Je alichotabiri Nyerere tayari kinatokea sasa?


Ndio maana hapa tutakaa tunabishana mpaka asubuhi. Unakataa kulinganisha Botswana na Tanzania. Lakini yakija masuala ya ujamaa mpo tayari kulinganisha Tanzania na Marekani, Ufaransa au Uingereza. Huo kwamba hapa unaBugi step.

Kuhusu feudalism, Mirambo, Mkwawa na ... walikuwa ni slave traders. Sijuhi kama hii itakusaidia kutofautisha kati ya feudalism na slave trade.

Ukoloni mamboleo ni myth iliyotungwa na viongozi kama Nyerere walioshindwa kuleta maendeleo katika nchi zao. Viongozi hawa na wananchi wao walikuwa na matumaini makubwa ya kupata maendeleo baada ya kupata uhuru.

Lakini waliposhindwa kuleta maendeleo, wakaanza kumtafuta mystical mchawi (mkoloni mamboleo)>
 
Zakumi,
Yaani unathubutu kusema Mkwawa na Mirambo walikuwa slave traders!.. ama kweli huijui historia ya nchi yako na ndio maana hufahamu Ujamaa..
Mkuu silinganishi Tanzania na Marekani ila nasema hatua walizopitia kama ulivyozungumzia steps ktk hoja iliyopita.. Kumbuka nimesema mimi napima winbgi wa kamasi, sipimi ukubwa au udogo wa pua... umeanzisha mwenyewe nami najibu hoja yako kulingana na hoja uliyotanguliza..
Maendeleo ya nchi hizi yalipatikana sii kutokana na ukubwa au udogo wa nchi zao ni steps ambazo ni pamoja na kupitia Ujamaa kwanza kabla ya Kufikia Ubepari kamili unaouona..
Mkuu darasa linapanda au unafanya makusudi..
 

Unategemea mtu ambaye hakupitia shule za ujamaa, kupandisha darasa. Anyway Mirambo na Mkwawa walikuwa ni slave traders. Na kuna uthibitisho mkubwa.

Kwa sababu walikuwa ni weusi na watu walikuwa wanatafuta heroes, basi historia imewalinda.

Thread hii sio kuhusu wao sitaendelea kutoa facts.
 
Lakini mkuu, yote haya unayoyasema sivyo yalivyo sasa na sio yanayosababisha tuwe hivi tulivyo sasa. Chama tawala sio kinachoshika hatamu (walau kisheria/kikatiba). Mengi yamebadilika, na hali imekuwa mbaya zaidi.

Sio kwamba imekuwa mbaya kwasababu za kuondoa chama kushika hatamu, bali kwa kufuata sera zisizofaa na ambazo wala sio zilizobuniwa na/au kuwekwa na Nyerere.
 
Mkuu Zakumi, nakubaliana na mengi uliyotangulia kusema hapo juu. Hata mimi siamini kuwa Ujamaa ungetusaidia sana katika kuleta maisha bora kama tunavyotamani. Labda kama Ujamaa huo ungerekebishwa na kuwa wenye ushirikishi zaidi, na uwe na mix ya kibepari kidogo. Hayo nayaachia hapo.

Kuhusu Katiba ya vyama vingi. Ni kweli kuwa iliundwa na chama tawala, chama ambacho bado ni CCM mpaka leo. Kwa kuwa iliundwa na chama hicho ambacho Nyerere alikiongoza, na kwa kuwa Katiba ilibadilishwa wakati yeye hakiongozi chama hicho. Si sahihi kumhusisha Nyerere na mapungufu yaliyofanywa na walioitunga Katiba hiyo baada ya yeye kung'atuka. Kwakuwa sie yeye aliewaambia waitunge hivyo. Na zaidi, kumbukumbu zinaniambia kuwa alipinga mengi yaliyokuwa yakifanywa na hao walitunga Katiba hiyo.

Ni kweli kuwa Katiba ya nchi haina maslahi kwa nchi yetu hasa katika kipindi hiki. Haiweki usawa wa kisiasa, haitoshi kisheria na haina tija kwa maendeleo ya nchi. Vipengele vingi na vinavyolalamikiwa ndani ya Katiba yetu, viliwekwa wakati Nyerere hayupo (1992). Hivyo pia, si sahihi kumlaumu yeye kwa makosa ya waliofanya hivyo.

Mkuu, ninachokisema mimi ni kwamba, matatizo yetu yanasababishwa na sisi wenyewe na uongozi wetu wa sasa baada ya Katiba mpya tuliyonayo na sera mpya tunazotumia. Hutuna tena dira, sera wala mwelekeo sahihi wa kutatua mambo muhimu katika nchi na kuleta maendeleo ya kudumu.
 
