Jamii ya viongozi wafanyabiashara

Jamii ya viongozi wafanyabiashara

Shayu

Platinum Member
Joined
May 24, 2011
Posts
608
Reaction score
1,655
Viongozi wetu ni muhimu sana kujiepusha na kufanya biashara kama wanataka kuongoza taifa hili vyema, huwezi kuviweka vitu hivi pamoja na vikafanya kazi katika ufanisi wa hali ya juu. (Uongozi + biashara).

Hutaepuka kuwa fisadi, hutaweza kusimamia haki kwa watu. Asili ya biashara ni (uroho) wa kupata faida, na ukiwa madarakani na wakati huo huo unafanya biashara kuna hatari ya kufisadi taifa.

Viongozi wetu ni muhimu sana wasiwe wafanyabiashara na wategemee mishahara tu wanayopewa na taifa na mafao baada ya kustaafu kwao, wakitoka kwenye uongozi wawe huru kufanya wanachotaka, kuna hatari kubwa sana kama viongozi wetu watakuwa wafanyabiashara nchi yetu itaharibika na kupoteza mwelekeo wake. kwasababu asili ya biashara ni uroho wa faida na serikali itaweza kuwasimamia ikiwa tu, wakiwa nje ya siasa na uongozi, na ikiwa viongozi wetu wakiwa sio wafanyabiashara.

Viongozi wetu wakiwa wafanyabiashara hakuna haki itakayosimamiwa. Wafanyabiashara lazima wakae nje ya siasa, wakiwa ndani ya siasa wananchi wa taifa hili hawatoweza kuwa huru. Wataendelea kuwa watumwa tu na watu wa kutumika kwa maslahi ya wachache.

Uhuru wa watu wetu utakuwepo ikiwa wafanyabiashara wakiwa nje ya siasa. Jiulize kwanini mfanyabiashara atake kuwa kiongozi?? Mfanyabiashara hawezi kuwa kiongozi na kamwe hatoweza kuangalia watu wa chini na maskini. Tabia yake ni kujikusanyia kadiri anavyoweza na mtu huyu (Mfanyabiashara) anatakiwa kusimamiwa na serikali ya watu wasio wafanyabiashara ili kudhibiti uroho wake.

Jamii ambayo viongozi wake ni wafanyabiashara ni jamii ambayo ni corrupt ambayo haiangalii utu bali faida ya mali. Kwahiyo ni muhimu kwa wafanyabiashara kuwekwa nje ya siasa na watu wakawaida waongoze Taifa. Madaraka wapewe watu wa kawaida.
watu wa kawaida wenye maadili ya kutosha ya kuongoza watu. watu waliotosheka na wasio walafi.

Kuna watu wanafikiri watu matajiri na wenye pesa hawatoiba ukiwapa uongozi, na maskini kwakuwa hawana kitu wataiba, hii sio kweli. Chanzo cha kuiba ni uroho na kutotosheka. Mtu mroho hatosheki na alichonacho hata awe na kiasi gani, hata umpe dunia nzima hatotosheka. Uroho hauna mipaka. Kuiba au kutokuiba kunategemea maadili ya mtu. Kuna maskini lakini wanaishi maisha ya uaminifu. Kwahiyo tunapochagua kiongozi wetu ni lazima na ni muhimu kufikiria mambo mengi sana.

Tunahitaji mtu mwenye maadili ya kutosha kutuongoza. Maadili yetu kama mtu mmoja mmoja na kama taifa yanategemea sana aina ya kiongozi tutakayemweka madarakani. Mtu mwenye maadili atachagua baraza la mawaziri lenye maadili na watu waliomzunguka kuwa wenye maadili, na mtu mwovu hivyo hivyo. Kumbukeni nuru na giza haviwezi kukaa pamoja. Kwahiyo tukichagua kiongozi mwovu tutegemee taifa la watu waovu. Mpera hauwezi kuzaa maembe. That is impossible.

Kwahiyo integrity ya nchi hii itategemea watu tutakaowaweka madarakani. Nawaambia haya kwasababu tunaelekea katika uchaguzi na nchi yetu imegubikwa na mambo mengi sana ambayo si sahihi. Taswira ya nchi yetu imeharibika kwa mauaji ya albino. Kuna mgawanyiko kwenye taifa letu ambao unahitaji mtu makini mwenye uwezo wa kuleta taifa hili pamoja na kuunda upya maadili ya taifa letu.

