Jamani huu ni utapeli au???

madameA

JF-Expert Member
Joined
Oct 22, 2012
Posts
435
Reaction score
176
Hodi humu ndani!

Jamani week iliyopita nilipigiwa simu (namba naihifadhi) ikinitaja kwa jina langu, ikiniuliza kama nilishawahi kuomba sponsorship ubalozi wa Belgium, na kama bado niko shule au nilishamaliza.

Mimi kwa sasa ni kweli ninasoma masterz kwenye chuo kimojawapo hapa nchini, na ni kweli huko nyuma kabla sijaamua kujilipia mwenyewe, niliomba sponsorship (Belgium sponsorship) wengi najua mnazifahamu lakini sikupata(Hazikutolewa kabisa). Na pia nilishawahi kuingia kwenye web page ya belgium embassy na kuacha details zangu including namba ya simu nikionesha nia ya uhitaji wa sponsorship.

Hivyo nahisi huyo mtu alitoa details zangu huko. Hata hivyo nilimjibu aliyenipigia simu kuwa ni kweli, nilishwahi kuomba na bado niko shule. Akaniambia nitume admission letter + certificates kupitia emails ambazo alinitumia (EMAIL nazihifadhi). Nikafanya hivyo. Hiyo ilikuwa Ijumaa iliyopita.

Siku ya pili yake (Jumamosi) akanipigia simu kuwa nime-qualify kupata sponsorship, hivyo natakiwa kutuma dollar 50 kupitia M-PESA, ili niweze kutumiwa fomu. Akaniambia namba atakayonipa kwa ajili ya kutuma hela ni ya Mhasibu wao.

Nikamwambia kwanza siwezi kutuma hela kwenye M-PESA kwa sababu zifuatazo:
(1) Nitapata wapi risiti ya malipo nitakayofanya,
(2) Siwezi kutuma malipo ya kiofisi kwenye namba ya mtu binafsi, otherwise anitumie form inayoonesha account namba ya ofisi ambayo malipo hayo yanatakiwa yafanyike.
Pia nilimwambia nataka nifike ofisini, ili nipate maelezo zaidi. Akaniambia atanipangia appointment.
from that day hakunipigia tena na mm sijamtafuta. Tukio hili limetokea last week.

Jamani huu kweli sio utapeli???!!! au kama kuna mtu anajua chochote kuhusu issue hii anijuze.
 
Ulitoa majibu sahihi kabisa malipo yoyote ya kiofisi lazima yaambatane na risiti au form zinazotambulika kiofisi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…