LGE2024 Jawadu Mohammed: Chama kinachotaka kupambana na Rais Samia 2025 kijitafakari

LGE2024 Jawadu Mohammed: Chama kinachotaka kupambana na Rais Samia 2025 kijitafakari

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

Papaa Mobimba

JF-Expert Member
Joined
Jan 27, 2018
Posts
882
Reaction score
3,337

Chama Cha Mapinduzi kimesema kwamba uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika Novemba 27, 2024 utatuma salama kwa mtu au chama chochote kinachotaka kupambana na Rais Samia Suluhu Hassan mwaka 2025 huku kikidai kuwa atakeyetaka kuthubutu ajitafakari upya kama ana sifa za kupambana.

Kauli hiyo imetolewa na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Mkoa wa Dodoma, Jawadu Mohammed alipokuwa akiwanadi wagombea wa nafasi za uenyekiti na ujumbe wa Serikali za mitaa, vitongoji na vijiji katika kijiji cha Keikei kata ya Keikei wilaya ya Kondoa mkoani Dodoma.

Aidha amesema baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kuachiwa nchi na Hayati Dkt. John Pombe Magufuli watu wengi pamoja na baadhi ya vyama vya siasa walidhani Rais Samia hatoweza kuongoza nchi lakini imekuwa tofauti kwani ametekeleza miradi ya maendeleo kwa kiasi kikubwa.

Jambo TV
 
Nchi ya kusadikika hata jiwe linaweza kuwa rais, maana upuuzi wowote unaoongea chawa wanakukenulia mi meno inakuchekea. Unauza kila rasilimali ya nchi, unajichotea fedha za wizi michawa inakutukuza na kukusifu.
 

Chama Cha Mapinduzi kimesema kwamba uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika Novemba 27, 2024 utatuma salama kwa mtu au chama chochote kinachotaka kupambana na Rais Samia Suluhu Hassan mwaka 2025 huku kikidai kuwa atakeyetaka kuthubutu ajitafakari upya kama ana sifa za kupambana.

Kauli hiyo imetolewa na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Mkoa wa Dodoma, Jawadu Mohammed alipokuwa akiwanadi wagombea wa nafasi za uenyekiti na ujumbe wa Serikali za mitaa, vitongoji na vijiji katika kijiji cha Keikei kata ya Keikei wilaya ya Kondoa mkoani Dodoma.

Aidha amesema baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kuachiwa nchi na Hayati Dkt. John Pombe Magufuli watu wengi pamoja na baadhi ya vyama vya siasa walidhani Rais Samia hatoweza kuongoza nchi lakini imekuwa tofauti kwani ametekeleza miradi ya maendeleo kwa kiasi kikubwa.

Jambo TV
CHAWA katika ubora wake. CCM hakiwezi kufanya makosa kuwaletea wananchi mgombea asiyekubalika na asiye na sifa kwa kuwa na makandokando mengi.
 
Back
Top Bottom