Aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, January Makamba amempongeza Dk Faustine Ndugulile kwa kuchaguliwa kuwa Mkurugenzi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) Ukanda wa Afrika.
Dk Ndugulile ambaye ni Mbunge wa Kigamboni (CCM), jijini Dar es Salaam amechaguliwa jana Jumanne, Agosti 27, 2024 katika Mkutano wa Afya wa 74 wa Shirika la Afya Duniani (WHO) unaoendelea Brazzaville, Congo.
Wagombea wengine walikuwa ni Dk Boureima Hama Sambo (Niger) Dk N'da Konan Michel Yao (Cote d'Ivoire) Dk Ibrahima Soc'e Fall (Senegal) na Dk Richard Mihigo (Rwanda).
Soma Pia: Dkt Faustine Ndugulile ashinda kinyang'anyiro cha ukurugenzi Mkuu wa WHO kanda ya Afrika
Dk Ndugulile amepata ushindi huo baada ya nchi 19 kuipigia kura Tanzania katika mzunguko wa kwanza, 12 Senegal, huku Niger na Rwanda zikipigiwa kura saba kila moja.
Baada ya kutangazwa mshindi, pongezi zimeendelea kumiminika na Watanzania mbalimbali akiwemo January ambaye kabla ya uteuzi wake kutenguliwa Julai 21, 2024 na nafasi yake kuteuliwa Balozi Mahmoud Thabit Kombo, alishiriki kwenye kampeni.
Dk Ndugulile ambaye ni Mbunge wa Kigamboni (CCM), jijini Dar es Salaam amechaguliwa jana Jumanne, Agosti 27, 2024 katika Mkutano wa Afya wa 74 wa Shirika la Afya Duniani (WHO) unaoendelea Brazzaville, Congo.
Wagombea wengine walikuwa ni Dk Boureima Hama Sambo (Niger) Dk N'da Konan Michel Yao (Cote d'Ivoire) Dk Ibrahima Soc'e Fall (Senegal) na Dk Richard Mihigo (Rwanda).
Soma Pia: Dkt Faustine Ndugulile ashinda kinyang'anyiro cha ukurugenzi Mkuu wa WHO kanda ya Afrika
Dk Ndugulile amepata ushindi huo baada ya nchi 19 kuipigia kura Tanzania katika mzunguko wa kwanza, 12 Senegal, huku Niger na Rwanda zikipigiwa kura saba kila moja.
Baada ya kutangazwa mshindi, pongezi zimeendelea kumiminika na Watanzania mbalimbali akiwemo January ambaye kabla ya uteuzi wake kutenguliwa Julai 21, 2024 na nafasi yake kuteuliwa Balozi Mahmoud Thabit Kombo, alishiriki kwenye kampeni.