wabunge waliipitisha," alisema Jaji Warioba wakati akijibu swali la mwandishi wa habari Jabir Idrissa aliyetaka kujua kauli ya tume kuhusu maoni ya baadhi ya wanasiasa kuwa rais aliingilia kazi zake.

"Hivi ingekuwaje kama rais angetoa salamu za Mwaka Mpya bila kuzungumzia mchakato muhimu kwa nchi kama huu wa katiba?" alihoji Jaji Warioba.

Akizungumzia mikutano ya kukusanya maoni iliyomalizika mwezi uliopita, Jaji Warioba alisema kazi hiyo ilianza Julai 2 mwaka jana na Tume yake imetembelea na kufanya mikutano 1,776 katika mikoa yote 30 ya Tanzania Bara na Zanzibar.

Kwa mujibu wa Jaji Warioba, jumla ya wananchi 1,365,337 walihudhuria mikutano hiyo na kati yao, 64,737 walitoa maoni kwa kuzungumza katika mikutano na wengine 253,486 walitoa kwa maandishi katika mikutano hiyo.

Alisema takwimu hizi hazijumuishi maoni yanayoendelea kukusanywa na tume yake kupitia posta, totuvi ya tume, mitandao ya kijamii na ujumbe mfupi wa simu za mkononi ambao hadi kufikia jana walipokea sms 16,261.

Kuhusu idadi ya wananchi waliojitokeza mikutanoni na kutoa maoni yao, mwenyekiti huyo alisema tume imeridhika na idadi hiyo na kufafanua kuwa kilichokuwa kinatafutwa ni hoja na kwamba haukuwa wakati wa kupiga kura.

Jaji Warioba alifafanua kuwa, katika awamu zote nne za mikutano ya kukusanya maoni, wananchi wametoa maoni kuhusu maeneo yote muhimu kama utawala, haki, maadili na mamlaka yao na mengineyo.

Akizungumzia hatua inayofuata, Jaji Warioba alisema kuwa kuanzia Jumatatu, tume hiyo itaanza kukutana na makundi mbalimbali kwa lengo la kukusanya maoni yao kuhusu katiba mpya.

Makundi hayo ni vyama vya siasa; vyama vya kitaaluma; asasi za kiraia; taasisi za kidini, vyama vya wafanyakazi, wakulima, wafanyabiashara na makundi mengine mbalimbali.

[TD="bgcolor: #ffffff"]
Mwenyekiti-na-Katibu-wa-Tume-ya-Mabadiliko-ya-Katiba-Jaji-Joseph-Warioba-na-Assaa-Rashid.jpg



na Mwandishi wetu

[/TD]
[TD="width: 140, bgcolor: #ffffff"][/TD]
 
- rais wa jamhuri jk anatakiwa kubebwa na warioba? Are you serious?

Le mutuz

Pale Rais anaposhindwa kujibu hoja au kuwa na kigugumizi katika kutetea hoja au kauli yake hujitokeza waungwana kujibu kwa niaba yake!

Kwa msingi huo anabebwa!
 
- rais wa jamhuri jk anatakiwa kubebwa na warioba? Are you serious?

Le mutuz

Na wewee!

Kwani humjui alivyo dhaifu!
We msomi bwana anza kuongea kwa kuongozwa na elimu yako na kuona kwako mambo mengi....hii kitu ya Ma-CCM acahana nayo!
 
Jaji Warioba kachaguliwa na JK kuwa Mwenyekiti wa Tume ya mabadiliko ya Katiba sasa hapo sijui nani kambeba mwenzake.

Chadema walikurupuka na hoja yao dhaifu eti rais Kikwete atakiwi kusema chochote kuhusu katiba.

John Mnyika, acha kukurupuka ovyo.
 
Last edited by a moderator:
Hata kama Rais Kikwete alimchagua jaji Warioba kuwa mwenyekiti wa tume ya katiba,Je hii ni sababu inayomfanya Rais Kikwete kuwa msemaji wa tume?
 
Si ni bosi wake? Atambeza alafu yeye akale wapi?
 
