Hatimaye alikuwa kimya sana tangu ameteguliwa lakini sasa January Makamba ameibuka kwenye kampeni za kuwanadi wagombea wa chama chake CCM
=====================
Mbunge wa Jimbo la Bumbuli ambaye pia ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa, January Makamba amesema chama hicho kinajivunia ubora wa wagombea wake, sera bora, na rekodi nzuri ya uongozi, vitu ambavyo vinakipa chama hicho nafasi kubwa ya kushinda katika uchaguzi wa serikali za mitaa utakaofanyika Novemba 27, 2024.
Akizungumza wakati wa kuwafanyia kampeni wagombea wa CCM Jimboni Bumbuli mkoani Tanga, Makamba ameeleza kuwa mchakato wa upatikanaji wa wagombea ndani ya chama umejikita katika kuhakikisha wanachaguliwa viongozi bora kupitia mchujo wa kina.
"Sisi CCM tunaamini kwamba kwenye Chama Cha Mapinduzi tunazo turufu kadhaa ambazo zinatubeba kuhakikisha kwamba tunashinda. Moja ni ubora wa wagombea. Sisi tuna namna ambavyo tunawapata wagombea wetu, kwanza wanapigiwa kura, pili wanapitishwa na vikao, na kikao cha mwisho kabisa ni Halmashauri Kuu ya Wilaya, ambayo ina watu wengi. Kwahiyo, mkimkuta mgombea hapa labda anayegombea uenyekiti wa kijiji, amepitishwa na watu wengi zaidi, amepitishwa kwenye mchujo zaidi, kwahiyo mnakuwa na uhakika kuwa yeye ni bora. Kwa hiyo tunajivunia na ubora wa wagombea," amesema Makamba.
Ameongeza kuwa sera za CCM zimeendelea kuwashawishi wananchi kwa kuwa zinahusu moja kwa moja maisha yao ya kila siku, hasa kupitia programu za maendeleo vijijini.
"Tunajivunia na sera nzuri. Tunawaeleza wananchi nini tutafanya, na sisi Chama Cha Mapinduzi tuna programu yetu ya maendeleo ya watu katika vijiji vyetu. Kwahiyo ni rahisi zaidi kuwaeleza na kuwashawishi kwa sababu ni mambo yanayowahusu," amesisitiza na kuongeza,
"Tunayo rekodi nzuri ya kuwa na wagombea tayari ambao wameongoza vizuri,"
Viongozi wa CCM naona km wanatumia nguvu kubwa sana kuwaaminisha watanzania kuwa wao n Bora sana kuliko wengine, na utafikiri watu tunaoambiwa maneno hayo n wageni Kwenye hii nchi 😅 yaan km vile watanzania wt tumefika Leo paaaaa nakuanza kuambiwa uzuri wa viongozi watakao tuongoza ktk nchi mpyaa ,CCM wametuona hatuoni ,wajinga ,mazwazwa...
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (MNEC), January Makamba ametoa kauli kwamba suala litakalokibeba Chama Cha Mapinduzi kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa ni namna kinavyoshughulika na kero zinazowakabili wananchi.
Makamba ambaye pia ni Mbunge wa Bumbuli ameongeza kwamba katika uchaguzi huu kunashindanishwa mambo manne ambayo ni ubora wa wagombea, ubora wa sera, ubora wa vyama, rekodi ya uongozi. Ameeleza kwamba mambo yote hayo manne yanaibeba CCM.
Hata hivyo, amesema kwamba uhakika wa ushindi wa CCM unatokana na namna CCM inavyoshughulikia na itakavyoendelea kuzishughulikia nakuzimaliza changamoto zinazowakabili wananchi.
Hayo ameyasema Novemba 21,2024 wakati akizungumza na wananchi na wanachama wa CCM katika mikutano ya hadhara ya kampeni za uchaguzi wa serikali za mitaa iliyofanyika katika Halmashauri ya wilaya ya Bumbuli mkoani Tanga.
Hatimaye alikuwa kimya sana tangu ameteguliwa lakini sasa January Makamba ameibuka kwenye kampeni za kuwanadi wagombea wa chama chake CCM
=====================
Mbunge wa Jimbo la Bumbuli ambaye pia ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa, January Makamba amesema chama hicho kinajivunia ubora wa wagombea wake, sera bora, na rekodi nzuri ya uongozi, vitu ambavyo vinakipa chama hicho nafasi kubwa ya kushinda katika uchaguzi wa serikali za mitaa utakaofanyika Novemba 27, 2024.
Akizungumza wakati wa kuwafanyia kampeni wagombea wa CCM Jimboni Bumbuli mkoani Tanga, Makamba ameeleza kuwa mchakato wa upatikanaji wa wagombea ndani ya chama umejikita katika kuhakikisha wanachaguliwa viongozi bora kupitia mchujo wa kina.
"Sisi CCM tunaamini kwamba kwenye Chama Cha Mapinduzi tunazo turufu kadhaa ambazo zinatubeba kuhakikisha kwamba tunashinda. Moja ni ubora wa wagombea. Sisi tuna namna ambavyo tunawapata wagombea wetu, kwanza wanapigiwa kura, pili wanapitishwa na vikao, na kikao cha mwisho kabisa ni Halmashauri Kuu ya Wilaya, ambayo ina watu wengi. Kwahiyo, mkimkuta mgombea hapa labda anayegombea uenyekiti wa kijiji, amepitishwa na watu wengi zaidi, amepitishwa kwenye mchujo zaidi, kwahiyo mnakuwa na uhakika kuwa yeye ni bora. Kwa hiyo tunajivunia na ubora wa wagombea," amesema Makamba.
Ameongeza kuwa sera za CCM zimeendelea kuwashawishi wananchi kwa kuwa zinahusu moja kwa moja maisha yao ya kila siku, hasa kupitia programu za maendeleo vijijini.
"Tunajivunia na sera nzuri. Tunawaeleza wananchi nini tutafanya, na sisi Chama Cha Mapinduzi tuna programu yetu ya maendeleo ya watu katika vijiji vyetu. Kwahiyo ni rahisi zaidi kuwaeleza na kuwashawishi kwa sababu ni mambo yanayowahusu," amesisitiza na kuongeza,
"Tunayo rekodi nzuri ya kuwa na wagombea tayari ambao wameongoza vizuri,"