Anahitaji kupata psychotherapy!Hilo ni jambo la kawaida kwa akina mama wajawazito, akifika miezi 4 au 5 tatizo linaanza kupungua, japo sio kwa wote.
Hata mimi ilishanitokea, wife alikuwa hapendi harufu ya perfume yangu, ikabidi nimuombe anichagulie perfume ambayo haitamkwaza, tukafanikiwa kupita kikwazo hiki.
Akaanza kuchukia mayai ya kukaanga ikabidi nyumba yangu mayai yawe yanachemshwa.
Hii ya mke kutapika akikuona,nimeishuhudia kwa mke wa rafiki yangu.
Mara nyingi ufumbuzi wa tatizo huwa anao yeye mwenyewe.hebu jaribu kumsikiliza usikie yeye anatakaje,huenda ukapata ufumbuzi wa tatizo lake.
Ila usishangae atakapokuambia kwamba ufumbuzi wa tatizo lake ni kumruhusu akakae kwao mpaka ajifungue.Na ukikataa ataendelea na hali hiyo ya kutapika.
Kuna sababu nyingi sana zinazopelekea mama mja mzito kutapika.Sababu kubwa kuliko zote ni mabadiliko ya hormone mwilini, ambayo husababisha hali ya kichefuchefu na kutapika miezi 4 ya mwanzo.Pia mabadiliko haya yanaweza kufanya hali iwe mbaya zaidi kama mama ana mimba ya mapacha(Twins), au wakati mwingine kama ana aina ya mimba iitwayo MOLAR PREGNANCY.
Lakini pia mama anapokuwa a magonjwa kama upper urinary tract infection(pyelonephritis), Malaria na mengine anaweza kupata kichefu chefu na kutapika.
lakini wakati mwingine ni Psychogenic, yaani wengine wanafanya kutapika kama fasheni, na wanaweza wakaweka na vitabia vingine kuongeza ukubwa wa tatizo, kama kusema nikimuona mume wangu natapika, au kumpenda shemeji yake kuliko wewe.Ndiyo watu wa aina hii wanaohitaji psychotherapy, yaani wanapelekwa kwa health provider, na wakikaa na wakazungumza anarudi nyumbani tatizo linakuwa limeisha.
kuna watafiti pia wameripoti kwamba, akina mama wenye ujauzito ambao ni wa mtoto wa kike wanatapika zaidi kuliko wale wenye ujauzito wa mtoto wa kiume.bahati mbaya tafiti hizi zimekuwa zikipingana mara kwa mara.