January ataja mambo manne yaliyompa ushindi Dk Ndugulile

January ataja mambo manne yaliyompa ushindi Dk Ndugulile

jjackline

Senior Member
Joined
Jul 25, 2024
Posts
111
Reaction score
274
Aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, January Makamba amempongeza Dk Faustine Ndugulile kwa kuchaguliwa kuwa Mkurugenzi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) Ukanda wa Afrika.

Dk Ndugulile ambaye ni Mbunge wa Kigamboni (CCM), jijini Dar es Salaam amechaguliwa jana Jumanne, Agosti 27, 2024 katika Mkutano wa Afya wa 74 wa Shirika la Afya Duniani (WHO) unaoendelea Brazzaville, Congo.

Wagombea wengine walikuwa ni Dk Boureima Hama Sambo (Niger) Dk N'da Konan Michel Yao (Cote d'Ivoire) Dk Ibrahima Soc'e Fall (Senegal) na Dk Richard Mihigo (Rwanda).

Soma Pia: Dkt Faustine Ndugulile ashinda kinyang'anyiro cha ukurugenzi Mkuu wa WHO kanda ya Afrika

Dk Ndugulile amepata ushindi huo baada ya nchi 19 kuipigia kura Tanzania katika mzunguko wa kwanza, 12 Senegal, huku Niger na Rwanda zikipigiwa kura saba kila moja.

Baada ya kutangazwa mshindi, pongezi zimeendelea kumiminika na Watanzania mbalimbali akiwemo January ambaye kabla ya uteuzi wake kutenguliwa Julai 21, 2024 na nafasi yake kuteuliwa Balozi Mahmoud Thabit Kombo, alishiriki kwenye kampeni.

Snapinsta.app_457034397_501377472638714_7542389748912878880_n_1080.jpg
 
Ila hapa jamaa kapiga parefu na inaonekana yuko smart maana kutoboa kwa hao ma francophone huwa sio rahisi
Alichokiomba inaonekana alikifanyia tafiti haswa
Unafikiri hatuna watu wazuri intellectually ndugu, tatizo wengi wao hujitoa ufahamu sababu ya matumbo yao na kusahau uwezo wao kiakili.

Pia mabogus mithili ya Nape ndio kwa muda mrefu yamekuwa yakitumika kama wawakilishi wa wasomi wetu wa Tz. Watu wasioweza kujenga hoja yeyote yenye mantiki.

Mbaya zaidi uongozi wa Tz ni mzuri sana katika kuharibu akili za wasomi wao. Mtu anaweza kuja na maono mazuri ya kimaendeleo lakini akaishia kutumika kisiasa.

All in all Dr. Ndugulile kadhihirishia ulimwengu kuwa Tz we are more than tabloids and social media maniacs.
 
Aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, January Makamba amempongeza Dk Faustine Ndugulile kwa kuchaguliwa kuwa Mkurugenzi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) Ukanda wa Afrika.

Dk Ndugulile ambaye ni Mbunge wa Kigamboni (CCM), jijini Dar es Salaam amechaguliwa jana Jumanne, Agosti 27, 2024 katika Mkutano wa Afya wa 74 wa Shirika la Afya Duniani (WHO) unaoendelea Brazzaville, Congo.

Wagombea wengine walikuwa ni Dk Boureima Hama Sambo (Niger) Dk N'da Konan Michel Yao (Cote d'Ivoire) Dk Ibrahima Soc'e Fall (Senegal) na Dk Richard Mihigo (Rwanda).

Soma Pia: Dkt Faustine Ndugulile ashinda kinyang'anyiro cha ukurugenzi Mkuu wa WHO kanda ya Afrika

Dk Ndugulile amepata ushindi huo baada ya nchi 19 kuipigia kura Tanzania katika mzunguko wa kwanza, 12 Senegal, huku Niger na Rwanda zikipigiwa kura saba kila moja.

Baada ya kutangazwa mshindi, pongezi zimeendelea kumiminika na Watanzania mbalimbali akiwemo January ambaye kabla ya uteuzi wake kutenguliwa Julai 21, 2024 na nafasi yake kuteuliwa Balozi Mahmoud Thabit Kombo, alishiriki kwenye kampeni.

Kuna yule Rais wenu mwenye roho mbaya alimbaniaga Membe 😂😂😂😂
 
Unafikiri hatuna watu wazuri intellectually ndugu, tatizo wengi wao hujitoa ufahamu sababu ya matumbo yao na kusahau uwezo wao kiakili.

Mbaya zaidi uongozi wa Tz ni mzuri sana katika kuharibu akili za wasomi wao. Mtu anaweza kuja na maono mazuri ya kimaendeleo lakini akaishia kutumika kisiasa.

All in all Dr. Ndugulile kadhihirishia ulimwengu kuwa Tz we are more than tabloid and social media maniacs.
Hiyo para ya mwisho 🙏🙏🙏
Basi ni muhimu hizi akili zitumike na ndani pia kuleta maendeleo hasa ya taasisi
 

January ataja mambo manne yaliyompa ushindi Dk Ndugulile​

Hayo mambo manne ni yapi? Sijayaona.
 
Back
Top Bottom