Uchaguzi 2020 Japo mimi mpinzani Ila CCM wanafanya kampeni za kistaarabu sana mwaka huu

Uchaguzi 2020 Japo mimi mpinzani Ila CCM wanafanya kampeni za kistaarabu sana mwaka huu

chinchilla coat

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2016
Posts
5,107
Reaction score
10,969
Mara nyingi naegemea Upinzani Ila leo nawapongeza CCM kwa walivyoanza kampeni zao. Hawajawashambulia Wapinzani kwa kejeli au matusi kama ilivyokuwa mwaka 2015 ambapo Lowassa alitukanwa sana kuhusu Afya yake, ambaye Sasa hivi wapo naye huko.

Lakini tangu waanze mpaka sasa naona Magufuli akielezea tu kazi alizofanya na kuahidi atakazofanya endapo atachaguliwa, wapambe wake wengi nao hawajajilita kushambulia Sana Wapinzani

Japokuwa kuna vijembe mara moja moja Ila sio mbaya Ila Kuna tatizo Huko Mara ambapo nimesika yupo mpiga kampeni kamtukana mgombea wa Upinzani m*alaya nadhani chama kitamkemea.

Nashauri Upinzani pia usijikite sana kumshambulia Magufuli, japo najua Ni lazima ashambuliwe sababu ndio mtendaji mkuu wa Serikali, lakini akosolewe kisera zaidi.

Ikiwa hivi kampeni zetu zitakuwa za kistaarabu kuliko za nchi nyingi Africa Mashariki na pengine nitapata pride ya kuwa Mtanzania tena.
 
ni kwa vile wametutukana Watanzania kwa miaka karibia 5 sasa walipokuwa wao ndiyo mabosi.
sasa hivi tunapoelekea kwenye uchaguzi, sisi umma (Watanzania) ndiyo mabosi wao, lazima washike adabu!
 
ni kwa vile wametutukana Watanzania kwa miaka karibia 5 sasa walipokuwa wao ndiyo mabosi.
sasa hivi tunapoelekea kwenye uchaguzi, sisi umma (Watanzania) ndiyo mabosi wao, lazima washike adabu!
Hahaa, kumbe?
 
Sina uhakika Sana Kama wanafanya campaign za ustaarabu labda wacha tusubiri manake ndo campaign zimeanza anza hatujuhi Sana baadae.

Jambo ambalo binafsi naliona kwa uhakika ni ukweli kwamba CCM wako organized kwenye campaign zao. Wanajua Sana protocol, order na administration ya mkutano yao.

Kwenye pitapita zangu , nilijikuta Arusha na nikahudhuria campaign za chadema. Bila kuuma maneno that meeting was poorest ever.

Mitambo mibovu, uchelewaji kwenye tukio kwa wahusika, mgombea kutosikika kwenye vipaza sauti nk. Team ya campaign ya chadema kwa ushauri wangu inabidi iiige timu ya campaign ya ccm.
 
CCM wamejipanga vyema...wanataja waliyo tekeleza kwa kishindo then wanataja watakayo yafanya miaka 5 ijayo
 

Hii mahsusi kwa wanaopozi kama wapinzani.

Mwaka huu asishangae mtu hata bashiri, jiwe, au chakubanga wakijinasibu nao kuwa ni wapinzani.

Tuwe mkao wa kusikia mengi.

Kalinye kalinye la Lissu haliwaachi wengi na akili sawa.
 
Magufuli ni Rais awezi ku act kama mgombea Urais...Magufuli anao uzoefu anajua kazi za serikali
 
Afadhali umeliona hilo mkuu,waelezee labda watabadilika,CCM oyee...
 
Back
Top Bottom