Hatuwezi kuunda taifa bila maadili. Kwahiyo ni muhimu taifa letu kurudi katika mstari wa maadili hatuwezi kuendelea pasipo maadili. Turudishe upya utawala wa sheria na order katika taifa letu. Turudishe upya nidhamu. Tunahitaji kuhuisha upya taifa letu na kuleta matumaini mapya na umoja kwa watu wetu wote.

Ubinafsi ambao umemea ndani kabisa ya moyo wa taifa letu ni lazima ukomeshwe tulete kutumikia kwa taifa letu. Kuna matumaini makubwa kama tutabadilika na amani ya kweli itapatikana kama tukizingatia haya mambo. Amani na utulivu wa moyo sio ya kutokuwepo na vita tu.

Ni muhimu sana kutenganisha biashara na uongozi ili tupate mwelekeo kama taifa. Uongozi hauhitaji mtu anayeingia madarakani kupata faida, unahitaji mtu anayeingia madarakani kutumikia. Mfanyabiashara hawezi kutetea maskini anaangalia maslahi yake. kwahiyo wafanyabiashara wakiingia kwenye siasa tegemea maadili ya taifa kuyumba. Ni watu wanaotakiwa kukaa nje ya siasa na kudhibitiwa na serikali.

Matatizo haya yameikumba CCM ambayo ilikuwa inajinadi ni chama cha wakulima na wafanyakazi kilianza vizuri na sasa inaharibu, sababu ya kuchanganya biashara na siasa. Kwasababu ya kuwakumbatia wafanyabiashara na kuwadharau common people.

Pale ambapo watu wengi ambao ni maskini wanapodharauliwa na kuwakumbatia matajiri, kuna hatari kubwa. Lazima kuwe na balance katika nchi kati ya maskini na matajiri pamoja na watu wa kipato cha kati. Kadiri muda unavyokwenda na maisha yanavyoendelea kuwa magumu na uwiano kati ya maskini na matajiri unavyoongezeka ndivyo CCM itakavyoendelea kupata tabu.

Serikali yeyote inaposahau kuangalia watu na kujikita katika kujilimbikizia mali inakosa ushawishi kwa wananchi na ni hatua moja kubwa ya kuifanya serikali hiyo kuwa ya ukandamizaji.

Kwahiyo ni dhahiri kwamba serikali ya CCM ikiendelea na tabia hii huenda tukawa na chama cha kikandamizaji na cha kidikteta. Kiongozi hapaswi kujilimbikizia mali atasahau haki za raia na kuwakandamiza. Ndio haya tunayo yaona katika CCM. Hawaonyeshi mfano wa maadili kwa watu wa taifa hili. Tulitegemea wao wawe mfano. Wananchi wa taifa hili hawapaswi ku support chama ambacho kimekosa maadili. Chama ambacho hakilei vijana katika maadili bora ambayo yatasababisha taifa hili kuendelea. Iangalie CCM ilivyo sasa hivi !

''Siku hizi kuna wao na sisi'' Tabaka la viongozi na walalahoi! Hawajali elimu kwa watu maskini, watoto wao hawasomi katika shule wanazosimamia! Back to your senses CCM! Ulaghai mnaofanya kwa kuzunguka nchi nzima kulinda maslahi yenu na sio ya taifa hausaidii. Wananchi wanajua kinana anachofanya ni usanii wanajua kinana sio miongoni mwao na hata hajui wanavyotaabika, yeye ni watabaka jingine. Tabaka la watu walio juu ya sheria. Tubuni mtapona usanii hausaidii.
 
Kama mfanyabiashara awezi jali wananchi kwa sababu anaangalia maslahi binafsi? Je serikari ikifanya biashara ina mwangalia mteja kwa jicho gani chukulia mifano hai ya sasa iliyopo Tanzania?

Na moja ya jukumu la serikari kutengeneza mazingira ya kukuza biashara kupitia sera ikiwa wao wenyewe watunga sera hakuna hata mmoja ana experience ya biashara wanaelewa vipi changamoto za wafanyabiashara si itabidi wakae nao chini na kujadili; ukisha kaa na mtu mka jadili jinsi ya kutunga sera uoni akiwa ndani anaweza shawishi vizuri zaidi kwa faida ya kukuza biashara ama?
 
Kama mfanyabiashara awezi jali wananchi kwa sababu anaangalia maslahi binafsi? Je serikari ikifanya biashara ina mwangalia mteja kwa jicho gani chukulia mifano hai ya sasa iliyopo Tanzania?

