Kuna faida Japan inayopata,ni woga wake au ni ukarimu tu wa watu wake.
Mkuu Japan 🇯🇵 Ilipopigwa kuanzia mwaka 1945-52 ilikaliwa kimabavu na Marekani kisha ilisainishwa mkataba wa amani uliokuwa na vipengele vingi, vichache kati ya hivyo ni;
Kulipa fidia (baadhi ya nchi zilisamehe), kuachia makoloni yake yote, kukubali makosa yote ya kivita iliyoshitakiwa kwayo na mahakama ya kijeshi, kuyapendelea mataifa ya ‘Allied Powers’ katika biashara n.k
Lakini Marekani ilibadili gia, ikaanza kukuza uchumi wa Japan 🇯🇵
lengo kuu ni kuzuia vimelea vya ukomunist kuota mizizi ndani ya Japan 🇯🇵.
Na baadae Marekani ikaunda mfumo kati ya nchi za New Zealand, Australia, Korea Kusini, Japan na Marekani wa kiulinzi na kibiashara wanaouita ‘San Francisco System’.
Leo hii Japan 🇯🇵 ni mshirika wa karibu sana wa Marekani kwa sababu hizo.
FAIDA AU UOGA?
Ni faida Mkuu, Japan 🇯🇵 inanufaika sana kiuchumi (ninaeleza hapa chini) na kiulinzi.
Lakini pia inapata hasara fulani fulani.
Sababu za kufufuka kwa Uchumi wa Japan 🇯🇵
Binafsi nitaziweka katika makundi mawili
1) Za ndani
2) Za nje
1) Za ndani - Kundi la kwanza nitaachana nalo ila kwa kifupi ni kuhusu sera za ndani kama vile kuhamasisha wanawake kufanya kazi.
2) Za nje - Hapa hoja kubwa na Vita vya Korea (1950-53).
Vita hivyo vilipoanza Marekani ilitumia ushawishi wake kuiingiza UN vitani kuilinda Korea Kusini, na kutokana na jiografia ya Korea ilivyo ambapo Magharibi ilipakana na China 🇨🇳 (Wakomunist), Kaskazini na Korea Kaskazini 🇰🇵 (Wakomunist) mashariki na Bahari ya Pasifiki na visiwa vya USSR (Wacomunist), Kusini na Bahari tena na Japan 🇯🇵 iliyodorora kiuchumi.
Kwa Marekani adui alikuwa ni Wakomunist hivyo kijeshi ilikua ni ‘logical’ wao kuiwezesha Japan Kiuchumi hasa kufufua viwanda ambavyo vilizalisha silaha na mahitaji ya kutosha kwaajili ya vikosi vya UN na Marekani huko Korea. Na kwa mpango huu Marekani 🇺🇸 Iliweza kufupisha ‘supply line’ hivyo kuiwezesha kupambana vizuri kwenye rasi ya Korea.
Mpango wa kufufua viwanda vya Japan 🇯🇵 uliisaidia sana Japan 🇯🇵 maana viwanda vyake vilizalisha bidhaa nyingi zikiwemo silaha na kupata soko la uhakika.
Kuanzia kipindi hiko wachumi wanaeleza 🇯🇵 Ilikuwa kwenye kipindi cha “Economic Boom” mpaka miaka ya 1970.
Nafikiri nimejibu swali lako.