Jakaya Kikwete: Tusiweke 'takataka’ kwenye maoni ya Katiba mpya

Jakaya Kikwete: Tusiweke 'takataka’ kwenye maoni ya Katiba mpya

MwanaDiwani

JF-Expert Member
Joined
Mar 22, 2013
Posts
5,536
Reaction score
2,266
MWENYEKITI wa Taifa wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Jakaya Kikwete amesema ili nchi iwe na umoja, kuna umuhimu wa mchakato wa kutoa maoni ya kuandikwa kwa Katiba mpya, ufanyike kwa umakini.

Alisema hayo mjini hapa jana, wakati akifungua kikao cha cha Baraza la Katiba la CCM ngazi ya Taifa, ambapo kikao hicho kinahudhuriwa na Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya chama hicho (NEC).

“Kama tutaingiza takataka katika kutoa maoni, tutavuna takataka katika kupata Katiba mpya,” alisema Rais Kikwete katika hotuba yake hiyo.

Rais Kikwete alisema iwapo wajumbe wa NEC, watafanya kazi hiyo kwa umakini mkubwa, nchi itaendelea kuwa katika hali ya utulivu na mshikamano.

Alisema kama kazi hiyo itafanyika vizuri, kutakuwa na nchi yenye utulivu; na ikifanyika vibaya, kwa kuingiza takataka, hata matokeo yake yatakuwa ni takataka.

“Ni lazima kuhakikisha kazi hii, inafanyika kwa utulivu ili nchi iendelee kuwa na umoja,” alisema. Alisema anapenda kuona kila mmoja, anatoa hoja na kuacha kupiga kelele; na hata wale wanaokosoana, wafanye hivyo taratibu. “Kila mmoja atoe hoja, aache kupiga kelele, mkosoane kwa utaratibu, mjumbe usiibue usichokitaka, eleza kile unachokitaka na ukijengee hoja,” alisema.

Alisema wengine walikuwa ni wajumbe kwenye mabaraza yaliyopita na sasa wapo; na kutaka watoe miongozo; na kila mmoja asione haya, kutoa yale anayofikiria yatasaidia.

“Nasisitiza tuvumiliane, wengine wanaweza kuwa na mawazo tofauti. Kwani mtu akitoa mawazo yake, usiyoyapenda, usipige kelele kwa kuwa tusipokuwa makini, hatutakuwa tunajadili Katiba, bali tutakuwa tunapiga kelele,” alisema Rais Kikwete.

Pia, alisema vyama vya siasa vimepata fursa kama taasisi, vitoe maoni ya rasimu ya katiba; na kazi inayofanya na NEC ni kutengeneza utaratibu mzuri wa namna ya kuingiza mawazo ya wanachama wa CCM kwenye rasimu ya Katiba.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akitoa taarifa yake, alisema kuna jumla ya mabaraza ya Katiba 18,879 ya CCM, ambapo wanachama milioni 2.6 walishiriki kutoa maoni hayo kupitia mabaraza hayo.

Alisema bado maoni kutoka Jumuiya ya Wanawake Tanzania (UWT), ambapo yanaendelea kukusanywa na yanatarajiwa kufikishwa katika Tume ya Mabadiliko ya Katiba, mara kazi hiyo itakapokamilika.

Sakata la Bukoba

Wakati Rais Kikwete akionya juu ya umakini katika Katiba mpya, Kamati Kuu ya CCM imewaita Dodoma viongozi wa chama hicho mkoani Kagera, akiwemo Mbunge wa Bukoba Mjini, Balozi Khamis Kagasheki ambaye pia ni Waziri wa Maliasili na Utalii na Meya wa Manispaa ya Bukoba, Anatory Amani kwa ajili ya mahojiano.

Hatua hiyo inafuatiwa na sakata la kuvuliwa uanachama madiwani wanane wa Manispaa ya Bukoba. Katika mkutano wake na waandishi wa habari jana, Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye alisema viongozi sita wameitwa kwa ajili ya mahojiano hayo mjini Dodoma.

Licha ya viongozi hao kuitwa, Nnauye alisema hatma ya Mwakilishi wa Kiembe Samaki kupitia CCM, Mansour Himid Yusuf ipo mikononi mwa NEC iliyokaa kuanzia jana.

Alitaja walioitwa mjini Dodoma kwa ajili ya mahojiano kuwa ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kagera, Katibu wa CCM Mkoa, Katibu wa CCM Wilaya ya Bukoba Mjini, Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Bukoba na Meya wa Manispaa ya Bukoba.

