Jambo hili lilinishangaza sana sikuwa nalifahamu. Wewe je, unalifahamu?

SHIEKA

JF-Expert Member
Joined
Dec 20, 2011
Posts
8,240
Reaction score
4,265
Niliamka na kujisikia mwili wote kama umekakamaa na maumivu ya kichwa kwa mbaali. Nikajishauri niende hospitali haraka.
Daktari akataka nipimwe damu na mkojo.

Damu ilipatikana isipokuwa mkojo. Mtaalamu wa maabara akaniuliza: Hujisikii haja ndogo hata kidogo? Nikamjibu sisikii chochote. Akanipa maelezo yafuatayo: Nenda choo cha kuvuta kwa maji kisha vuta maji halafu uyatezame yanavyotiririka, utapata haja ndogo!

Nikafanya hivo na kweli nikahisi haja ndogo!

Wadau, hii ni saikolojia au bayolojia au ni nini? Tafuta siku ujaribishe uone.
 
Inaitwa 'miziziology'! Kesho ukijikuta umelala nje usije ukadhani ni mathematics!
 
That's reflex action, nj kama ukikaa na mtu anayepiga chafya/ miayo na wewe ukapiga chafya/ muayo.

Ile sauti ya maji kutiririka inasisimua kukufanya utake kutoa haja ndogo.
 
Hata ukinawa mikono kwenywe bomba la maji mkojo lazima upate.
 
Alicheza na akili yako tu, na hiyo ndiyo phychology.

Alishajua shida yako ni kupata haja ndogo; kwa hiyo alichokifanya pale ni kuifanya akili yako ijiandae kukifanya kile unachokihitaji. Kwa kifupi ni kwamba ulipokuwa unaangalia maji yakimiminika akili yako ilishajengwa kisaikolojia kwamba kitakachofuata pale ni kujisikia kupata haja ndogo, kwa hiyo ulichokifanya pale bila wewe mwenyewe kujitambua ni kujenga hisia ya kupokeakitu ambacho unakitarajia - yaani haja ndogo. Hisia hizo ndio ziliifanya ubongo wako upeleke taarifa kwenye kibofu chamko kwamba sasa hivi kuna kitu kinatakiwa kitoke - ambacho definately ndio huo mkojo uliouona.

MAELEZO YANGU YANAWEZA KUHITAJI UFAFANUZI AU MAREKEBISHO ZAIDI, kwa hiyo mwenye kuwa na la ziada atupe darasa...
 
Inaitwa 'miziziology'! Kesho ukijikuta umelala nje usije ukadhani ni mathematics!
Makonsigwa! Hujambo faza? Wacha niogelee kwenye komenti yako maana imenifurahisha mno. Ishukuru sana teknology ya Jamii forums kukuwezesha kutuma komenti ya aina hiyo. Ukiendelea hivyo usishangae ukipigwa ban na Invisible halafu ukasema ni ukatiliology.
 
Last edited by a moderator:
MAELEZO YANGU YANAWEZA KUHITAJI UFAFANUZI AU MAREKEBISHO ZAIDI, kwa hiyo mwenye kuwa na la ziada atupe darasa...
Maelezo mazuri yaliyojikita kwenye sayansi.
 
That's reflex action, nj kama ukikaa na mtu anayepiga chafya/ miayo na wewe ukapiga chafya/ muayo.

Ile sauti ya maji kutiririka inasisimua kukufanya utake kutoa haja ndogo.
Asante Kiranga. Maelezo yako yamezingatia ukweli wa kisayansi.
 
Last edited by a moderator:
Mimi huwa nahesabu moja mpaka kumi, hata kama sikuwa na mkojo kabisa basi huwa unatoka
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…