Japo hakuna ajuaye sababu za kutwaliwa kaka, isipokuwa yeye, kuna watu saw it coming, wakasema, wakapuuzwa, akatwaliwa. Dada ukisikia usipuuze hili

Hana mvuto hata majukwaani anaongea km muuza Wanzuki, mimacho anarembua km wale wadada wa Ubungo Riverside..
 
Nyie wachawi habari zenu,Mnajifanya watabiri kumbe Wanga tu hamna lolote .Lengo lenu kuwatia watu jakamoyo lakini hamfanikiwi kamwe.Mnajifanya kuongea kwa mafumbo ili muonekana mna jambo la maana lakini ni namna ya kujifurahisha tu.
Kumer-niisha nini ?
 
Advocate, hii nayo ni "Voices from within "?????
 
Nyie wachawi habari zenu,Mnajifanya watabiri kumbe Wanga tu hamna lolote .Lengo lenu kuwatia watu jakamoyo lakini hamfanikiwi kamwe.Mnajifanya kuongea kwa mafumbo ili muonekana mna jambo la maana lakini ni namna ya kujifurahisha tu.

Lililo muhimu tuwe tunaishi au tunatwaliwa, tujitahidi kwa uwezo wetu wote, kutenda haki.

Dhuluma huzaa laana mbalimbali.

Tukitaka tuishi au kutwaliwa kwa amani, tusilazimishe wala kutengeneza mazingira ya kudlulumu haki ili kuyapata madaraka.

Tengeneza mazingira na michakato ya haki, watu wakitaka wakuchague, wasipokuchagua, mshukuru Mungu ukapumzike kwa amani. Lakini yale mambo ya mara form moja, mara hakuna mtu mwingine kugombea, yanakujengea laana. Na kuna wakati Muumba wetu huamua kuwaonesha ujinga wao wale wanaodhulumu haki za wengine ili tu wayapate madaraka. Anaruhusu wafanye uovu wao, kisha huwaondoa na kuwanyima nafasi ya kuyafurahia madaraka hayo waliyoyapora kwa nguvu. Kumbuka lile fundisho la Mungu:

" Lakini Mungu akamwambia: ‘Mpumbavu wewe; leo usiku roho yako itachukuliwa. Na vitu vile vyote ulivyojirundikia vitakuwa vya nani?’

Tutafute madaraka na mali kwa namna zilizo halali, siyo kwa kudhulumu wengine. Tujue kuwa juu yetu yupo aliye mkuu kuliko sisi ambaye ni mlinzi wa haki za wote, ambaye anaweza kukufanya uyakose madaraka uliyoyapoka kwa nguvu, lakini akakunyima pia urithi wa mbinguni aliotuandalia.

Gombea uongozi, shawishi kwa kadiri unavyoweza, lakini kamwe usiwadhulumu wengine. Waasisi wa nchi hii waliikabidhi na kuomba ulinzi wa mamlaka ya Mungu wetu, na maombezi ya Malkia wa mbingu mkingiwa dhambi ya asili, ndiyo sababu ya kuomba nchi ipate uhuru usiku wa tarehe 8 Desemba, ambayo ni sikukuu ya Bikira Maria, mkingiwa dhambi ya asili.
 
Uongozi ni sawa na koti lakuazima.. Siku zote mchezaji haoni makosa ila watazamaji ndio huwona makosa na ukiwa na busara utasikiliza maoni ya watazamani na ndio maana mpira ni dakika 90 ila kuna mapumziko ambapo wachezaji upewa mrejesho wa uchezaji wao... na wakati mwingine refa huwamua kumtoa huyu na kumuweka yule sasa ktk siasa hakuna tofauti. Bahati mbaya refa ndio mchezaji na ndio mpanga team na huwa hachoki.... Labda azimie kwa uwanja....

Umenikumbusha mbali sana

Niliwaza sana sikujuwa kile kinataka tokea


Nikiwa shabiki mkubwa wa Mzee hayati Baba nikawaza pia hili...

Nakaona picha hii

 
Ni kweli lakini usisahau hata katiba hii hii mbovu wanaivunja
katiba ya chama chao ndo nayo balaa wanaikanyaga!
Ni mtu mjinga tuu anaweza kulinganisha kati ya katiba ya chama au kikundi chochote cha hiari na katiba ya nchi.
Kwa hiyo siwezi kukujibu maana nimekuelewa uko kundi gani.
 

Hili ni kweli andiko la wakubwa...I salute....waswahili wanasema anayedhani amesimama....
 
Kama coach ndio mchezaji na refa wakati huo huo,

Mbona watazamaji hawafurahii mchezo!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…