Alisema viongozi hao, walitarajiwa kufika mjini Dodoma jana ili kuweza kuonana na Kamati Kuu kwa ajili ya mahojiano zaidi. Nnauye alisema Kamati Kuu baada ya kushughulikia sakata la Madiwani wa Bukoba, limeamua kuwaita Dodoma viongozi hao na wanatakiwa kufika Dodoma kuonana na Kamati Kuu leo kwa ajili ya mahojiano.

Hata hivyo, alisema baadhi ya viongozi hao, wakiwemo Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kagera wapo Mjini Dodoma, wakiendelea na kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM. “Baada ya mahojiano na viongozi hao Kamati Kuu itatoa taarifa ya hatua zaidi dhidi ya sakata hilo la madiwani,” alisema.

Sakata la kuvuliwa madaraka kwa madiwani wanane wa CCM wa Manispaa ya Bukoba ilileta sintofahamu kutokana na CCM taifa kupinga kitendo hicho.

Madiwani hao wanatajwa kuwa ni Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Bukoba, Yusuph Ngaiza ambaye ni Diwani wa Kata ya Kashai, Diwani wa kata ya Kitendagulo, Samwel Ruangisa, Diwani wa Viti Maalum Murungi Kichwabuta, Diwani wa kata ya Nyanga, Deusdedith Mutakyawa na Diwani wa kata ya Miembeni, Richard Gaspar ambaye pia ni Naibu Meya.

Wengine ni Diwani wa kata ya Buhemba, Alexander Ngalinda, Diwani wa kata ya Hamugembe, Robert Katunzi pamoja na Diwani wa Kata ya Ijunganyondo, Dauda Kalumuna.

Kuvuliwa udiwani kwa viongozi hao, kulipingwa, kutokana na waliofanya hivyo walikiuka kanuni na taratibu za Katiba. Kutokana na hali hiyo, Nnauye aliwataka madiwani hao kuendelea na kazi hadi hatua zaidi, zitakapochukuliwa na Kamati Kuu itakapokutana.

Mvutano huo wa kisiasa, baina ya Kagasheki na Amani unadaiwa kutishia kukigawa chama hicho mkoani Kagera, hali iliyofanya CCM ngazi ya taifa kuingilia kati suala hilo.
[video=youtube_share;G6_PyJm4IIE]http://youtu.be/G6_PyJm4IIE[/video]

Chanzo: Habarileo.
 
MWENYEKITI wa Taifa wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Jakaya Kikwete amesema ili nchi iwe na umoja, kuna umuhimu wa mchakato wa kutoa maoni ya kuandikwa kwa Katiba mpya, ufanyike kwa umakini.

Alisema hayo mjini hapa jana, wakati akifungua kikao cha cha Baraza la Katiba la CCM ngazi ya Taifa, ambapo kikao hicho kinahudhuriwa na Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya chama hicho (NEC).

"Kama tutaingiza takataka katika kutoa maoni, tutavuna takataka katika kupata Katiba mpya," alisema Rais Kikwete katika hotuba yake hiyo.

Rais Kikwete alisema iwapo wajumbe wa NEC, watafanya kazi hiyo kwa umakini mkubwa, nchi itaendelea kuwa katika hali ya utulivu na mshikamano.

Alisema kama kazi hiyo itafanyika vizuri, kutakuwa na nchi yenye utulivu; na ikifanyika vibaya, kwa kuingiza takataka, hata matokeo yake yatakuwa ni takataka.

"Ni lazima kuhakikisha kazi hii, inafanyika kwa utulivu ili nchi iendelee kuwa na umoja," alisema. Alisema anapenda kuona kila mmoja, anatoa hoja na kuacha kupiga kelele; na hata wale wanaokosoana, wafanye hivyo taratibu. "Kila mmoja atoe hoja, aache kupiga kelele, mkosoane kwa utaratibu, mjumbe usiibue usichokitaka, eleza kile unachokitaka na ukijengee hoja," alisema.

Alisema wengine walikuwa ni wajumbe kwenye mabaraza yaliyopita na sasa wapo; na kutaka watoe miongozo; na kila mmoja asione haya, kutoa yale anayofikiria yatasaidia.

"Nasisitiza tuvumiliane, wengine wanaweza kuwa na mawazo tofauti. Kwani mtu akitoa mawazo yake, usiyoyapenda, usipige kelele kwa kuwa tusipokuwa makini, hatutakuwa tunajadili Katiba, bali tutakuwa tunapiga kelele," alisema Rais Kikwete.