Kuhusu katiba hakuna mabadiliko yoyote ya maana na ndio maana CCM wanashinda tena kisheria kwa kutumia bajaji wakati CHADEMA wanatumia Helikopta.
Vipengele kidogo (kama kweli ni kidogo) vilivyobadilishwa ndivyo vyenye madhara makubwa kwa Taifa. Vipengele hivyo ndivyo vinavyonyima vyama vya Upinzani fairness katika ushindani. Ndivyo vinavyosababisha matatizo mengi tuliyonayo. Inaweza kuonekana kuwa ni mabadiliko kidogo, lakini yenye madhara makubwa.

Kuhusu sheria wakati wa Nyerere I beg to differ. Kama sheria zilikuwa zinafuatwa kwanini waandishi wa habari hawakuwa huru au hatukuwa na uhuru wa kufanya tunavyotaka?

Mkuu, kufuata sheria na kutoa uhuru haviendani moja kwa moja.

Sheria zilizowekwa zinaweza kunyima uhuru, na kuzifuata ikawa ni kufuata sheria. Wakati huo huo, kutozifuata ikawa kuvunja sheria.


Hapana. Nadhani hatukuelewana.

Ninachosema kuhusu uhuru ni kwamba, tunapotea kwa kufuata misingi isiyofaa. Hatutaki kujirekebisha, na hali inabadilika na kuwa mbaya siku hadi siku. Simaanishi uhuru wa kukomboa nchi kutoka kwa wakoloni kama alivyofanya Nyerere. Bali nazungumzia mapinduzi ya kweli ya fikra na nia ya kuleta mabadiliko muhimu kwa ustawi wa Taifa. Hivi sasa, hakuna dalili za kufuata njia sahihi.
Maendeleo yanayoweza kupatikana kwa (mi)fumo tunayoitumia hivi sasa, si maendeleo endelevu. Ni maendeleo ambayo mtu ili afanikiwe anatakiwa adhulumu, aibe rasilimali za umma, au avunje sheria kwa namna moja ama nyingine. Na hii ndio inayosababisha viongozi kutushia wafanyabiashara kupakaziwa kodi au hata kufuatiliwa na TRA na kadhalika. Inatakiwa kuwe na mfumo unaofaa ambao kila mtu anaweza kufanya shughuli zake kihalali na kupata riziki yake kihalali na kwa uendelevu. Kwa sasa hiyo si rahisi hata kidogo
.
 
nyerere hakutabiri kitu, alitumia lugha ya kisanii kusema kitu kilichoonekana wazi kuwa hakiepukiki (which is more like projection than prophecy).

Wengine watasema hata kuwa yeye alijivika huo unabii mwenyewe kwa kusema "wataibuka manabii wenye kuhubiri haki kwa kuwahukumu wengine" wakati yeye mwenyewe akihubiri haki kwa kuwahukumu wengine.

Sasa nabii/mtabiri nani hapo?
 
Naona tunasogea sogea tu, haya twendeni tu, yamechipukia Uganda haya....
 

Zakumi, neno msomi lina maana pana sana maana hata mganga wa kienyeji anayezungumzia kazi yake kwa kuielewa vyema naye pia ni msomi wa fani yake.

Huwezi pia ukaziita fikra za mwingine ni potofu na za kwako si potofu. Hapa tukubali tu kwamba tunakubali kutokubaliana! Kama wewe unaona Ujamaa haukukusaidia kitu, fine. Unasema Ujamaa usingeliweza kuwa na shule hata ya chini ya mbuyu bila misaada. Naomba unitajie nchi ngapi za Kiafrika ambazo zilifuata siasa za Kibepari zilizosomesha watu wake bila misaada?

Kutafuta na kupata misaada ili kuweza kusomesha wananchi kwa misingi ya Kijamaa badala ya misaada hiyo kutafutwa kwa misingi ya Kibepari na kunufaisha/kusomesha wachache, ndicho kilichotusomesha sisi watoto wa maskini wa enzi hizo.Wassisi wa Taifa hili wangeamua kufuata Ubepari na kuwa Mabepari akina sie tusingechungulia kwenye chumba kinachoitwa darasa. Kwa hiyo tuna kila sababu ya kuwa na fikra unazoziita 'potofu' za kusifia kuelimishwa na Ujamaa.

Usijidanganye Zakumi, midhali wewe ni Mtanzania na wazazi na mababu zako walitoka Tanganyika/Tanzania hawakuzamia kutoka Uajemi na kwingineko moshi moshi wa Ujamaa lazima utakuwa umekunufaisha kwa namna moja ama nyingine.
 
kuendelea kumlaumu nyerere ni kupoteza muda cha mbolea ni kuangalia nini kifanyika kukabiliana na ukata uliopo sambamba na mbinu za kuwezesha kuhakikisha tunapata vichwa bungeni viweze kutunga sheria zitakazokabiliana na matatizo ya sasa
 

Zakumi,

Tafsiri ya Ujamaa kwa kiingereza ni Socialism. Tanzania tangu Uhuru ni nchi ya Kijamaa - A Socialist Country. Nadhani imo ndani ya Katiba kama haijabadilishwa hivi karibuni. Itikadi ya TANU, Chama cha Mapinduzi ni "Siasa ya Ujamaa na Kujitegemea" kwa kiingereza ni "Socialism & Self-Reliance". Chama cha Labour cha Uingereza kinatambulika kama "Democratic Socialist Party" kwa tafsiri yangu mie ni Chama cha Demokrasia na cha Kijamaa.