JUMAPILI, JANUARI 06, 2013 08:42 NA BAKARI KIMWANGA, DAR ES SALAAM

*Apinga madai yake dhidi ya Rais Kikwete
*Asema hafanyikazi kwa mashinikizo ya kisiasa

MWENYEKITI wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Tanzania, Jaji Mstaafu Joseph Warioba, amempuuza Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu. Jaji Warioba alisema hana muda wa kubishana na mbunge huyo na kusema kuwa, tume yake haifanyi kazi kwa mashinikizo ya kisiasa na wala si jukwaa la wanasiasa.

Kauli hiyo ya Jaji Warioba imekuja siku moja baada ya Lissu kumpa siku 14 Rais Jakaya Kikwete, kutoa ufafanuzi kwa nini ameingilia mamlaka ya Tume hiyo kinyume cha sheria.

Lissu pia aliwatuhumu wajumbe wa Tume hiyo kuwa wana kawaida ya kupeleka taarifa kwa Rais Ikulu, zinazohusiana na mwenendo wa kazi za tume, jambo ambalo ni kinyume cha utaratibu.

Katika madai yake Lissu ambaye pia ni Mnadhimu wa Kambi ya Upinzani bungeni, alitishia kuwasilisha hoja binafsi katika mkutano ujao wa Bunge, kupinga hatua hiyo.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Jaji Warioba alisema tume yake haifanyi kazi kwa kushinikizwa na wanasiasa na badala yake waiache ifanye kazi yake.

"Hapa hatufanyi kazi kwa shinikizo la kisiasa, kama yeye analalamikia sheria yeye mwenyewe ni mwanasheria na pia alishiriki kuipitisha bungeni.

"Si dhambi Rais kuizungumzia Katiba katika hotuba yake ya mwaka mpya na kwa hatua hii hakuvunja sheria, kulisemea imekuwa nongwa?

"Mbona vyombo vya habari vinaandika masuala ya tume, ninaomba ieleweke kilichozungumzwa ni kile kile ambacho kila wakati nakisema kwa waandishi hata ratiba yetu ya kazi ipo hivyo.

"Narudia tena hakuna mjumbe wa tume anayefanya kazi kinyume cha sheria, sisi hatufanyi kazi ya siasa ninaomba tuachwe tufanye kazi yetu ya kitaalamu.

"Acheni wanasiasa wafanye siasa na sisi tuacheni tufanye kazi yetu tuliyokabidhiwa jamani," alisema Jaji Warioba.

Kuhusu kukamilika kwa awamu ya kwanza ya ukusanyaji maoni kwa wananchi, Warioba alisema katika awamu hiyo mikoa 30 ilifikiwa na wananchi walitoa maoni yao.

Alisema katika awamu ya nne iliyomalizika Desemba 19, mwaka jana, tume yake ilifanya mikutano 417 katika mikoa sita iliyokuwa imebaki kwenye ratiba.

Jaji Warioba alisema, hadi kukamilika kwa awamu zote jumla ya mikutano 1,776 imefanyika na wananchi milioni 1,365,337 walihudhuria mikutano hiyo ya utoaji maoni ya katiba.

"Mwitikio wa utoaji wa maoni umekuwa wa amani na utulivu na wananchi 64,737 wametoa maoni yao kwa kuzungumza, huku 253,486 wametoa kwa maandishi katika awamu zote nne.

"Simu za mkononi, ukurasa wa Facebook, tovuti na posta mwitikio umeongezeka na jumla ya wananchi 2,587 wametoa maoni yao huku ujumbe mfupi wa simu ukiwa 16,261 uliopokelewa hadi sasa.

"Mbali na mafanikio hayo, Tume ilikabiliwa na changamoto kadhaa kwa wanasiasa kuwaelekeza wananchi aina ya maoni waliyopaswa kutoa katika mikutano," alisema.

Makundi maalumu

Kuanzia kesho Januari 7 hadi Machi mwaka huu, Tume itaanza kukutana na makundi maalumu, kwa lengo la kukusanya maoni yao kuhusu Katiba Mpya.

"Makundi hayo ni pamoja na vyama vya siasa, wafanyakazi, vyama vya kitaaluma, asasi za kiraia, taasisi za kidini, wakulima na wafanyabiashara na makundi mengine.

