Jaribio la kutapeliwa leo

Jaribio la kutapeliwa leo

Vikintu

JF-Expert Member
Joined
May 26, 2021
Posts
2,051
Reaction score
3,162
Habari wanajukwaa. Leo nimepigiwa simu kutoka namba +255673099097, mpigaji akijitambulisha kuwa anafanya kazi makao makuu ya vodacom. Nilivyosikia hivyo tu, nikajua matapeli hawa. Basi nikajifanya mjinga kwenda naye taratibu ili asishtuke.

Alisema kuwa kuna mtu katuma pesa kwenye account yangu ya voda kimakosa, na akataka kujua kama nimepata message yoyote. Mimi nikamwambia, akate simu kwanza niione message yenyewe. Hakutaka kunipa muda huo, badala yake akaniuliza kiasi cha pesa kilichopo katika account yangu. Aliposisitiza sana nikaamua kudanganya kwa kumtajia kiasi kikubwa. Bila hata kunipa fursa ya kutazama kama kuna message yoyote akaishia kunitukana tusi baya sana huku akisema haioni pesa hiyo.

Kiasi chenyewe nilichomtajia ni shs 250,000, ambazo kwakweli hazikuwemo. Alivyomaliza kutukana akakata simu.

Nimebaki na maswali kadhaa. La kwanza, namba aliyotumia kupiga nadhani ni ya mtandao wa Tigo, huku akijitambulisha kuwa yuko vodacom, sijui ni kwanini?

Pili, alijuaje kuwa kweli sina pesa yoyote kwenye account yangu ya mpesa?

Nawasilisha.
 
Laki 2.5 ndio kiasi kikubwa??? Tafuta hela ndugu yangu
Kitu gani ambacho hakieleki hapa? Yeye kasema ameamua kumwambia kiasi kikubwa kulinganisha na uhasiliwa wa kilichopo kwenye account yake. Na reason behind ni kwamba alitaka kuchezea akili za tapeli hivyo akasema kiasi ambacho ni reasonable na tapeli ataamini kwa urahisi.
 
Habari wanajukwaa. Leo nimepigiwa simu kutoka namba +255673099097, mpigaji akijitambulisha kuwa anafanya kazi makao makuu ya vodacom. Nilivyosikia hivyo tu, nikajua matapeli hawa. Basi nikajifanya mjinga kwenda naye taratibu ili asishtuke.

Alisema kuwa kuna mtu katuma pesa kwenye account yangu ya voda kimakosa, na akataka kujua kama nimepata message yoyote. Mimi nikamwambia, akate simu kwanza niione message yenyewe. Hakutaka kunipa muda huo, badala yake akaniuliza kiasi cha pesa kilichopo katika account yangu. Aliposisitiza sana nikaamua kudanganya kwa kumtajia kiasi kikubwa. Bila hata kunipa fursa ya kutazama kama kuna message yoyote akaishia kunitukana tusi baya sana huku akisema haioni pesa hiyo.

Kiasi chenyewe nilichomtajia ni shs 250,000, ambazo kwakweli hazikuwemo. Alivyomaliza kutukana akakata simu.

Nimebaki na maswali kadhaa. La kwanza, namba aliyotumia kupiga nadhani ni ya mtandao wa Tigo, huku akijitambulisha kuwa yuko vodacom, sijui ni kwanini?

Pili, alijuaje kuwa kweli sina pesa yoyote kwenye account yangu ya mpesa?

Nawasilisha.
Sasa kama alijua huna pesa, unadhani kwa nini alikupigia?
Wale huwa wanabeti. Huyo aliingiwa na hisia utakuwa unamdanganya.
 
Back
Top Bottom