Me bado siamini kama upon
Kwa muktadha huu, Basi huna mvuto wa kitu chochote, hata nyota yako haing'ai kabisa, achilia mbali kuwaka tu, imezima tokea tumboni mwa mzazi wako. nasema hivi mimi ni mchawi asilia!
Asili ya sisi wachawi ni wivu wa kupindukia dhidi ya watu maarufu wenye mvuto wa Mali, Elimu kubwa, Biashara, Uongozi/Utawala, Umiliki wa mambo Makubwa, wenye Talents zao na kauli nzito ktk jamii.
Hawa ni lishe Bora sana kwetu sisi wachawi, na tuna waonaga tangia tumboni, mwa Mama zao. ikibidi tuna haribu hizo mimba mapemaa tena maksudi, Kwa kufanya hivi tuna pandishwa cheo na kuongezwa nguvu zaidi!
Ogopa sana mtu anaye itwa Mkuu wa wachawi! na wengi wa hawa wanaongoza Makanisa Makubwa na Misikiti leo hii! na wafuasi wa makanisa hawajui wengi ni kama wewe! wenye uwezo wa kuwatambua ni kama sisi! siyo makanisa yote! ni baadhi tu!
Lkn ni hatari kuharibu hizi mimba kutokana na asili na nyota ya mtu mwenyewe! ndo maana wengine tunawasubiri huku huku Duniani! na ikitokea tuki kuweka alama tu,utosini, popote uendako utaonwa na kutambuliwa na wachawi wenzetu tu!
Hao ndiyo wanatakiwa kuumizwa ili wasifikie malengo yao, yaani watu wenye hizo sifa ni chakula cha wachawi, kwa kuwaroga na kuwaua wanapata nguvu za kiuchawi, na kupanda cheo!
Ukiona hujawahi kuumizwa au kutafutwa na wachawi jua kwamba huna hayo mambo, hapo juu, wewe ni una nyota yenye njaa kali hawawezi kushiba na hutakaa ujue wachawi maisha yako yote!
Hata ikitokea ukaununua uchawi hautakaa ukakukubali! zaidi utaishia kuanguka na ungo tu! kukamatwa kwenye mageti ya watu wenye kinga, kushikwa na vichwa vya watu, wakati unakatiza na wenzako!. kucharangwa mapanga!
Jiunge na makanisa ya Kizungu ukatoe zaka na sadaka yako huko, au slimu ndo njia pekee kwako. ili uishi kwa kujichanganya. hata huko kanisani utaona wenzako wanatolewa majini kila leo, lkn wewe no. labda ni kupe mfano rahisi,
Ndgu yako mwenye pesa ndiyo watu wa familia/ukoo watamiminika kwenda kwake kupata maisha bora mara kwa mara kuliko Maskini, au mwenye maisha ya kawaida,
Awali ya yote wanajisikia sifa kusimulia kwa wenzi wao, kumtembelea ndg yao mwenye Kighorofa mjini, ila wewe hutakaa uone ndg akija kwako hata ukiwa lazimisha. '' njooni mnitembelee bwana''!!!!!
sababu huna mvuto wa chakula kizuri, nyumba nzuri, pa kulala pazuri, gari huna waje kupata shida? na mwenye nyota dhaifu ikitokea umesoma kidogo hutapata kazi nzuri, kila unapo karibia barabara ya mafanikio, njia inafurika maji!
Nyota ya mtu ni jambo halisi tangia zama, Kumbuka Mamajusi Mashariki walikuja kumsifu Yesu walipoona nyota yake! iking'aaa!