"Tutafanya kazi hiyo hadi Machi, ambapo tutaanza kuandaa rasimu ya maoni hayo na kuanzia Juni hadi Agosti, itakuwa inajadiliwa na Mabaraza ya wilaya.

"Baada ya mabaraza kujadili kwa kina, tutarejea tena kuandaa rasimu nyingine ambayo tutaiwasilisha katika Bunge maalumu la Katiba Novemba mwaka huu, kabla wananchi kupiga kura ya maoni ya kukubali au kuikataa Katiba Mpya," alisema.
 

WARIOBA atatetea SERIKALI ya CCM sasa HIVI umeona MALIPO yake kwa SIKU kwenye HIYO TUME ya KATIBA?
 
Na wewee!

Kwani humjui alivyo dhaifu!
We msomi bwana anza kuongea kwa kuongozwa na elimu yako na kuona kwako mambo mengi....hii kitu ya Ma-CCM acahana nayo!

MKUU!

Msomi atakuwa huyu!!!!?? Au unamlinganisha na dada yake??? Hapa mzee wa watu kala hasara. Mtu anaweza kwenda shule lakini asielimike na ndiyo huyu jamaa. Si unaona tangu apate kale ka-ujumbe kule MAGAMBANI kila kukicha ni PUMBA tupu!!!!
 
MWENYEKITI wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba, ametoa ufafanuzi kuhusu hotuba ya Rais Jakaya Kikwete aliyoitoa usiku wa mwaka mpya na kuzungumzia mchakato wa katiba unaoendelea, na kusema rais hapaswi kulalamikiwa kwani yote aliyosema yamo ndani ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba.

Jaji Warioba alitoa kauli hiyo kujibu kauli ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), iliyomlalamikia Rais Kikwete kuingilia kazi za Tume ya Mabadiliko ya Katiba.

Jaji Warioba alitoa ufafanuzi huo jana katika mkutano wake na waandishi wa habari wakati akizungumzia tathmini ya kazi ya kukusanya maoni binafsi ya wananchi kupitia mikutano iliyomalizika Desemba 19 mwaka jana.

"Kuna kitu gani kipya alichosema rais? Yote aliyosema yapo kwenye Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, na mimi katika mikutano yangu yote nimeyaeleza na hakuna asiyejua," alisema Jaji Warioba ambaye ameshawahi kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Waziri Mkuu na Makamu wa Rais.

"Rais alielezea mchakato wote kuanzia kukusanya maoni, kuandaa rasimu, kufanyika kwa mabaraza ya katiba, Bunge maalum la katiba na kura ya maoni…haya yote yapo kwenye sheria ambayo wabunge waliipitisha," alisema Jaji Warioba wakati akijibu swali la mwandishi wa habari Jabir Idrissa aliyetaka kujua kauli ya tume kuhusu maoni ya baadhi ya wanasiasa kuwa rais aliingilia kazi zake.

"Hivi ingekuwaje kama rais angetoa salamu za Mwaka Mpya bila kuzungumzia mchakato muhimu kwa nchi kama huu wa katiba?" alihoji Jaji Warioba.

Akizungumzia mikutano ya kukusanya maoni iliyomalizika mwezi uliopita, Jaji Warioba alisema kazi hiyo ilianza Julai 2 mwaka jana na Tume yake imetembelea na kufanya mikutano 1,776 katika mikoa yote 30 ya Tanzania Bara na Zanzibar.

Kwa mujibu wa Jaji Warioba, jumla ya wananchi 1,365,337 walihudhuria mikutano hiyo na kati yao, 64,737 walitoa maoni kwa kuzungumza katika mikutano na wengine 253,486 walitoa kwa maandishi katika mikutano hiyo.

Alisema takwimu hizi hazijumuishi maoni yanayoendelea kukusanywa na tume yake kupitia posta, totuvi ya tume, mitandao ya kijamii na ujumbe mfupi wa simu za mkononi ambao hadi kufikia jana walipokea sms 16,261.

