OCC Doctors
Senior Member
- Jul 20, 2018
- 113
- 172
[Hyperhidrosis] Mara nyingi huwa ni jasho inayotoka kwenye viganja vya mikono, unyayo wa miguu, sehemu za kwapani, na sehemu za makalioni [haswa kwa wanaume] hii hutokana na tezi zinazozalisha jasho kufanya kazi kupita kiasi. Lakini hali ya kutokwa na jasho kwenye mikono na miguu pekee hii hufahamika kama [palmoplantar hyperhidrosis] ni jasho kutoka kwa wingi kwenye viganja vya mikono na vikanyagio vya miguu, Sababu kubwa huwa ni unene uliopindukia [obesity], au ugonjwa wa [gout], au kuelekea kukoma kwa hedhi [menopause], pia huwa ni moja ya dalili ya mwili kuwa na sumu, au ishara ya kisukari, [diabetes mellitus], na vilevile huwa ni ishara ya mvurugiko wa vichocheo mwilini [hormonal imbalance-overactive thyroid gland).