Pia, alisema vyama vya siasa vimepata fursa kama taasisi, vitoe maoni ya rasimu ya katiba; na kazi inayofanya na NEC ni kutengeneza utaratibu mzuri wa namna ya kuingiza mawazo ya wanachama wa CCM kwenye rasimu ya Katiba.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akitoa taarifa yake, alisema kuna jumla ya mabaraza ya Katiba 18,879 ya CCM, ambapo wanachama milioni 2.6 walishiriki kutoa maoni hayo kupitia mabaraza hayo.

Alisema bado maoni kutoka Jumuiya ya Wanawake Tanzania (UWT), ambapo yanaendelea kukusanywa na yanatarajiwa kufikishwa katika Tume ya Mabadiliko ya Katiba, mara kazi hiyo itakapokamilika.

Sakata la Bukoba

Wakati Rais Kikwete akionya juu ya umakini katika Katiba mpya, Kamati Kuu ya CCM imewaita Dodoma viongozi wa chama hicho mkoani Kagera, akiwemo Mbunge wa Bukoba Mjini, Balozi Khamis Kagasheki ambaye pia ni Waziri wa Maliasili na Utalii na Meya wa Manispaa ya Bukoba, Anatory Amani kwa ajili ya mahojiano.

Hatua hiyo inafuatiwa na sakata la kuvuliwa uanachama madiwani wanane wa Manispaa ya Bukoba. Katika mkutano wake na waandishi wa habari jana, Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye alisema viongozi sita wameitwa kwa ajili ya mahojiano hayo mjini Dodoma.

Licha ya viongozi hao kuitwa, Nnauye alisema hatma ya Mwakilishi wa Kiembe Samaki kupitia CCM, Mansour Himid Yusuf ipo mikononi mwa NEC iliyokaa kuanzia jana.

Alitaja walioitwa mjini Dodoma kwa ajili ya mahojiano kuwa ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kagera, Katibu wa CCM Mkoa, Katibu wa CCM Wilaya ya Bukoba Mjini, Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Bukoba na Meya wa Manispaa ya Bukoba.

Alisema viongozi hao, walitarajiwa kufika mjini Dodoma jana ili kuweza kuonana na Kamati Kuu kwa ajili ya mahojiano zaidi. Nnauye alisema Kamati Kuu baada ya kushughulikia sakata la Madiwani wa Bukoba, limeamua kuwaita Dodoma viongozi hao na wanatakiwa kufika Dodoma kuonana na Kamati Kuu leo kwa ajili ya mahojiano.

Hata hivyo, alisema baadhi ya viongozi hao, wakiwemo Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kagera wapo Mjini Dodoma, wakiendelea na kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM. "Baada ya mahojiano na viongozi hao Kamati Kuu itatoa taarifa ya hatua zaidi dhidi ya sakata hilo la madiwani," alisema.

Sakata la kuvuliwa madaraka kwa madiwani wanane wa CCM wa Manispaa ya Bukoba ilileta sintofahamu kutokana na CCM taifa kupinga kitendo hicho.

Madiwani hao wanatajwa kuwa ni Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Bukoba, Yusuph Ngaiza ambaye ni Diwani wa Kata ya Kashai, Diwani wa kata ya Kitendagulo, Samwel Ruangisa, Diwani wa Viti Maalum Murungi Kichwabuta, Diwani wa kata ya Nyanga, Deusdedith Mutakyawa na Diwani wa kata ya Miembeni, Richard Gaspar ambaye pia ni Naibu Meya.

Wengine ni Diwani wa kata ya Buhemba, Alexander Ngalinda, Diwani wa kata ya Hamugembe, Robert Katunzi pamoja na Diwani wa Kata ya Ijunganyondo, Dauda Kalumuna.

Kuvuliwa udiwani kwa viongozi hao, kulipingwa, kutokana na waliofanya hivyo walikiuka kanuni na taratibu za Katiba. Kutokana na hali hiyo, Nnauye aliwataka madiwani hao kuendelea na kazi hadi hatua zaidi, zitakapochukuliwa na Kamati Kuu itakapokutana.

Mvutano huo wa kisiasa, baina ya Kagasheki na Amani unadaiwa kutishia kukigawa chama hicho mkoani Kagera, hali iliyofanya CCM ngazi ya taifa kuingilia kati suala hilo.

Chanzo: Habarileo.
Toa na maoni yako wewe gamba
 
Toa na maoni yako wewe gamba
"Nazungumza wazi hapa leo, vyama vya siasa ni taasisi, vifuate utaratibu vijadili kama Baraza la katiba la Taasisi na kutuwasilishia maoni yao, sisi Tume hatutachukua maoni ya jukwaani wala ya kwenye helikopta."-Jaji Warioba.
 