Kuhusu idadi ya wananchi waliojitokeza mikutanoni na kutoa maoni yao, mwenyekiti huyo alisema tume imeridhika na idadi hiyo na kufafanua kuwa kilichokuwa kinatafutwa ni hoja na kwamba haukuwa wakati wa kupiga kura.

Jaji Warioba alifafanua kuwa, katika awamu zote nne za mikutano ya kukusanya maoni, wananchi wametoa maoni kuhusu maeneo yote muhimu kama utawala, haki, maadili na mamlaka yao na mengineyo.

Akizungumzia hatua inayofuata, Jaji Warioba alisema kuwa kuanzia Jumatatu, tume hiyo itaanza kukutana na makundi mbalimbali kwa lengo la kukusanya maoni yao kuhusu katiba mpya.

Makundi hayo ni vyama vya siasa; vyama vya kitaaluma; asasi za kiraia; taasisi za kidini, vyama vya wafanyakazi, wakulima, wafanyabiashara na makundi mengine mbalimbali.

[TD="bgcolor: #ffffff"]
Mwenyekiti-na-Katibu-wa-Tume-ya-Mabadiliko-ya-Katiba-Jaji-Joseph-Warioba-na-Assaa-Rashid.jpg



na Mwandishi wetu
[/TD]
[TD="width: 140, bgcolor: #ffffff"][/TD]

Jaji warioba lazima alambe miguu bwana. Hizo milioni kwa siku angezipata wapi kama sio kulipa fadhila kwa aliye ,teua??? ndiyo maana tunasema rais apunguziwe madaraka, maana hakuna mteule wake atayempinga. Lazima alambe miguu ya aliye mpa ulajia.
 
MKUU!

Msomi atakuwa huyu!!!!?? Au unamlinganisha na dada yake??? Hapa mzee wa watu kala hasara. Mtu anaweza kwenda shule lakini asielimike na ndiyo huyu jamaa. Si unaona tangu apate kale ka-ujumbe kule MAGAMBANI kila kukicha ni PUMBA tupu!!!!

Hahahaaaa!
Umenipa raha sana kamanda!
 
- rais wa jamhuri jk anatakiwa kubebwa na warioba? Are you serious?

Le mutuz



Mkuu Le mutuz,
SIKU ZOTE SERIKALI SI WATU/MTU BALI NI MAANDISHI (SHERIA) AMBAZO NDIZO TUNAZIFUATA.ALICHOKISEMA MZEE WARIOBA NI UTHIBITISHO WA KISHERIA JUU YA KAULI YA MH. RAIS,KATIKA HILI MZEE WARIOBA AMETUMIA TAALUMA YAKE KUJIBU HOJA AMBAZO MH. RAIS ASINGEWEZA KUZUJIBU KISHERIA IKIZINGATIWA KUWA RAIS SI MWANASHERIA.
 
mkuu le mutuz,
siku zote serikali si watu/mtu bali ni maandishi (sheria) ambazo ndizo tunazifuata.alichokisema mzee warioba ni uthibitisho wa kisheria juu ya kauli ya mh. Rais,katika hili mzee warioba ametumia taaluma yake kujibu hoja ambazo mh. Rais asingeweza kuzujibu kisheria ikizingatiwa kuwa rais si mwanasheria.

na kwa sababu si mwanasheria ndiyo maana alitoa kauli zinazo pingana na sheria ya kuanzisha tume ya kuchukuwa maoni ya kuandika katiba mpya. Pamoja na yote, bado jaji warioba ameamua kukariri kile alicho sema aliyemteua (bosi wake). Kitu ambacho ni kinyume na sheria iliyo anzisha tume hii. Au kwa sababu ni jaji basi munamuona kwamba yeye hakosei au kumlinda aliye mpa kibarua? Hata hivyo inajulikana wazi kwamba jaji warioba anaibeba ccm. Maana kila linalo lalamikiwa na wananchi yeye analipinga. Kwa maana kwamba yeye ndio kila kitu. Hivyo anatupa mashaka makubwa kwamba, katiba itakayo patikana itakuwa si ya watanzania bali ya wale wenye kutaka maslahi yao yalindwa.
 
Back
Top Bottom