Jamani hawa ma last born watatupasua vichwa!

Bishanga

JF-Expert Member
Joined
Jun 29, 2008
Posts
15,321
Reaction score
10,075
Wazazi wenzangu jamani hebu tujuzane,nyie ma last born wenu mna wa handle vipi.Wa kwangu yaani pasua kichwa,homework kufanya kwa mbinde,nguo ndo hivo anavaa zimejikunja,ukiingia chumbani mwake utadhani ni Kandahar,chakula ale sahani aache hapo,anachofikiria yeye ni video games,kucheza mpira,sinema,ili mradi basi tu. Toto kubwa la miaka 12 mpaka leo linalialia,yaani.
Na mamemba humu ambao na ninyi ni ma last born hebu nipeni experience ya makuzi yenu,mahusiano yenu na wazazi na kaka/dada zenu yalikuwaje wakati mnakua? pliz pliz tell me something.
 
Mhhh malezi yako nayo yanachangia mkuu
Kama ulimlelea kumdekeza hawezi kubadilika kwa muda mfupi
Kaa nae mfundishe na mpe masuala ya maisha maana ni muda mfuipi ujao ataenda boarding school na ni nani atamfulia na kumuoshea sahani zake
Na hizo game na video shuleni ataziona wapi
Mkunje mapema bado mdogo
Mimi ni last born ila sina hizo aise na wala sikupata malezi ya kudekezwa na wazazi
 
mimi ni last born na niko vizuri tu wa kulaumiwa hapo ni nyie wazazi kwani hayo magame kayaokota si mmempa wenyewe jamani.
mlee mtoto kwa njia nzuri bwana wala hataicha hadi atakapokuwa mzee
 
Mkuu ilikuwa mijeledi kwa kwenda mbele? mambo magumu sana haya aisee.
 
mimi ni last born na niko vizuri tu wa kulaumiwa hapo ni nyie wazazi kwani hayo magame kayaokota si mmempa wenyewe jamani.
mlee mtoto kwa njia nzuri bwana wala hataicha hadi atakapokuwa mzee

sasa naanza kuhisi nyie ma last born mnaanza kujipanga mjitetee,ngoja tusubiri waje wazazi wengine na mamemba wengine ambao ni watoto wa kati,kisha tuta compare na kukontrast notisi.
 
Mkuu ilikuwa mijeledi kwa kwenda mbele? mambo magumu sana haya aisee.

Mkuu ilikuwa ni mapambano kwa kwenda mbele hakuna cha kusema mimi ni last born
Kwa malezi ya sasa kwa mtoto mjeledi una nafasi yake ila sometimes hausaidii na sana sana unamfanya awe sugu na ahisi kwamba oprion ya mwisho uliyo nayo kama mzazi ni mjeledi na anakuwa sugu wa hiyo mijeledi
Nafikiri malezi ya kukaa na mtoto kuongea nae maana kwa umri wake ashajua ni kipi anapaswa kufanya na kipi hapaswi kufanya na mpe ukweli kuwa kuna life baada ya baba na mama ambalo linakuja mbele yake
Ataenda shule atakumbana na watu ambao hawakulelewa kudekezwa watamfanya aione shule mbaya na huko sasa ndo ana chance kubwa ya kufanya madudu ambayo kwako wewe itakuwa ni balaa kama mzazi
 
sasa naanza kuhisi nyie ma last born mnaanza kujipanga mjitetee,ngoja tusubiri waje wazazi wengine na mamemba wengine ambao ni watoto wa kati,kisha tuta compare na kukontrast notisi.

Sidhani kama tunapanga kujitetea maana tungelelewa na magame na video na kuacha vyombo mezani baada ya kula na kutojua hata kufua nguo zetu tusingekuwa hapa kwa sasa
Walifanya kazi inavyopaswa na ndo maana tuna hili life la sasa
 
Mmh! Mbona even me ni last born! Nilikua mtukutu thosedayz,lakini ukikua unaachana na habari za kulala kwa zizi la ng'ombe!naamini akikua ataacha ila mjenge kiroho maana kwa nguvu zako kulea hutoweza bila msaada wa mungu!
 
