JamiiForums, Mkombozi wangu wa Fikra!

JamiiForums, Mkombozi wangu wa Fikra!

Hamza Nsiha

JF-Expert Member
Joined
Jul 25, 2022
Posts
221
Reaction score
197
Leo nimeamua kutoa ya moyoni kuhusu, Manufaa niliyoyapata JamiiForums.

Kiukweli, nilibahatika kujiunga na JamiiForums mwezi wa saba~ mwaka huu mara baada ya kutumiwa tangazo linalohuso shindano la "STORIES OF CHANGE 2022" kutoka kwa rafiki yangu ambaye anadai aliliona kutoka kwenye mtandao wa Instagram.

Kabla ya hapo, nilikuwa nikisikia kuhusu "JamiiForums" lakini sikubahatika kuifuatilia kiundani hususani nilisikia baadhi ya marafiki zangu wakichangia mada mbalimbali za kisiasa huku wakianisha vyanzo mbalimbali vya habari ikiwemo JamiiForums.

Lakini, cha ajabu tangu nilipojiunga kama mwanachama wa JamiiForums, dhahiri nimegundua kuwa nilifanya makosa makubwa sana kutojiunga toka zamani_ kwa maana hivi sasa JamiiForums ndio mtandao wangu pendwa. Kila siku lazima niperuzi kuangalia mada mbalimbali zilizowekwa kikaangoni, pamoja na kusoma stori mbalimbali ni ukweli dhahiri kuwa JamiiForums imenikomboa katika mambo mbalimbali ambayo yamenifanya kuwa mchangia mada mkubwa katika stori na midahalo mbalimbali nje na JamiiForums.

Pia kitu kikubwa, ni kuwa nimeweza kuwashawishi baadhi ya rafiki zangu ambao walikuwa na fikra kama zangu za awali kuhusu JamiiForums. Lakini mpaka sasa wamefanikiwa kujiunga huku wakifurahishwa na Shindano la "STORIES OF CHANGE"

Pia ningependa kufahamu mwana JamiiForums mwenzangu, ilikuwaje mpaka ukaingia katika mtandao huu mzuri na wenye tija au na wewe uliingia kupitia rafiki yako?

Mwisho wa yote, japo si kwa ubaya _Ningependa kuwashukuru wana Jukwaa wenzangu ambao tumekuwa tukishea mawazo mbalimbali katika mada tofauti nilizowahi kuzipakia.

Pia mimi ni mshiriki wa "STORY OF CHANGES" nikiwa na mada inayohusu "VITA YA VIJANA DHIDI YA MAENDELEO YA SAYANSI NA TEKNOLOJIA"

hivyo si vibaya kama utapata muda wa kupitia ili kujifunza baadhi ya mawazo niliyoweza kuainisha pia ukipendezwa zaidi unaweza kunipatia kura yako.
 
Kwanza sio Jamii Forum, ni JamiiForums. Ngoja sasa nirudi kusoma ulichoandika..
 
Pia mimi ni mshiriki wa "STORY OF CHANGES" nikiwa na mada inayohusu "VITA YA VIJANA DHIDI YA MAENDELEO YA SAYANSI NA TEKNOLOJIA"

hivyo si vibaya kama utapata muda wa kupitia ili kujifunza baadhi ya mawazo niliyoweza kuainisha pia ukipendezwa zaidi unaweza kunipatia kura yako.
Nyingine zote porojo tu. Ulichotaka kusema hasa ndo hichi. Nimeshakupigia kura japo sijamaliza kusoma andiko lako. Nitarudi baadaye
 
Yeah! Safi sana.. Mimi nilijiunga mwenyewe tu baada ya kupita mitandaoni na kuona, nikawa member, kwa sasa JF imeisha makali, siku za nyumba ilikuwa na wachangiaji mahiri sana wenye uelewa wa mambo kwa upana kabisa.

Siku hizi wengi wameiabandon kutoka na sababu kadha wa kadha, lakini bado unaweza kuambulia manufaa lukuki kwa baadhi ya members ambao wana madini pia, Na pia kule JF store umaweza ukajipatia vitabu mbalimbali bure, kwa ajili ya kukuza ufahamu wako, kwa hiyo bado JF ina manufaa makubwa kabisa hasa kwa mwanachama.

Makala yako kwenye story of change sijaisoma, kama nitajaaliwa wepesi nitaenda niione.

Hongera na karibu sana JamiiForums, where it used to be the Home of Great Thinkers and we Dared to talk openly!
 
Yeah! Safi sana.. Mimi nilijiunga mwenyewe tu baada ya kupita mitandaoni na kuona, nikawa member, kwa sasa JF imeisha makali, siku za nyumba ilikuwa na wachangiaji mahiri sana wenye uelewa wa mambo kwa upana kabisa.

Siku hizi wengi wameiabandon kutoka na sababu kadha wa kadha, lakini bado unaweza kuambulia manufaa lukuki kwa baadhi ya members ambao wana madini pia, Na pia kule JF store umaweza ukajipatia vitabu mbalimbali bure, kwa ajili ya kukuza ufahamu wako, kwa hiyo bado JF ina manufaa makubwa kabisa hasa kwa mwanachama.

Makala yako kwenye story of change sijaisoma, kama nitajaaliwa wepesi nitaenda niione.

Hongera na karibu sana JamiiForums, where it used to be the Home of Great Thinkers and we Dared to talk openly!
Safi snna mkuu unazidi kunipa madini kuhusu JamiiForums ngoja niingie huko Store nikajipakulie madini.
 
Asante sana! Mkuu, mambo mazuri kama haya tunayapata kutoka kwenu wakubwa! Nimerekibisha pia.
Yeah, Jamii Forum ni kitu kingine kabisa, nasikia ni mtandao uko Kenya huko!
Be Blessed for your humbleness!
 
Umesikia leo mm toka 2012 Ni member Bila kujisajili rasm nikatimba 2019 baada ya kuona Sasa nimekomaa vzr

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom