Uchaguzi 2020 Je, CCM kutumia kanuni za Dini na taratibu za kanisa katoliki za misa kuomba kura ni dharau kwa waamini wa kikatoliki?

seedfarm

JF-Expert Member
Joined
Feb 9, 2020
Posts
260
Reaction score
2,655
Members, Ushahidi wa video umeambatanishwa ukionyesha jinsi wanachama wa CCM wakikebehi na kudharau taratibu na kanuni za kanisa katoliki kwa kugeuza muundo na mifumo na kuwa kiitikio cha ccm

Rai yangu haya mambo yasipokemewa, Kuna watu wataanza kuwaigiza waislam na italeta shida na taabu sana

Hii video ni ya kukemea na kupingwa na kila mtu hasa wana CCM wenyewe

Watu kugeuza sala na taratibu za watu iwe Dua au Maombi na kuweka viitikio vya CCM ni dharau kubwa

Uchaguzi usiwatoe watu ufahamu na kuanza kuleta dharau kwa imani za watu

Huyo aliyefanya hayo akemewe na wana ccm wenyewe

Video imeambatanishwa
Your browser is not able to display this video.
 
Watu kugeuza sala na taratibu za watu iwe Dua au Maombi na kuweka viitikio vya ccm ni dharau kubwa

Elezea kinagaubaga aina ya sala na taratibu za wakatoliki zilizotumika/zinazotumika vibaya na ccm.
Sie wengine simu hazina uwezo wa kufungua videos.
 
Linapokuja suala la madaraka CCM wako tayari kuua ili wayapate. Dharau kwa dini kupitia wanaCCM hii si ya kwanza. Unakumbuka Nabii tapeli mmoja pale Dodoma alitoa cover ya biblia na kuweka iliyoandikwa CCM na hakukemewa? Leo mtu anajitoa ufahamu na kufuatisha tone ya kipekee ya Kikatoliki katika kuendesha Misa na kuingiza maneno ya kisiasa na bado chama na NEC wanaona ni sawa tu.
 
Viongozi wa kikatoliki wenyewe si waunga mkono juhudi tu ref: Askofu Nyaisonga wacha wafanye dhihaka mpaka kila mtu atakapoona dini ni upuuzi flani kisha ndio tuonyeshane makali.
 
Hizo tabia wanazo wafuasi wa Illuminat, no wonder maccm yatakuwa ma illuninat
 
Nitashangaa sana kama Baraza la maaskofu katoliki ( TEC) wakikaa kimya kwenye hili
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…