Januari Makamba aanza kuwafanyia fitina Mawaziri wenzake

Januari Makamba aanza kuwafanyia fitina Mawaziri wenzake

saidoo25

JF-Expert Member
Joined
Jul 4, 2022
Posts
624
Reaction score
1,456
Tumeona siku za karibuni Makamba badala ya kujitika kutatua matatizo makubwa yaliyoko kwenye Wizara yake yanayolalamikiwa wa wananchi kila mahali ikiwemo tatizo la kukatika kwa umeme, kuchelewa kwa miradi ya Rea, lakini ameanza kuwapiga fitna mawaziri wenzake ili waonekane hawafanyi kazi.

Mfano ni tukio la juzi kitendo cha Makamba kumtaka Waziri wa Kilimo Bashe kutolea ufafanuzi suala la Bei ya mbolea wakati suala hilo lilishazungumzwa bungeni na baadae Waziri mwenyewe Bashe akiwa Kilosa alitolea ufafanuzi wote kuhusiana na hatua anazochukua.

Bashe aliweka wazi hatua inazochukua ikiwemo kurudisha mfumo wa unununuzi wa mbolea kwa pamoja, kurejesha utaratibu wa kuweka bei elekezi na kurejesha utaratibu wa usimamizi wa karibu wa Serikali kwenye mbolea ili kuondoa uholela wa wafanyabiashara kuwaumiza wakulima.

Sasa nini kinachomfanya Makamba kuwatengenezea fitina mawaziri wenzake kwa Rais ili waonekane hawafanyi kazi ikiwa yeye wizara yake ndio inaongoza kwa usimamizi mbovu wa Miradi hadi Makamu wa Rais Dk. Philip Mpango aliinyooshea kidole wizara hiyo alipokuwa ziarani Mkoa wa Katavi.
 
Ulichoandika ndio fitina yenyewe,sijui kuna serikali ngapi zinahudumu ikiwa hilo unaona ni fitina..
Umeshawahi kumuona Jumaa Aweso anafanya hivyo? zaidi unamuona anafokea wakandarasi wake walioko kwenye wizara yake na kuvunja jumuiya za watumiaji maji ili wananchi waondokane na adha ya maji
 
Wewe unachuki zako binafsi na huo waziri mbona hapo ni kawaida tu, kuomba ufafanuzi kwa jambo lolote acheni kijana afanye kazi zake.
 
Kama ameulizwa maswali yanayohusiana na Wizara nyingine lazima aelekeze kwa Waziri wa Wizara husika aweze kutolea majibu.
 
Kama ameulizwa maswali yanayohusiana na Wizara nyingine lazima aelekeze kwa Waziri wa Wizara husika aweze kutolea majibu.
Umeshawahi kumuona Jumaa Aweso akifanya hayo inamaana yeye kwenye ziara zake haulizwi mambo nje ya wizara yake?
 
Umeshawahi kumuona Jumaa Aweso anafanya hivyo? zaidi unamuona anafokea wakandarasi wake walioko kwenye wizara yake na kuvunja jumuiya za watumiaji maji ili wananchi waondokane na adha ya maji
Anafanya Sana tuu sema hivi nyie mna attention zaidi na January..

Juzi tuu hapo Naibu Waziri Ujenzi alitoa maagizo kwa Mameneja wote wa Barabara wa TanRoads na Tarura ilhali Tarura wako Tamisemi..

Mwisho inategemea na scenario,mara kadhaa niliwahi muona Waziri wa Ardhi aliyestaafu akipokea Kero za Wananchi kwa masuala yaliyo nje ya Wizara yake na kusema atayawasilisha kwa Waziri wa kisekta..

So acha ujinga,wanatumikia serikali moja na wananchi ndio waliyaibua hayo mbele yake.
 
Anafanya Sana tuu sema hivi nyie mna attention zaidi na January..

Juzi tuu hapo Naibu Waziri Ujenzi alitoa maagizo kwa Mameneja wote wa Barabara wa TanRoads na Tarura ilhali Tarura wako Tamisemi..