Fimbo kidogo hua unatembeza inapostahili? Manake nyie wa mjini ati hamchapi wanenu
 
Sidhani kama tunapanga kujitetea maana tungelelewa na magame na video na kuacha vyombo mezani baada ya kula na kutojua hata kufua nguo zetu tusingekuwa hapa kwa sasa
Walifanya kazi inavyopaswa na ndo maana tuna hili life la sasa

Unajua Rocky binadamu tunazaa miili hatuzai roho,watoto wa nyumba moja wanakua na kuwa viumbe tofauti utadhania walikutana barabarani, ndo mana wakati mwingine kulea inakuwa ni pata potea,mwingine anachapa mwingine hachapi,mwingine anamjaza ma toy mwingine anamnyima kabisa,mwingine anampeleka boarding akiwa mdogo sana mwingine anasema huendi kokote hadi umalize form six.Mzazi yupi yuko sahihi na yupi hayuko sahihi is hard to tell sana sana uta judge kwa kuangalia final product ambayo ni what kind of a person mtoto ame turn into katika adulthood.
ndugu yangu ukiona asubuhi asubuhi nimeamka na thread kama hii we jua ni frustrations,sometime you need a place ya kutafuta solace,jf mojawapo.
 
Fimbo kidogo hua unatembeza inapostahili? Manake nyie wa mjini ati hamchapi wanenu

nina watoto wengi tu na wengine wamekwishamaliza chuo wanafanya kazi,i have never in my life picked a mjeledi na kumchapa mwanangu.
Utotoni wewe ulichapwa? unadhani ilikusaidia? maishani mwangu sijawahi kuchapwa na baba wala mama yangu(RIP wote wawili).Bakora nilikung'utwa shule,tena sa ingine zile za kupigwa vidole na mgongo wa rula na sidhani kama zilikuwa zinanisaidia lolote.I abhore violence ndo mana hata wanawake zangu huwa siwapigi,wakiniudhi nina namna yangu ya kuwaadhibu.
 

I understand bro and kwa mzazi najua nini maana ya hilo unalosema
Hata wewe mwenyewe ukiangalia malezi mliyolelewa pale nyumbani na wazazi wako yako tofauti sana na upendeleo ulikuwa unaonekana wazi
Kitu kimoja ambacho huwa naamini ni kuwa mshirikishe Mungu katika kila hatua ya mtoto wako anayokua
Na kabla ya kwenda hata kuongea nae masuala ya maisha muombe Mungu akujalie hekima na akufundishe kile unachopaswa kuongea na mtoto wako maana unaweza kujikuta unaharibu badala ya kutengeneza
 
B' umejiuliza ile kwa ukweli kabisa nafasi yako wewe kwa yeye kua alivo sasa??
Maana kama video games ndo anapenda, kucheza mpira but responsibilities
hataki, mie naona hizo ndo zingekua weapons za kumweka katika mstari...
 

kitu muhimu sana hicho umeshauri,thanks for the thought.Siku zote wazazi tunatamani wanetu wakue wawe na mafanikio,tuna toil,tunaamka usiku kuwapeleka shule,tunafuatilia home work zao,kwa hiyo ina frustrate unapoona katoto wala hakaelewi yaani kanakuwa kapo kapo tu na ku take for granted.
 
B' umejiuliza ile kwa ukweli kabisa nafasi yako wewe kwa yeye kua alivo sasa??
Maana kama video games ndo anapenda, kucheza mpira but responsibilities
hataki, mie naona hizo ndo zingekua weapons za kumweka katika mstari...

kumnyima sio? yataka moyo,huwa unajisikiaje mwanao anapokuomba kitu tena kwa upole kabisa....mummy please naomba nicheze kidogo...don't you melt inside?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…