JamiiForums yatoa mafunzo kwa Wadau wa Habari kuhusu umuhimu na njia za Uhakiki wa Taarifa

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760

Julai 26, 2024, JamiiForums ikishirikiana na The Collaboration on International ICT Policy for East and Southern Africa (CIPESA) iliendesha Mafunzo ya Uhakiki wa Taarifa kwa Wadau wa Tasnia ya Habari kama sehemu ya kuwajengea uwezo katika kutekeleza majukumu yao.

Washiriki walifundishwa athari ya taarifa potofu hususan kwenye kipindi cha Uchaguzi, jinsi ya kutambua taarifa hizo na namna wanavyoweza kutumia ujuzi na nyenzo mbalimbali kuzihakiki.

Aidha, Washiriki hao walipata fursa ya kufafanuliwa jinsi JamiiForums inavyopambana na taarifa potofu kupitia Jukwaa lake mahususi la JamiiCheck.com ambalo huwashirikisha Wananchi mchakato wa kuhakiki maudhui yanayopatikana ndani na nje ya Mtandao.










 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…