Na moja ya jukumu la serikari kutengeneza mazingira ya kukuza biashara kupitia sera ikiwa wao wenyewe watunga sera hakuna hata mmoja ana experience ya biashara wanaelewa vipi changamoto za wafanyabiashara si itabidi wakae nao chini na kujadili; ukisha kaa na mtu mka jadili jinsi ya kutunga sera uoni akiwa ndani anaweza shawishi vizuri zaidi kwa faida ya kukuza biashara ama?

Jukumu la serikali na viongozi ni kutumikia wananchi na kuweka maono na mikakati ya taifa. Kama viongozi wakiruhusiwa kufanya biashara wakiwa madarakani hawatoweza kutenda hayo. Lazima kutatokea mgangano wa maslahi na kiongozi anatakiwa kuweka kipaumbele maslahi ya taifa kabla ya maslahi binafsi. Ngoja nikupe mfano; Kama mmoja wa viongozi wetu wakiwa wanafanya biashara ya shule hawatopenda kuona shule za jamii zikiimarika watapenda kuona zikiwa mbovu kusudi wao wapate faida katika shule zao. Maamuzi yao yote yatakuwa influenced na faida za kibiashara kwao wao na marafiki zao.
 
Nakubaliana na wewe kuhusu viongozi na biashara.. Kwa kweli ukiangalia kwa makini ni hawa hawa viongozi wanaozorotesha maendeleo ya jamii iliyowazunguka kwa migongo ya biashara. Wanasiasa ni miongoni mwa watu wanalipwa vizuri na serikali yetu na ambao hawapati taabu yoyote ya kucheleweshewa mishahara ua mafao yao, ni watu wanapewa huduma za afya bure tena hata nje ya nchi. Kwa maana hiyo hakuna umuhimu wowote wa mwanasiasa kuwa wafanya biashara.

Kama taifa tufike mahali tufanye maamuzi magumu, au ufanye siasa au huwe mfanya biashara. Chukulia mfano swala la umeme hawa hawa wanasiasa ndo wanaofanya biashara ya Tenesco za mafuta ya kuendeshea mitambo, ndo wenye tenda za kuleta nguzo za umeme na nk. Sasa mtu kama huyu unategemea anaweza kutoa mchango wake, au kutunga sheria za kuibana Tanesco katika swala zima la umeme?

Mfano mwingine wanasiasa ndo hao hao unakuta wanamiliki shule za "private" sasa hebu niambe huyu mwanasiasa kama anashule katika jimbo lake na pia kuna shule ya serikali katika jimbo hilo yenye matatizo lukuki hivi kweli huyu mtu atatoa mchango wake wa kuboresha shule ya serikali na aache shule yake? Tena unakuta hata pesa ambazo zilitakiwa kwenda kwenye shule za serikali zinapelekwa kwenye shule zake.

Tukienda katika sekta za kilimo nako ni hivyo hivyo unakuta mwanasiasa anakwenda nje ya nchi kwa ajira ya semina za kilimo cha kisasa kwa gharama za serikali au wafadhili lakini kipindi anaporudi na ile elimu pengine na vitendea kazi ambavyo amepewa na hawa wafadhili, kinachofanyika sio kuwapata elimu wale wakulima katika eneo lake bali ni kukunua maekari za mashamba na kuanza kulima yenye mwenye na vile vitendea vya alivyopewa na wafadhili kwa ajili ya wakulma anavitumie yeye mwenyewe...

Tena wengine tumeona kwa kutumia migongo ya siasa wanakwenda kukopa na serikali udhamini hii mikopo ili huyu mwanasiasa akafanye biashara.
Mara nyingi mikopo huwa hawarudi na mwisho wa siku serikali ndo inarudisha hiyo mikopo.
Nakibaya zaidi hawa watu huwa hawalipi kodi, wafanyakazi wao kulipwa pesa kidogo maana kwa mfumo tulionao hapa Tanzania mwanasiasa ana kinga ya pekee ukienda kumstaki wewe ndo utawekwe ndani.

Mfano ni mingi sana ukiangalia kwa makini wanasiasa ni miongozi mwa watu wanaofilisi serikali yetu kwa kutumia kofiia zao za ubunge/uwazir na nk.

Tutapinga hatua kama wanasiasa wakifanya kazi za siasa na biashara waachie wafanya biashara.
 
