Jamhuri Kihwelu atua Coastal Union

Jamhuri Kihwelu atua Coastal Union

Hussein Massanza

JF-Expert Member
Joined
Dec 26, 2012
Posts
1,016
Reaction score
2,195
kiwhelo.jpg


Kocha wa timu ya Mwadui FC Jamhuri kiwhelu ‘Julio' ametua timu ya Coastal Union hadi mwisho wa msimu huu.

Kocha huyo mwenye maneno mengi, ameiwezesha timu ya Mwadui kupanda daraja kushiriki ligi kuu ya Vodacom msimu ujao.

Coastal Union imekuwa na matokeo mabaya msimu huu kwenye ligi kuu ya Vodacom hivyo imelazimika kumchukua kocha huyo ‘kwa mkopo' ili aweze kuinusuru timun hiyo kongwe isiteremke daraja.

Tayari African Sport timu nyingine ya Tanga imepanda daraja baada ya zaidi ya miaka 20, iwapo Coastal Union itabaki ligi kuu, timu hizo zenye upinzani wa jadi zikarudisha hamasa ya soka mkoani Tanga.

Chanzo: Habari247
 
Siku zote shina la mti linapokauka basi hata matawi yake nayo yatakauka tu! Simba inashuka daraja na matawi yake yote yatashuka daraja.
 
Siku zote shina la mti linapokauka basi hata matawi yake nayo yatakauka tu! Simba inashuka daraja na matawi yake yote yatashuka daraja.

kweli tumeona leo simba kapigwa 5 sifuri na prisons
 
Back
Top Bottom