Heri Dhaifu ameshtukia takataka maana tunaounga mkono serikali tatu tuliambiwa ni "wazee tunaosubiri kufa" Kwa mtazamo huu wa mwenyekiti wenu Kama ameacha undumilakuwili ina maana kila maoni yatazingatiwa.
 
"Nazungumza wazi hapa leo, vyama vya siasa ni taasisi, vifuate utaratibu vijadili kama Baraza la katiba la Taasisi na kutuwasilishia maoni yao, sisi Tume hatutachukua maoni ya jukwaani wala ya kwenye helikopta."-Jaji Warioba.

Kama agenda ya kuandika Katiba mpya haikutoka CCM na bado M/Kiti wa CCM akalazimika kuanzisha mchakato wa kuandika Katiba mpya, vivyo hivyo pamoja na kujidanganya kwamba "Wananchi" sio Taasisi, wataendelea kulazimika kukubaliana na maoni yatakayo letwa na Helikopta tu!

Inajulikana wazi kwamba CCM na Makada wake wote, hawana kabisa UTASHI wa kuandika Katiba Mpya. Wameamua "KUKUBALIANA KUTO KUKUBALIANA" kutokana na MGANDAMIZO wa NGUVU YA UMMA.

Vinginevyo, wanalazimika kufamu kwamba, kama watatumia nguvu ya DOLA na hatimaye kutupatia Katiba isiyo kidhi matakwa ya waTanganyika, T 2015 CDM itakapo ongoza DOLA ni lazima tuwasukume kuandika Katiba ya waTanganyika na sio Katiba ya wana CCM na MAFISADI wake. Na hapo itakuwa lazima kuweka vipengele vya kuwaadhibu wale wote walio ifikisha Tanganyika hapa ilipo.
 
MTU MMOJA MMOJA KWA WATANZANIA WOTE WAWE NA HAKI YA KUTOA MAONI YAO MAPENDEKEZO YAO WALA NGUVU ZISUMIKE KTK KUMEZA mchakato wa katiba ITAKUWA NI UKANDAMIZAJI TUNATAKA TANZANIA SAFI YAKUWAJIBISHANA wanyonge nao wafaidi TUNU NA NEEMA ZA MUUMBA WAO JUU YA RASIMALI ZA NCHI YAO kuna ubaya gani NCHI IKAWA NA VYAMA VIWILI VYENYE NGUVU VINAVYOPOKEZANA UTAWALA KAMA GERMAN//USA//UK MAISHA YETU NI MIAKA 50 ~80 MIMALI MINGI MPK YA VITUKUU, WHAT THIS!
 
Kama agenda ya kuandika Katiba mpya haikutoka CCM na bado M/Kiti wa CCM akalazimika kuanzisha mchakato wa kuandika Katiba mpya, vivyo hivyo pamoja na kujidanganya kwamba "Wananchi" sio Taasisi, wataendelea kulazimika kukubaliana na maoni yatakayo letwa na Helikopta tu!

Inajulikana wazi kwamba CCM na Makada wake wote, hawana kabisa UTASHI wa kuandika Katiba Mpya. Wameamua "KUKUBALIANA KUTO KUKUBALIANA" kutokana na MGANDAMIZO wa NGUVU YA UMMA.

Vinginevyo, wanalazimika kufamu kwamba, kama watatumia nguvu ya DOLA na hatimaye kutupatia Katiba isiyo kidhi matakwa ya waTanganyika, T 2015 CDM itakapo ongoza DOLA ni lazima tuwasukume kuandika Katiba ya waTanganyika na sio Katiba ya wana CCM na MAFISADI wake. Na hapo itakuwa lazima kuweka vipengele vya kuwaadhibu wale wote walio ifikisha Tanganyika hapa ilipo.
Chunguzi mbali mbali zimefanyika lakini hazijagundua sababu hasa inayomfanya binadamu kuota ndoto, laiti kama tungekuwa tunafahamu sababu yake nafikiri bandiko lako hili lingepata majibu mbadala.

Ndiyo hao hao wanaofanya mikutano ya hadhara inayochukua masaa chini ya mawili huku kila msemaji akichukua less than 30 minutes kuhutubia wakati Rasimu ya Katiba ina soft copy kurasa 107 na pia ina ibara 240. This is more than a joke!

Ndiyo hao hao walisema watajitoa kwenye mchakato wa katiba huku mashinikizo yao ya kibabe yakigonga mwamba kwa watu ambao walichagua utaifa zaidi ya uchama.