Mwisho inategemea na scenario,mara kadhaa niliwahi muona Waziri wa Ardhi aliyestaafu akipokea Kero za Wananchi kwa masuala yaliyo nje ya Wizara yake na kusema atayawasilisha kwa Waziri wa kisekta..

So acha ujinga,wanatumikia serikali moja na wananchi ndio waliyaibua hayo mbele yake.
Makamba aliapa kusimamia Sekta ya Nishati au Kilimo? na Bashe kazi yake ni nini labda unisaidie uelewa
 
Makamba aliapa kusimamia Sekta ya Nishati au Kilimo? na Bashe kazi yake ni nini labda unisaidie uelewa
Umeanza utoto sasa unless huelewi maana ya kuwa kiongozi.

Nimekutokeae na mifano bado unauliza mambo ya kijinga..

Nyie ndio huwa mkiwa viongozi sehemu huwa mnaleta ligi za kindezi na kusema hayo hayahusu..

Nimewahi kuona sehemu eti DED anavutana na Meneja wa Tarura Kuhusu barabara as if wako Nchi mbili tofauti,na hapa yule Meneja wa Mkoa wa Tarura ndio alikuwa fala hadi akapigwa chini.
 
Tuache kumsingizia kila kitu mheshimiwa makamba, unasema amechelewesha miradi fulani utazani makamba amebeba hela kaziweka kwenye akaunti yake kwa manufaa yake binafsi, fedha za imma Zina utaratibu wake na hawezi akawa amepitishiwa bajeti na hela zipo halafu acheleweshe mradi na Rais akae kimya, Tusipende kumchukua mtu kwa kufundishwa au kufuata mkumbo tu kwa kuwa mtu fulani kwa sababu zake kaamua kumchukua,
 
Wewe utakuwa Bashe na kama siyo ni Wakala wake. Lakini pamoja na yote hayo hii beef ya BASHE vs MAKAMBA nimeipenda na natamani wazidishe tofauti zao ili mwisho wa siku tutajua KILAZA nani na nini wanachokitaka 2025 maana kila mmoja anaanza kuondoa jam mapema.
 
Mtoto mpendwa anadeka, wakati hamuingii Bashe hata robo ya uwezo alionao, ashukuru ni mtoto wa mlamba asali
 
Tumeona siku za karibuni Makamba badala ya kujitika kutatua matatizo makubwa yaliyoko kwenye Wizara yake yanayolalamikiwa wa wananchi kila mahali ikiwemo tatizo la kukatika kwa umeme, kuchelewa kwa miradi ya Rea, lakini ameanza kuwapiga fitna mawaziri wenzake ili waonekane hawafanyi kazi.

Mfano ni tukio la juzi kitendo cha Makamba kumtaka Waziri wa Kilimo Bashe kutolea ufafanuzi suala la Bei ya mbolea wakati suala hilo lilishazungumzwa bungeni na baadae Waziri mwenyewe Bashe akiwa Kilosa alitolea ufafanuzi wote kuhusiana na hatua anazochukua.

Bashe aliweka wazi hatua inazochukua ikiwemo kurudisha mfumo wa unununuzi wa mbolea kwa pamoja, kurejesha utaratibu wa kuweka bei elekezi na kurejesha utaratibu wa usimamizi wa karibu wa Serikali kwenye mbolea ili kuondoa uholela wa wafanyabiashara kuwaumiza wakulima.

Sasa nini kinachomfanya Makamba kuwatengenezea fitina mawaziri wenzake kwa Rais ili waonekane hawafanyi kazi ikiwa yeye wizara yake ndio inaongoza kwa usimamizi mbovu wa Miradi hadi Makamu wa Rais Dk. Philip Mpango aliinyooshea kidole wizara hiyo alipokuwa ziarani Mkoa wa Katavi.
UTABIRI UMETIMIA LEO WAZIRI WA MAJI AWESO ANAONEKANA HAFAI KWA SABABU YA MAKAMBA KUKATA UMEME MIRADI YA MAJI
 
Baraza la Mawazi ni team moja na hufanyakazi kwa kushirikiana, hili linaweza kuwa wamekubaliana aulize swali hilo ili aweze kubapa nafasi ya kuelezea Umma kinachoendelea.
 
Back
Top Bottom