Jamani ukipenda Ua basi penda na boga lake


Labda Bacha ataelewa sasa maana mbishi kama nini
 
Kwa hisia hii yamekukuta pole. Ila haya maneno yamuingie Bacha na ubishi wake

sasa jamani ndugu wasiongee kabila lao,
eti kwakuwa shemeji yao haelewi hicho kiluga?
huyo mwanamke si aliolewa akijua kabisa ameolewa kwenye kabila gani,
sasa leo hao shemeji zake kuongea kiluga inamkwaza vipi?
 
oraiti Dina,sasa unamwambiaje huyo bwana
awafukuze hao ndugu au,
kwani yawezekana wapo pale kwa mahitaji mbalimbali,
shule, ugonjwa n.k.

Niseme wafukuzwe ili wote wanitenge na kutaka kuniua? Kama alivyosema mdau mmoja, wape nyavu za kuvulia kaka sio samaki ambaye ushamuunga na viungo vyote! Mimi ninachojiuliza hao vijana ulikuwa nao siku zote au wanahamia na nguo moja moja kwenye mfuko mpaka makabati yanajaa? Bacha usije ukafikiri mie 'mpalestina' sana when it comes to ndugu wa mume, hapana, bali sipendi watu wafanye nyumbani kwangu ghetto! Na hii ina-apply kote, hata kwa ndugu zangu mwenyewe, tena hao ndio sitaki lawama kabisa. Ninao wadogo wanne ambao wote nimehangaika nao mwenyewe, lakini wakiwa kwa mzazi wao (mama, ambaye nashukuru mungu kwa uwepo wake). Na sijawahi kuongezewa ada hata punje na baba mwenye nyumba, lakini kuweka kambi kwangu hapana, unless kuna shida maalum, coz sitaki pia kumkwaza mwenzangu.
 
sasa jamani ndugu wasiongee kabila lao,
eti kwakuwa shemeji yao haelewi hicho kiluga?
huyo mwanamke si aliolewa akijua kabisa ameolewa kwenye kabila gani,
sasa leo hao shemeji zake kuongea kiluga inamkwaza vipi?

Mmh, Bacha, mie nna mashaka unatuchochea ili uone moshi wetu, nimekustukia.
 

Unajua Dina sio kwamba naweza kukuona wewe ni mpalestina,
hapana , hata kidogo!tunajaribu kushea aideas hapa ili tuone maisha kwa ujumla tunayafanya yawe ya furaha kwa kiasi gani,
Naelewa kabisa kuwa maisha yetu ya kitanzania yanafanana sana, extended families!
yawezekana kwako ikawa ngumu sana kuihi na ndugu lakini kwa mwingine kukawa hamna namna ni lazima awe nao!!!!
Hii ni kutokana na mifumo yetu ya kimaisha kwa ujumla!

sasa, hebu angalia hii!wazazi wamefariki,
vijana walikuwa wanasomeshwa na mzee,
wewe kaka mkubwa angalau unakipato fulani, na automatically utayabeba hayo majukumu!
unaonaje basi hao ngugu 2, au 3 wakija kwako waendelee na shule na wengine ,
kuwatengenezea misingi ya maisha yao?
ukizingatia kimbilio la mwisho ni kwako!!!
 
Mmh, Bacha, mie nna mashaka unatuchochea ili uone moshi wetu, nimekustukia.

Hapana Dina,
usihofu hivyo,
BTW: Hii ni mitizamo tu ya maisha tuliyonayo na haiwezi kufanana!!!lakini maisha yanasonga!!!
 
sasa jamani ndugu wasiongee kabila lao,
eti kwakuwa shemeji yao haelewi hicho kiluga?
huyo mwanamke si aliolewa akijua kabisa ameolewa kwenye kabila gani,
sasa leo hao shemeji zake kuongea kiluga inamkwaza vipi?

Bacha wewe lazima utakuwa kabila fulani hivi sitaki kulitaja
Maana unatetea uongee kilugha wewe na wadogo zako mkeo hasikii hivi utajisikiaje kweli
Mimi nampenda mke wangu siwezi kumtenda haya kamwe
 
Bacha salamu mkuu,

Ukimwona King'asti mwambie babu alikuwa anamuulizia!

Na daughter pia.
 