Ndiyo hao hao kwa hofu wanaanza kusoma barua kutoka Tume ya Jaji Warioba kuhusu kuunda mabaraza ya Taasisi kwa sababu ujumbe wa Jaji Warioba kuhusu maoni yanayoandikwa ndani ya helikopta na kwenye mikutano ya hadhara unawatesa.

Ndiyo hao hao wanaofanya siasa za kuvizia without sense of political unambiguous direction.
 
"Nazungumza wazi hapa leo, vyama vya siasa ni taasisi, vifuate utaratibu vijadili kama Baraza la katiba la Taasisi na kutuwasilishia maoni yao, sisi Tume hatutachukua maoni ya jukwaani wala ya kwenye helikopta."-Jaji Warioba.

chopa itakutoa roho mdogo wangu.
 
Kauma agenda ya kuandika Katiba mpya haikutoka CCM na bado M/Kiti wa CCM akalazimika kuanzisha mchakato wa kuandika Katiba mpya, vivyo hivyo pamoja na kujidanganya kwamba "Wananchi" sio Taasisi, wataendelea kulazimika kukubaliana na maoni yatakayo letwa na Helikopta tu!

Inajulikana wazi kwamba CCM na Makada wake wote, hawana kabisa UTASHI wa kuandika Katiba Mpya. Wameamua "KUKUBALIANA KUTO KUKUBALIANA" kutokana na MGANDAMIZO wa NGUVU YA UMMA.

Vinginevyo, wanalazimika kufamu kwamba, kama watatumia nguvu ya DOLA na hatimaye kutupatia Katiba isiyo kidhi matakwa ya waTanganyika, T 2015 CDM itakapo ongoza DOLA ni lazima tuwasukume kuandika Katiba ya waTanganyika na sio Katiba ya wana CCM na MAFISADI wake. Na hapo itakuwa lazima kuweka vipengele vya kuwaadhibu wale wote walio ifikisha Tanganyika hapa ilipo.

Unaona majibu yenu hata madaraka hamjachukua tayari mnataka kuigawa nchi
 
Unaona majibu yenu hata madaraka hamjachukua tayari mnataka kuigawa nchi[/QUOTE]

Kwa hiyo woote wanao iba kuku, au kuto watendea haki wengine makosa yao yana angukia kwenye "KUIGAWA NCHI"?

Hata vitabu vyote vitakatifu vinatuambia kwamba "BAADA YA KIFO NI HUKUMU". Kwani akina Mramba na Yona wamepelekwa mahakamani kwa sababu zipi?
 
"Nazungumza wazi hapa leo, vyama vya siasa ni taasisi, vifuate utaratibu vijadili kama Baraza la katiba la Taasisi na kutuwasilishia maoni yao, sisi Tume hatutachukua maoni ya jukwaani wala ya kwenye helikopta."-Jaji Warioba.

Wewe subiria na wala usiwe mkurupukaji. Approach za CHADEMA katika masuala nyeti kama haya usifanye mchezo nao kabisa. Wewe na Mavuvuzela wenu walio fikia tamati ya kubuni mambo mapya katika siasa zaidi ya POLICCM wata shangazwa.

Kwa akili zenu wewe na MAGAMBA wenzako mnafikiria mambo yataishia kwenye mikutano ya wazi tu!!! Kwa taarifa yako kila siku na kwa saa 24, CHADEMA kama Taasisi wanachama wanaijadili Rasimu ya Katiba.

Hata humu jamvini si unaona michango ya wana CHADEMA? Au mpaka uone Gwanda la CHADEMA ndio ujue kuna mikutano wa wana CHADEMA kujadili Rasimu ya Katiba? Kwa taarifa yako CHADEMA ni MIOYO YA WATANGANYIKA.
 
Hizo takataka ni zipi? Maoni ya watu yanawezaje kuwa takataka? Sheria inayosimamia mchakato wa uundwaji wa katiba mpya inampa kila raia/taasisi haki sawa katika kutoa maoni. Kuita baadhi ya maoni ya watu ni takataka ni uvunjwaji wa sheria hii na dharau kubwa kwa raia ambao mawazo/maoni yao yanatofautiana ama kupingana na huyu ama yule.

Ili mchakato huu uwe huru na wa haki ni lazima watu wavumiliane na kuheshimiana, si kutoa kauli ya namna hii. Lazima sote tukubaliane katika kutokubaliana na kuafikiana. Hii si kauli nzuri masikioni na katika mustakabali wa uundwaji wa katiba mpya. Mungu ibariki Tanzania.
 
Back
Top Bottom