Kasomi
JF-Expert Member
- Sep 3, 2014
- 11,030
- 20,391
Nchini Tanzania Kuna makabila Zaidi ya 120 (125 hivi)
Lakini kuna Makabila yenye watu zaidi ya milioni moja makabila hayo ni Wasukuma, Wanyamwezi, Wachaga, Waha, Wagogo, Wahaya, Wajaluo na Wamakonde.
Jambo la pekee kuhusu jamii zilizoishi na zinazoendelea kuishi Tanzania ni kwamba wakazi asili wanawakilisha makundi yote makuu manne ya lugha barani Afrika.
1. Idadi kubwa sana ya Watanzania ni wa jamii ya Wabantu (k.m. Wasukuma, Wazaramo, Wapare na Wapogoro).
2. Nje ya hao, kuna Waniloti, kwa mfano Wamasai na Wajaluo ambao wengi wao zaidi wanaishi Kenya.
3. Kundi lingine ni makabila ya Wakushi wanaoishi kaskazini mwa Tanzania; hao ni makabila ya Wairaqw, Wafiome, Wasi na Waburunge.
4. Kuna kundi la Wakhoisan wanaofanana na makabila ya Botswana na Namibia; wanaitwa Wasandawe .
Hatimaye kuna Wahadzabe wachache ambao utafiti wa DNA umeonyesha hivi karibuni wana uhusiano wa asili na Watwa wa nchi za Afrika ya Kati.
Pia kuna asilimia ndogo ya watu wenye asili ya nje ya bara la Afrika, kwa mfano Wahindi, Waarabu, Waindochina, Wafarsi, Wachina, Wagiriki na Waingereza. Hii ilisababishwa na karne za mchanganyiko wa mahitaji ya biashara yaliyofanywa na mabara ya Ulaya na Asia hapo Afrika.
Lakini kuna Makabila yenye watu zaidi ya milioni moja makabila hayo ni Wasukuma, Wanyamwezi, Wachaga, Waha, Wagogo, Wahaya, Wajaluo na Wamakonde.
Jambo la pekee kuhusu jamii zilizoishi na zinazoendelea kuishi Tanzania ni kwamba wakazi asili wanawakilisha makundi yote makuu manne ya lugha barani Afrika.
1. Idadi kubwa sana ya Watanzania ni wa jamii ya Wabantu (k.m. Wasukuma, Wazaramo, Wapare na Wapogoro).
2. Nje ya hao, kuna Waniloti, kwa mfano Wamasai na Wajaluo ambao wengi wao zaidi wanaishi Kenya.
3. Kundi lingine ni makabila ya Wakushi wanaoishi kaskazini mwa Tanzania; hao ni makabila ya Wairaqw, Wafiome, Wasi na Waburunge.
4. Kuna kundi la Wakhoisan wanaofanana na makabila ya Botswana na Namibia; wanaitwa Wasandawe .
Hatimaye kuna Wahadzabe wachache ambao utafiti wa DNA umeonyesha hivi karibuni wana uhusiano wa asili na Watwa wa nchi za Afrika ya Kati.
Pia kuna asilimia ndogo ya watu wenye asili ya nje ya bara la Afrika, kwa mfano Wahindi, Waarabu, Waindochina, Wafarsi, Wachina, Wagiriki na Waingereza. Hii ilisababishwa na karne za mchanganyiko wa mahitaji ya biashara yaliyofanywa na mabara ya Ulaya na Asia hapo Afrika.