Labda Bacha ataelewa sasa maana mbishi kama nini

hapana mkubwa,
sio kwamba mimi ni mbishi kwenye hili,
naelewa kabisa udhia uliopo kwa kuishi na ndugu kwangu,
lakini kaka kuna majukumu mengine ni mazito na hayakwepeki!labda uamue kuwa kauzu tu!!!!!!!
 

Bacha hivi leo una nini lakini hebu ngoja nisome PM nitarudi
 
sasa jamani ndugu wasiongee kabila lao,
eti kwakuwa shemeji yao haelewi hicho kiluga?
huyo mwanamke si aliolewa akijua kabisa ameolewa kwenye kabila gani,
sasa leo hao shemeji zake kuongea kiluga inamkwaza vipi?

Na wewe bacha sijui lengo la mada yako ni nini! mbona kama un-provoke ili usikie hasira za watu? Kuongea kilugha haikatazwi, ila muwe na kiasi bwana, fikiria wewe ndg zako wamekuja mnaongea kilugha muda wooote no kiswahili, halafu mnacheeeka we unafikiri mkeo ambaye haelewi lugha hiyo atafikiriaje. Kama ni jambo la kawaida kwanini msiongee kiswahili ili na mkeo achangie kama kweli unampenda na hamumfichi jambo hapo. Na yeye ndg zake wakija wakiongea lugha yao muda woote na wewe upo hapo wewe utajisikiaje kiukweli kabisa
 
Bacha wewe lazima utakuwa kabila fulani hivi sitaki kulitaja
Maana unatetea uongee kilugha wewe na wadogo zako mkeo hasikii hivi utajisikiaje kweli
Mimi nampenda mke wangu siwezi kumtenda haya kamwe

kwani MLIMAZUNZU nani alikwambia kuwa,
ukiongea kiluga ndo utakuwa humpendi mkeo,
jamani hiyo si ni luga tu ya mawasiliano,
na hasa pale maongezi yanapowahusu hao watumiaji wa hiyo lugha!
 
Bacha salamu mkuu,

Ukimwona King'asti mwambie babu alikuwa anamuulizia!

Na daughter pia.

Alikuwepo kipindi fulani, sasa sijui kaenda wapi tena,
labda kama unamuulizia Dina!!!!!!
nipo nae hapa kwenye kupenda ua na boga lake!!!!!!
 
hapana mkubwa,
sio kwamba mimi ni mbishi kwenye hili,
naelewa kabisa udhia uliopo kwa kuishi na ndugu kwangu,
lakini kaka kuna majukumu mengine ni mazito na hayakwepeki!labda uamue kuwa kauzu tu!!!!!!!

Kuna mtu kasema unataka kuona POVU hautupati ng'ooooooooooo

Yaani uongee kijita/kikurya wakati mie mndegereko sisikii halafu unaona sawa wewe hebu acha kutafuta ubaya wa watu
 
Bacha salamu mkuu,

Ukimwona King'asti mwambie babu alikuwa anamuulizia!

Na daughter pia.

Alikuwepo kipindi fulani, sasa sijui kaenda wapi tena,
labda kama unamuulizia Dina!!!!!!
nipo nae hapa kwenye kupenda ua na boga lake!!!!!!
 
kwani MLIMAZUNZU nani alikwambia kuwa,
ukiongea kiluga ndo utakuwa humpendi mkeo,
jamani hiyo si ni luga tu ya mawasiliano,
na hasa pale maongezi yanapowahusu hao watumiaji wa hiyo lugha!

Acha kuongea maudhi wewe uuongee kilugha mwenzio hasikii unaona raha..............................
 
Kwa hisia hii yamekukuta pole. Ila haya maneno yamuingie Bacha na ubishi wake

Naonaga kwa aunty yangu yani wakija ndugu za mumewe wanalonga kikwao mpaka wanaondoka na mume wake nae anachangia mana anafahamu mkewe si kabila lake ila habadiliki wala kubalisha hao ndugu zake.
Huwa namwonea huruma sana!!..sasa kama huyu akikimbia kujifungia chumbani naona ni bora kuliko kuduwaa na kilugha cha watu.
 

waambie bana! wamezowea hawa!
 

Halafu Bacha anatetea anahitaji msaada huyu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…