Jamani watu wa kiswahili nisaidieni,hii mbona ngumu?

Jamani watu wa kiswahili nisaidieni,hii mbona ngumu?

tabibumtaratibu

JF-Expert Member
Joined
May 29, 2011
Posts
2,414
Reaction score
1,215
Kwenye sarufi kuna kitu kinaitwa VIYEYUSHO,hiv ni vitu gani na aina zake ni zipi?
 
Naomba nijaribu hapo VIYEYUSHO ni KONSONANTI ambazo zinazotamkwa kama IRABU. katika kiswahili kuna aina mbili za VIYEYUSHO navyo ni: "W" na "Y" vipashio hivi viwili katika kutamka huweza kutamkwa kama IRABU. Kipashio "W" hutamka kama IRABU "U" Mfano: "Wanacheza" inatamkwa "Uanacheza" utakubaliana na mimi kama utaweza kutamka vema neno hilo, lakini pia kipashio "Y" kinatamkwa kama IRABU "i" mfano: "Yale" inatamka "iale"Sababu hiyo ndio inayofanya vipashio hivi kuitwa VIYEYUSHO. Vilevile katika lugha ya kiingereza vinaitwa SEMI-VOWEL ambavyo ni "W" na "J" Hii ni kwa mujibu wa uwezo wangu. Sijui kama nimekuelewesha kidogo au nimekuchanganya
 
Naomba nijaribu hapo VIYEYUSHO ni KONSONANTI ambazo zinazotamkwa kama IRABU. katika kiswahili kuna aina mbili za VIYEYUSHO navyo ni: "W" na "Y" vipashio hivi viwili katika kutamka huweza kutamkwa kama IRABU. Kipashio "W" hutamka kama IRABU "U" Mfano: "Wanacheza" inatamkwa "Uanacheza" utakubaliana na mimi kama utaweza kutamka vema neno hilo, lakini pia kipashio "Y" kinatamkwa kama IRABU "i" mfano: "Yale" inatamka "iale"Sababu hiyo ndio inayofanya vipashio hivi kuitwa VIYEYUSHO. Vilevile katika lugha ya kiingereza vinaitwa SEMI-VOWEL ambavyo ni "W" na "J" Hii ni kwa mujibu wa uwezo wangu. Sijui kama nimekuelewesha kidogo au nimekuchanganya
kwahyo Y ni kiyeyusho na pia ni kipashio? Kipashio nacho ni nini?
 
Back
Top Bottom