Jukumu la serikali na viongozi ni kutumikia wananchi na kuweka maono na mikakati ya taifa. Kama viongozi wakiruhusiwa kufanya biashara wakiwa madarakani hawatoweza kutenda hayo.
Misingi ya biashara binafsi ni ubunifu unaotokana na kuona faida za kibiashara na kuchukua opportunity, alikadhalika mfanyabiashra mwanasiasa anafanya mambo kwa misingi ya serikari na jinsi ya kufikia malengo yake.

In other words mfanyabiashara ana mbinu zake na serikari ina mbinu zake kwenye kufikia malengo yao, kila mtu ana namna za usimamizi wake wa kufikilia malengo vingenevyo matokeo tarajiwa ayatowezekana. Sasa basi iwapo serikari kuna mwingiliano wa kimaslahi kwa sababu ya kuajiri wafanyabiashara tatizo sio mwajiriwa tatizo ni mfumo wa serikari katika kufikia malengo; mfumo wa serikari unatakiwa pia uwe una usimamizi wa rasimali zake, unafanya vitu na kupima faida, una ajiri watu wenye uwezo wa kufikia malengo ya serikari kwa quality inayotarajiwa, ina uwezo wa ku-utilise human resource efficiently kufikia malengo, una mikakati inayo eleweka kwa kile kinacholengwa.

Hili hayo yatimie tuna anza na ilani ya chama inayomba dhamana ya kuendesha kama mwongozo wa serikari, kufikia malengo kuna hitajika resources kadhaa ambazo chama tawala lazima ieleze itazitoa wapi na kiwango gani tutegemee cha huduma kutoka kwao na walengwa wanafaidika vipi, kuna bunge linalo simamia serikari kwenye utekelezaji ilani za serikari, kuna vyombo vya dola na mahakama kuhakikisha vitu vinafanyika kwa misingi ya sheria za bunge.

Iwapo mfanyabiashara ana kuwa kikwazo basi ujue tatizo sio mtu bali mfumo mzima na uongozi wa juu, hakuna shabaha ya kupimwa kutoka kwenye ilani, hakuna usimamizi wa rasimali zake watu na zile zenye kuleta mabadiliko ya kiuchumi, vyombo vya dola ni hovyo kama kuna conflict of interest na serikari imakuwa deprived of value kwenye service zake kisa waajiriwa wake kuwa na maslahi binafsi basi tatizo sio mtu bali ni mechanism ya usimamizi serikarini na kutokuwa na matarajio nya quality kwneye miradi yake.

In short mtu wa aina yeyote awezi kuwa tatizo kuajiriwa serikarini, tatizo litakuwa mfumo wa serikari na agenda yaserikari kwenye kufikia malengo.

Lazima kutatokea mgangano wa maslahi na kiongozi anatakiwa kuweka kipaumbele maslahi ya taifa kabla ya maslahi binafsi.
Maslahi ya taifa hayatolewi na mimi na wewe (iwapo tungekuwa wafanya biashara na waajiriwa serikarini) bali vyama vinavyoomba ridhaa ya kutuongoza kwa hivyo wapiga kura ndio wenye power kuelekea uchaguzi je tunazijua mbinu zao, au tunaridhika na vipa umbele vyao, wameturidhisha wanaweza pata hizo resources za kutimiza vipaumbele wanavyodai, je wametuelezea kiwango cha huduma na tuna expectation gani kuhusu hizo services. Lakini mtu mmoja awezi kuwa kikwazo kisa ana biashara.

Ngoja nikupe mfano; Kama mmoja wa viongozi wetu wakiwa wanafanya biashara ya shule hawatopenda kuona shule za jamii zikiimarika watapenda kuona zikiwa mbovu kusudi wao wapate faida katika shule zao. Maamuzi yao yote yatakuwa influenced na faida za kibiashara kwao wao na marafiki zao.
Shule za private zina ada kubwa kuliko shule za serikari kwa hivyo kibiashara walengwa ni wengine, shule za serikari ni kutoa elimu kwa kuwafikia wengi either bure au kwa ada yenye uwezo wa wote kumudu according to government reasoning. Kila mtu ana malengo ya ku-quality na burden cost to those services in running those institution wananchi awatakiwi kujali private ina fanya nini tunatakiwa serikari inaposema inatoa elimu ina kiwango gani na inafaida gani chini ya hapo tudai au tunabadili serikari na kuwapa wengine ambao wana ahidi kuboresha na kutupa expectations za kiwango; ni hivi usipojua unaomba nini utapewa chochote.
 
