Mashabi wa Simba wanalijua soka na wataungana na mimi kwa hili nililolisema kuhusu uwezo wa wachezaji Unadhiilisha ushamba wako kwenye soka, naanza kuamini kua kuna mashabiki wamependa mpira baada ya kuanza kubet wewe ni mmoja wao
Maana wachezaji unaowataja wote hao hawazidi misimu mitatu hapa bongo, Hili linadhiilisha ushamba na ugeni wako kwenye soka, inaonekana hata baadhi ya wachezaji niliowataja haujawashuudia wakiwa kwenye ubora wao
Wewe ni tomaso wa Soka, Aziz k ni One season Wonder, ni mchezaji wa level za kawaida sana, hata nusu ya uwezo naperfomance ya Chama hajafika
Inaonekana Okwi unamsikia tu hukuwai kumshuhudia
Maamdiko yako yanaonyesha umetoka kijijini juzi mechi yako ya kwanza ni Simba dhidi ya Asec, Baada ya kutoka bush ukafikia kwa shemeji yako akakulazimisha kushabikia utopolo
Mshamba wa soka kaa chini jifunze na ufatilie vitu vipo mitandaoni
Mimi nimeishudia Simba ya Moses Mkandawile , Idd pazi, Rafael paul , Kajole, Mtemi Ramadhani, Twalib Hilal, (Super Kiwelu Musa) Zuberi Magoha nk, Wanakimbia wanagoma kuendelea na mechi Yanga walipewa penalt ambayo Yanga wangepata katika dakika izo za lala salama Yanga angetangazwa Bingwa wa Tanzania.
kwakua walikua wamefungana point na Simba.
Pale Shamba la bibi kipindi cha pili goli la kaskazini.
Goli lisilo lala na njaa.
Kitasa wa Yanga Hisiaka Hasan anachukua mpira ili akapige penalty Simba wamegoma.
Jukwaa la Yanga linalipuka kwa shangwe wakati mwamba Hisiaka Hassan (Chukwu ) ana kwenda kupiga tuta la kuipa Yanha ubingwa.
Na kwakua anafahamika kwa uwezo wake wa kupiga penalty Simba waka goma na mechi ikavunjika baada ya refa kusubiria kwa dk 15 na simba kukomaa penalty isipigwe.
Kesho yake Said Elcmaamry anaitangaza Yanga Bingwa 1985 kwa kupewa point 2 na magoli 2.
Sas usiniambie habari za okwi mtoto wa juzi ndio maana niliandika katika miaka 30 toka sasa kwakua ukirudi nyuma Tanzania kulikua na mafundi wengi.
Walikuwepo wakina Ngurungu, Juma Mkambi, Adolf Richard, Thuen Ally, Mtemi Ramadhan, Zamoyoni Mogela , Omary Husen ata kizazi cha Method Mogela, Issa athuman, Michael paul , Malota n.k kilikua na watu na ndipo mpira wa Tanzania ulipo ishia mwaka 93/94 .
Baada ya apo hakukua na wachezaji wa maana ndio kinakuja kizazi chenu cha okwi, boban, chuji, Haruna Nionzima ,mafisango, sunzu yaani ni upuuzi mtupu unao ita wachezaji.
Kuna mtu aliitwa Doto ruta Mokil(freezer) alikua aki ingia sub pale Yanga mwaka 1983 sasa fikiria icho kikosi kilikuaje.
Uyo Mokili chukua uwezo wa Ateba+ Ahoua+ Dube na bado alikaa Bench.
Sasahivi tuna angalia Copy za wacheza mpira ila si mpira.
Mstari wa mbele wa Simba ya 1993 hakuna ata mchezaji mmoja wa Simba ya sasa atayepata nafasi ata benchi.