Jamani hawa ma last born watatupasua vichwa!

leo nimegundua kweli majority mmu wanafagilia kuchapa watoto,yaani...hasa ukizingatia mi napinga hilo.

mimi siamini mtoto anarekebishika kwa kuchapwa. Kuna adhabu ukimpa mwenyewe lazma anyoke.
Wakati nipo shule tulikuwa tukiambiwa tuchague fimbo au adhabu tulikuwa tunachagua fimbo maana zitapoa muda huo huo na ni mara moja tu kuliko adhabu zinapoteza muda.
Msipende kuchapa watoto, mtawafanya wawe masugu.
 
hahaha! Yaani bishanga umeamua kunimilikisha kwa tf eeh? Haya bana. Hebu taja matatizo yetu. Najua mafirst born huwa tunapenda tuwe juu. Ni watu wa kutoa maagizo na lazima yafatwe.Mmh!
ukizingatia TF naye ni 1st born pia sasa mtaishije,si itakuwa full mikwaruzano.
by the way (hii ni siri kubwa nakumegea),TF jana nimemwona Namnani na SL,shhhhhhh usiseme.
 

wambie hao kina Avatar,Mzee na Fidel ndo wanafagilia bakora,mi naona na wao utotoni ilikuwa wakikosea kidogo ni mbata kwa kwenda mbele.
btw shule mlikuwa mnachapwa sehemu gani ya kiungo?
 
ukizingatia TF naye ni 1st born pia sasa mtaishije,si itakuwa full mikwaruzano.
by the way (hii ni siri kubwa nakumegea),TF jana nimemwona Namnani na SL,shhhhhhh usiseme.

Mbona baadae nilimuona na BB pale pale au we ulimuona muda gani
 

Mimi binti yangu anakaribia miaka 11 baba yake hajawahi hata kumfokea nini kumchapa, na unajua kwa nini? ni msikivu kila anachoambiwa anaelewa na kutenda vile mzazi anataka. Ana watoto wengine tena chini ya miaka 4 ila anawatandika usipime kwani ni watundu na si wasikivu kwa hiyo kuchapwa kwa mtoto inategemea na mtoto mwenyewe. Mi mwenyewe nimechapwa mpaka namaliza form IV dah wazazi wangu walikua nuksi sio kosa kumchapa mtoto ni njia mojawapo ya kumfundisha.

Inawezekana we bishanga ulikua mtulivu na msikivu kama binti yangu
 
wambie hao kina Avatar,Mzee na Fidel ndo wanafagilia bakora,mi naona na wao utotoni ilikuwa wakikosea kidogo ni mbata kwa kwenda mbele.
btw shule mlikuwa mnachapwa sehemu gani ya kiungo?

Mi fimbo zinaanzia kwa mama mpaka kwa mtoto.
Watoto wa wa kitanzania bila bakora usitegemee tabia nzuri.
 
Kwa hiyo ndio unamlea kijukuu? acha hizo bana

Kuoga tu anambembeleza eti mtoto mzuri nenda kaoge dahh
Kwenda shule anambembeleza nenda shule mwanangu akigoma anamwacha
Wazazi wa kibongo wanaleta malevi ya kizungu kwa watoto wao mwishi wa siku tunapata watoto wa mitaani, vibaka, wavuta bangi, wabwia unga n.k n.k fatilia hao watoto wenye tabia mbaya mitaani wengi wao wametoka familia bora malezi yao yalikuwa yakinyanya
 
Bwana Bishanga 1. tumia fimbo inapobidi usiache fimbo kabisa. 2. inabidi ajue wazazi wanataka nini na nini hawakitaki. 3. Mpangie muda wa kushughulika na mambo anayoyapenda mueleze na sababu. 4. Kila weekend mpe ratiba ya kuandaa chumba chake then kufua nguo apende asipende ikifika jioni kagua kazi ulizompangia asipotimiza anza na fimbo au mkanye kwa maneno. Ukimsimamia ndani ya wiki moja atanyooka pole sana nawajua hawa tena vivulana vinaa shida kama baba zao (joking)
 
Mi ni last born ila huyo wa kwako umemdekeza sana aisee, ubishi hadi kufanya homework?? Nilikuwa siendi kucheza hadi nimalize kazi, huyo wa kwako we unashindwa nini kumpangia ratiba?? Sikuambii uwe unamchapa chapa ila akileta ubishi muweke bakora. Achana na mambo ya haki za binadamu, dini yenyewe inakuruhusu kumuadhibu mtoto kwa bakora makalioni endapo unaona hakusikii. Atakuozea huyo shauri yako, 12 analialia??? Utamrekebisha lini na sasa hivi ndo anakua?
 
Kwetu mi wa mwisho jamani ila mbona ni mgumu sana kuliko hao ndugu zangu walionitangulia!
 

Mhhh! Haya bwana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…