Shayu:

You are misguided for this simple reason. You can’t be a very successful businessman if you aren’t a leader in a society. Take for example Bekhresa and Mengi. Outside their organizations, you see them as opportunist individuals who want to take every chance to enrich themselves. However, inside their organizations, they are responsible for negotiating loans, prepare budgets, paying salaries, accepting losses, setting business visions and above all managing people from various backgrounds. In leadership skills, you can’t get better than this.

Now with regard to the problems you have enumerated in your post, the root cause is the lack of ethics and we can’t attribute that only to the involvement of businessmen in politics and here’s the reason. We know the backgrounds of many Tanzanian politicians. Majority of them, if not all, have no background in business and they weren’t groomed to run successful business entities: private or public. Therefore, it’s a huge mistake to identify them as businessmen. In simple terms, they are just corrupt politicians who use business to cover their unethical activities.

Now, if the goal of your post is to bring the ethical issue to our attention, then the discussion should focus of the application of ethics at every level of society not just a segment of it. You can’t blame businessmen when almost every person in the society aspires a work position that would enable him to steal public money and use it as capital to open a business venture.

Ethics should be applied across-the board proportionally and accordingly. For example, if you are a teacher, businessman, lawyer, medical doctor, you should know what you are supposed to do and what the society expects from you. Equally important, the society should have a mechanism to impose and enforce its expectations. You can’t just have rules that nobody wants to follow.
 
Nakubaliana na wewe kuhusu viongozi na biashara.. Kwa kweli ukiangalia kwa makini ni hawa hawa viongozi wanaozorotesha maendeleo ya jamii iliyowazunguka kwa migongo ya biashara. Wanasiasa ni miongoni mwa watu wanalipwa vizuri na serikali yetu na ambao hawapati taabu yoyote ya kucheleweshewa mishahara ua mafao yao, ni watu wanapewa huduma za afya bure tena hata nje ya nchi. Kwa maana hiyo hakuna umuhimu wowote wa mwanasiasa kuwa wafanya biashara.



Kama taifa tufike mahali tufanye maamuzi magumu, au ufanye siasa au huwe mfanya biashara. Chukulia mfano swala la umeme hawa hawa wanasiasa ndo wanaofanya biashara ya Tenesco za mafuta ya kuendeshea mitambo, ndo wenye tenda za kuleta nguzo za umeme na nk. Sasa mtu kama huyu unategemea anaweza kutoa mchango wake, au kutunga sheria za kuibana Tanesco katika swala zima la umeme?

Mfano mwingine wanasiasa ndo hao hao unakuta wanamiliki shule za "private" sasa hebu niambe huyu mwanasiasa kama anashule katika jimbo lake na pia kuna shule ya serikali katika jimbo hilo yenye matatizo lukuki hivi kweli huyu mtu atatoa mchango wake wa kuboresha shule ya serikali na aache shule yake? Tena unakuta hata pesa ambazo zilitakiwa kwenda kwenye shule za serikali zinapelekwa kwenye shule zake.

Tukienda katika sekta za kilimo nako ni hivyo hivyo unakuta mwanasiasa anakwenda nje ya nchi kwa ajira ya semina za kilimo cha kisasa kwa gharama za serikali au wafadhili lakini kipindi anaporudi na ile elimu pengine na vitendea kazi ambavyo amepewa na hawa wafadhili, kinachofanyika sio kuwapata elimu wale wakulima katika eneo lake bali ni kukunua maekari za mashamba na kuanza kulima yenye mwenye na vile vitendea vya alivyopewa na wafadhili kwa ajili ya wakulma anavitumie yeye mwenyewe...

Tena wengine tumeona kwa kutumia migongo ya siasa wanakwenda kukopa na serikali udhamini hii mikopo ili huyu mwanasiasa akafanye biashara.
Mara nyingi mikopo huwa hawarudi na mwisho wa siku serikali ndo inarudisha hiyo mikopo.
Nakibaya zaidi hawa watu huwa hawalipi kodi, wafanyakazi wao kulipwa pesa kidogo maana kwa mfumo tulionao hapa Tanzania mwanasiasa ana kinga ya pekee ukienda kumstaki wewe ndo utawekwe ndani.

Mfano ni mingi sana ukiangalia kwa makini wanasiasa ni miongozi mwa watu wanaofilisi serikali yetu kwa kutumia kofiia zao za ubunge/uwazir na nk.

Tutapinga hatua kama wanasiasa wakifanya kazi za siasa na biashara waachie wafanya biashara.

Hongera Dada. Kwa kuonyesha werevu wako katika hili. Nakupongeza.
 
Back
Top Bottom