Jasho lenye harufu isiyo ya kawaida

Vituka

JF-Expert Member
Joined
Nov 9, 2011
Posts
2,266
Reaction score
1,264
Ninaishi na mtoto wa kike wa miaka 12, alikuwa anaishi kijijini na bibi yake na kwa sasa naishi nae huku mjini. Huyu mtoto kifupi kakulia mazingira magumu kimaisha na amedumaa pia, ana miaka 12 lakini nimempeleka shule wamemkubali darasa la kwanza. Tatizo lake ni kwamba ana sweat sana, yani usiku ile sehemu yote aliyolala inakuwa imeloa jasho. Halafu jasho lake si la kawaida kabisa, yani harufu yake ni kali sana kama ya kitu kilicho chacha. Naomba kujuzwa kama hili ni tatizo la kiafya au nini.
Nawakilisha.
 
Kama huyo mtoto umemtoa eneo la baridi na umemleta eneo la joto mimi naona ni kawaida tu labda watakuja wengine na mawazo ya kisayansi zaidi, lakini nakumbuka hata mimi nimesomea kijijini toka primary school mpaka High School Kibosho, nilipofika Chuo kikuu Dsm mahala penye joto nilikuwa natoa jasho jingi na lenye harufu ya kitu kilichochacha lakini mda ulivyozidi kwenda hali ilibadirika mpaka sasa 'sisweti' kiasi kile na hata 'nikisweti' harufu inakuwa ni ile ya kawaida ya jasho ambayo naipunguza kwa manukato naendelea kudunda:ranger:
 
Hili linatokana na mazingira zaidi wala usianze kupata hofu, kadri atakavyokuwa ana badilisha vyakula hali itatoweka.
 
vile vile mwambie kila siku apake ndimu kwenye kwapa zake.jasho likiwa linanuka huwa haipendezi,hasa ukikaa na watu karibu.apake mara 2 kwa siku,asubuhi na usiku.ndimu inasaidia kukata harufu ya jasho
 
hakikisha pia anakunywa maji kwa wingi itamsaidia
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…