Jamani bado tunaibiwa

Jamani bado tunaibiwa

CalvinKimaro

JF-Expert Member
Joined
Sep 11, 2017
Posts
245
Reaction score
314
Kilo ya korosho pale airport departure lounge inauzwa karibu Tshs.20000. Kampuni ya Ali Baba ya China inatangaza bei ni dola 10 kwa kilo. Hii ni baada ya kuongeza flavors. 3000 bado tunaibiwaaaaaa!!!!! Hebu jeshi bangueni uzeni wenyewe China mtuambie!!! Ila naona mafioso mbele! Watasusa korosho yetu kutukomoa. Ila tuwe masikini jeuri. Baada ya muda wenye makampuni China watakuja wenyewe! Huu ndio wakati muafaka mawaziri wapya kuonyesha wanaweza! Kaongeeni na makampuni uchina!
 
Airport ya wapi mkuu wananunua kwa hiyo bei niwashitue wana ntwara
 
Kitu ambacho watu hawaelewi na hawaeleweshwi pengine kwa makusudi ni kwamba Korosho inayouzwa Tsh 3,000/= ni ile ghafi

Ni ile ambayo haijatengwa na majani/uchafu, ni ile ambayo hiajabanguliwa, ni ile ambayo haijakaangwa, ni ile ambayo haijawekwa kwenye pakiti n.k
 
Unajua gharama ya kubangua korosho, na usafirishaji??
 
Mtoa mada ni mpotoshaji, uliza kwanza ujue hiyo ya 3000 ni ipi na ya 20000 ni ipi
 
Kupata kilo moja ya korosho ni lazima uwe na kilo 3 za korosho ghafi ambazo zitakugharimu shilingi 9,000 + usafiri + vibarua + gharama za kubangua + packing material + faida
 
Back
Top Bottom