Jamani nimefurahishwa na Pride Tanzania

jaani nilivyoeleweshwa ni kwamba Pride hii imeamua kuingia mpaka vijijini kwa kutumia kampuni yake tanzu iitwayo PRIDE (T) RURAL FINANCE WINDOW hii ni kwa wakulima ambao in normal sense hawawezi kukopeshwa na other financial institutions kama banks kwani awa hawana dhamana kama ardhi iliyopimwa wala nyumba za maana na kwa kilimo cha kuanzia 300000 ni kubwa sana kwani mi mwenyewe
shamba nimekodi sh 15000
kulima sh 30000 trecta kwa ekari
gharama za mbegu ni 1 kg =3000 sasa nimetumia kilo 6 =18000
kupalilia=15000
mbolea ukipenda =20000
kupalilia tena 15000
kuvuna =15000 kwa ekari
storage=1000 kwa gunia kwa mwezi ili usubiri bei ipande
gharama za jumla=128000 sasa ongeza na zusafiri labda 50000 utakuta unabakia na kiasi kikubwa tu cha kukulinda piga picha ukiuza gunia moja 35000 kwa bei ya shambani huku unagunia 35-40 kwa ekari utakuwabado hujajikomboa tu?
 
ujasiriamali ni pamoja na kuwa na moyo wa kuthubutu na kuwa na mawazo ya kushinda
 

Kwa sisi wakulima kwa mnyumbulisho huu tunakuelewa, mimi nasema ili kujikomboa mtu inabidi aanzie pale anapoweza, kwa hiyo laki tatu yako ukiweza kuisimamia vizuri na eka moja ikakupa gunia 20 za kuuza na hizo zingine urudishe mkopo wa Pride utakuwa umepata vitu viwili kwa pamoja.

Moja, umeanza kilimo kwa kuthubutu kwa vitendo, japo ni eka moja. Safari ni hatua mkuu songa mbele. Pili utapata uzoefu kupitia shamba lako hilo, na usiache kujifunza kila siku.

Nakutia moyo, mimi nilianza na kuku mmoja na jogoo kwa jirani, usiniulize ninao wangapi sasa.
 
riba yake ni asilimia 2.5 kwa mwezi ila nimependezwa na mikopo ya kilimo marejesho siyo kwa wiki inategemea na zao unalolichukulia na ukuaji wake halafu vigezo vyake ni nafuu

Hiyo 2.5% per month unajua ni sawa na 30% per year kwa hyo utatakiwa kuregesha 390,000/= ni riba kubwa saaaana ndugu, na huwajui Pride Tanzania wewe watakuzalilisha balaa yaani kama wamekwambia marejesho ni siku furani hauna wanakuaja kusomba kila kitu nyumbani kwako yaani hao ni noma nakwambia usione wamekupa mkopo kiurahisi sikiliza mziki wake
 
Wacha uongo, dawa gani hiyo?
au MAJIVU?
 
kwa hiyo afanyaje?
 
Riba ya 2.5% kwa mwezi ni sawa na 34.49% kwa mwaka compounded au 30% non-compounded, hii ni riba kubwa sana, sio mkopo wa akili huo.
 

uchambuzi mzuri. Mikopo ya pride inaanzia laki 2 na kuendelea. Inategemea na malengo ya mkopaji. Na wakopaji wengi wa pride ni wajasiriamali wadogowadodo ambao naweza kusema ni wale wa pembezoni ambao serikali haijui ifanye nini nao
 
Naomba kufahamu iwapo pride wanatoa mikopo kwa mtu mmoja bila ya kujiunga kikundi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…