Ujamaa wa Waasisi wa Taifa letu hauna uhusiano wowote na Ujamaa ambao umo vichwani mwa wengi wanaopinga huo Ujamaa wakiulinganisha Ujamaa huo na ule ulioshindwa na kuhitimisha Cold War.

Ujamaa wa Mwalimu Nyerere (bora niseme kuwa ni Ujamaa wake maana hata waliouasisi wanaukana) ulijikita kwenye "Misingi ya Ujamaa" ambayo ni endelevu kama ambavyo Chama cha Labour cha Uingereza mpaka leo kinajitambulisha kama ni Socialist Party kutokana na MISINGI yake.

Misingi ya 'Ujamaa wa Nyerere' ilikuwa ni UTU na HAKI SAWA KWA WOTE. Taifa Huru la Tanganyika na baadaye Tanzania lilianza kujengwa chini ya misingi hiyo ya HAKI SAWA KWA WOTE.

Kwa Misingi hiyo ya Ujamaa ndipo Serikali ya Kijamaa ya Tanganyika/Tanzania ilifanya kila juhudi kupata pesa ili hata watoto wa maskini nao waweze kupata elimu bure, ili elimu hiyo iweze kuwaondolea wananchi ujinga na umaskini kwa mpigo. Zahanati na hospitali zikajengwa kwa njia mbalimbali za misaada na nguvu za wananchi kwa kujitolea. Dawa mahospitalini zilipatikana bure kwa Afya bora kwa manufaa ya Wananchi waliokuwa hawana uwezo na hata waliokuwa na uwezo.

Kwa Misingi hiyo ya Ujamaa, viongozi walafi wakawekewa 'gavana' ndani ya Azimio la Arusha. Badala ya fedha za Umma kwenda mifukoni mwa 'mafisadi' zikapelekwa kupanua na kujenga viwanda. Tanzania ikajitosheleza kwa viwanda vya kila kitu. Wakaibuka 'mafisadi' wapenda utajiri wa haraka haraka wakashirikiana na MABEPARI, wakahujumu na kuua kila kitu!

Ujamaa haukuzuia Wafanyabiashara binafsi kufanya biashara zao. Walifanya biashara zao kwa misingi ya haki bila ubabaishaji. Wababaishaji waliihama nchi kwenda kufanya ubabaishaji wao kwingineko!

Zakumi 'Ujamaa' ukitumiwa vizuri unaweza sana kuwa alternative ya Ubepari hata kwa zama hizi!
 

Kwa kutumia ufafanuzi wako kuhusu msomi. Ina maana hata yaya aliyebobea kwa kazi yake ni msomi. That's wondeful. Pamoja na hayo yote, ninakataa kuitwa msomi.

Kuhusu kutumia fikra potofu: I take inspiration from you guys. Si mlikuwa mnasema zidumu fikra za mwenyekiti wa CCM. Na mlipogundua kuwa kuna zingine alichemsha. Mkaanza kusema kuwa zidumu fikra sahihi za mwenyekiti wa CCM. Swali langu, je zile fikra zisizo sahihi mliziweka katika kundi gani?

Kwa upande wangu fikra zisizo sahihi ni potofu. Labda kama kuna msamihati mwingine wa kutumia, naomba unifahamishe.

Afu unanilazimisha kukubali kuwa ujamaa unilisaidia au kunisomesha, wakati watu mahiri hapa JF waliobobea maisha ya Mwalimu na siasa za Ujamaa wanakubaliana na usemi wa mwalimu kuwa Ujamaa haukuwa implemented Tanzania.

Mwalimu Nyerere kwa maneno yake mwenyewe anasema tusiulaumu ujamaa kwa sababu haukuwa implemented nchini. Sasa kama ujamaa haukuwa implemented kwanini basi nikubali kuwa nilifaidika na moshimoshi wa ujamaa? It seems to me kuwa wapenzi wa Ujamaa hakuchoka kusoma vitabu vya Abunuwasi. Hivyo kusema ujamaa ulinisomesha ni sawa na kukubali kuwa Abunuwasi aliweza kula ugali kwa kutumia arufu ya kitoweo kilichopikwa katika nyumba ya jirani.

Na kama ujamaa haukuwa implemented Tanzania, basi hakuna nchi ya kiAfrika iliyokuwa ya kijamaa au kipebari. Na ndio maana wote tupo kwenye ligi ya umasikini.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…