Jamani kuna mwanamke kanitumia hili shairi nimjibu kivipi? Nawaombeni ushauri wenu

Jamani kuna mwanamke kanitumia hili shairi nimjibu kivipi? Nawaombeni ushauri wenu

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Joined
Feb 3, 2009
Posts
42,872
Reaction score
34,363
NIPENDE HIVI NILIVYO


nipende hivi nilivyo sinambie nibadili
ili niwe utakavyo,nikuridhi yako hali
penda nywele nilonazo,kama nimefunga shungi
sinambie nende nazo,saluni kupaka rangi.
mama kocho kanizaa,ndizo nywele nilonazo
hizi sitii chokaa,ondoa hayo mawazo
na rangi nilozaliwa,nyeusi siibadili
madawa kujichubuwa,mambo hayo sikubali
kifua changu kisawa,mola kaniumba kike
sendi kabisa kutiwa,ya feki nikabandike
midomo yangu kamili,imetulia mororo
kwanini niibadili,sioni yake kasoro
kama tumbo huliridhi,bwana njia iongoze
usinitie maradhi,ati tumbo nipunguze?
niengeze makaliyo,nitie palastiki
yananini nilonayo?hata nikatie feki?
aliniumba muweza,kwa vile yeye ajua
umbo linonipendeza,siendi kujiumbua
mola wangu yakahara,kasema kwenye kitabu
kaniumba umbo bora,kwanini nijiharibu
kama unataka niwe,ndotoni unavyoota
unipendae si mie endelea kutafuta
kama kazi yarabana,kwako wimbo wa marimba
mimi mbona sijaona ,wakwako ulomuumba
kasoro hwishi kutoa,mara lile mara hili
na wewe zimekujaa,hako kiumbe kamili
sura wapenda ya rashida, inakutia wazimu
makalio ya tilda na umbo la mariamu.
wacha wako ubinafsi,kutaka kujiridhisha
kwangu hapana nafasi,nilivyo nimejitosha
na kina dada wenzangu,nyote ninakuonyeni
kaa ushukuru mungu,maumbo alokupeni
hakuna haswaaa kiliko,alokikosea mungu
katika fikira zako akitengeza mzungu?
upungufu wa akili,uchache wa kufikiri
ni haswa ipi shughuli,ilomshinda kahari
acha kujikata kata,kwengine kujiengeza
kujibandika matuta,na kwengine kupunguza,
jishauwe na maringo,ulivyo unapendeza
jua apendae chongo,huapa kuwa kengeza
 
Nakupa yako pongezi, kupenda utamaduni. Hilo ndilo jema penzi, na si sifa ya kihuni. Kupenda uwe muwazi, na sikulalia saluni. Weka wazi sifa zako, siwe aibu ndoani. Sifa yetu wanaume, kuteseka ni fahari. Mwanamke asiseme, nakupenda kwa hiyari. Utamwambia ukome, Si sifa ya mtu mwari. Weka wazi sifa zako, siwe aibu ndoani. Najua utamaduni, kwako umeshiba sana. Kusemea uwanjani, si vyema kwa msichana. Subiria kwa chumbani, Kwenye ndoa kukutana. Vizuri kupendwa wewe. Ukipenda utachoka.
 
swadaktaaaaa...wana malenga endeleeni jamani..........
 
Nakupa yako pongezi, kupenda utamaduni. Hilo ndilo jema penzi, na si sifa ya kihuni. Kupenda uwe muwazii, na sikulalia saluni. Weka wazi sifa zako, siwe aibu ndoani. Sifa yetu wanaume, kuteseka ni fahari. Mwanamke asiseme, nakupenda kwa hiyari. Utamwambia ukome, Si sifa ya mtu mwari. Weka wazi sifa zako, siwe aibu ndoani. Najua utamaduni, kwako umeshiba sana. Kusemea uwanjani, si vyema kwa msichana. Subiria kwa chumbani, Kwenye ndoa kukutana. Vizuri kupendwa wewe. Ukipenda utachoka.
1.Ushikwapo shikamana, maneno ya tangu zama
Utunze kama amana,ukeshe ukitazama
Uweke yako dhamana,ingawa ya tangu zama
Penzi kweli kikohozi, haliwezi kufichika.

2.Penzi kweli kikohozi, haliwezi kufichika
Siweke mengi mapozi, mwenzio nimeshikika
Sipeleke kwa mulozi,nitazidi kuchizika
Penzi kweli kikohozi, haliwezi kufichika.
 
Nakupa yako pongezi, kupenda utamaduni.
Hilo ndilo jema penzi, na si sifa ya kihuni.
Kupenda uwe muwazi, na sikulalia saluni.
Weka wazi sifa zako, siwe aibu ndoani.

Sifa yetu wanaume, kuteseka ni fahari.
Mwanamke asiseme, nakupenda kwa hiyari.
Utamwambia ukome, Si sifa ya mtu mwari.
Weka wazi sifa zako, siwe aibu ndoani.

Najua utamaduni, kwako umeshiba sana.
Kusemea uwanjani, si vyema kwa msichana.
Subiria kwa chumbani, Kwenye ndoa kukutana.
Vizuri kupendwa wewe. Ukipenda utachoka.

Nimelipanga tu!
 
kwa hiyo alikutumia wewe ili shairi ili?...manake nilivyolisoma linaonekana ni shairi la kuwaasa wanawake wenzie... wala halihitaji jibu kwa sababu halijaandikwa kama swali!...na sidhani kama wanawake wengi wamelipenda hili shairi sababu ni ukweli mtupu
 
Back
Top Bottom