Je Communication skills inayofundishwa vyuoni kweli inareflect kile kilichokusudiwa?

Je Communication skills inayofundishwa vyuoni kweli inareflect kile kilichokusudiwa?

Solile

Member
Joined
Jul 26, 2009
Posts
24
Reaction score
10
Salamu kwenu
Baada ya kumsikiliza mh Livingstone Lusinde akimwaga hotuba yake, kilichoniijia akilini ni kwamba kweli hizi communication skills tunazofundishwa Vyuoni ndio zinapaswa kuwa hivyo.
Binafsi nimesoma Ardhi wakati ikiwa uchini ya UDSM na Prof Maarafu wa UDSM alikuwa anafundisha pale lkn haswa kitu ambacho tulikuwa tunafundishwa ni English language vitu kama tenses, verbs na kadhalika, lkn baada ya kusoma Masters (nchi za wenzetu) nikasoma Communication skill, iliyokuwa na sura tofauti kabisana ya ARDHI na kuniacha na maswali kuhusu communication skill zetu.
Wenzetu wanafundisha communication skills kama namna ya communication sehemu mbali mbali, makazini, katika jamii katika presentations na mengineyo
Ukijaribu kuangalia wahitimu mbali mbali wa vyuoni kwetu, namna wanavyo communicate katika emails, au barua hata ku-approach media inasikitisha.
Matokeo yake ndio kama haya, baadhi ya waheshimiwa wanapoenda kuwasilisha ujumbe kwenye jamii bila hata kuanalyse makumdi ya watu atakaowautubia na kule anachoutubia. Bila kusahau hata ma super star wetu huwa wanajiongea yanayokuja bila kujali matokeeo ya kauli zao.
 
aisee ni kweli kaka hata ss huku chuo hyo comm.skills inavyofundshwa mhhhhhh!we acha tu
 
Ni kweli course za Communication skills zinazotolewa nchini zina mapungufu.Binafsi nilipokuwa naianza course hiyo, wakati nikiwa chuo ,nilikuwa na matarajio kuwa,hadi kufikia mwisho wa muhula ,nitakuwa nimepata maarifa na stadi za kutosha kunipa umahiri katika eneo la mawasiliano,hasa ya umma.Kwa bahati mbaya kabisa,hilo halikutokea.Nilibaini kuwa modules hazikubeba maarifa yaliyokidhi matarajio.Ni kama vile tulikuwa tunasoma somo la kiingereza tu.
Wengi wa wahadhiri katika vyuo vyetu wana msemo kuwa:"at university ,students learn how to learn," wakimaanisha kamwe haiwezekani kufundishwa mambo yote muhimu ndani ya semester moja ,wakihimiza wanafunzi wajitafutie maarifa kwa bidii zao.Kuitikia wito huo,nilinunua kitabu kiitwacho "Public Speaking for College Students and workers".Hakika, kitabu hiki kimesheheni maarifa na stadi za kutosha ,na napendekeza iwapo yupo miongoni mwetu mwenye kiu ya kuwa mahiri katika nyanja ya mawasiliano, atafuta kitabu hicho..
 
Wanashindwa kujua kipi kinatakiwa kufundishwa kwa wanafunzi wa level hiyo na kimsingi kinachofundisha hapa Tz ni Englsh ambayo ni structural based badala ya Communicative English kitu kinaitwa BICS,yaani (Basic Interperson Communicative Skills)
 
Comm. Skills inasaidia! Mimi nimesoma kuhusu presentation, academic writiing, speaking, listening.... Zimenisaidia sana. Changamoto kumbwa ni kudumisha/ kuendeleza kwa muda mrefu zile mbinu nilizosoma
 
Salamu kwenu
Baada ya kumsikiliza mh Livingstone Lusinde akimwaga hotuba yake, kilichoniijia akilini ni kwamba kweli hizi communication skills tunazofundishwa Vyuoni ndio zinapaswa kuwa hivyo.
Binafsi nimesoma Ardhi wakati ikiwa uchini ya UDSM na Prof Maarafu wa UDSM alikuwa anafundisha pale lkn haswa kitu ambacho tulikuwa tunafundishwa ni English language vitu kama tenses, verbs na kadhalika, lkn baada ya kusoma Masters (nchi za wenzetu) nikasoma Communication skill, iliyokuwa na sura tofauti kabisana ya ARDHI na kuniacha na maswali kuhusu communication skill zetu.
Wenzetu wanafundisha communication skills kama namna ya communication sehemu mbali mbali, makazini, katika jamii katika presentations na mengineyo
Ukijaribu kuangalia wahitimu mbali mbali wa vyuoni kwetu, namna wanavyo communicate katika emails, au barua hata ku-approach media inasikitisha.
Matokeo yake ndio kama haya, baadhi ya waheshimiwa wanapoenda kuwasilisha ujumbe kwenye jamii bila hata kuanalyse makumdi ya watu atakaowautubia na kule anachoutubia. Bila kusahau hata ma super star wetu huwa wanajiongea yanayokuja bila kujali matokeeo ya kauli zao.

Naona unakosea kumwingiza Lusinde ktk kundi hilo, mtu asiye jieshimu ataitwaje mweshimiwa? tafadhali muweke ktk kundi analo stahili.
 
By cZg from ETU: Mnania nzur saana wadau wa elimu Tanzania lakini hamuongelei mikakati ya uboreshaji elmu zaidi ya ukosoaji sasa ndo kusema ili nami mtoto wa mkulima nifahamu hiyo 'communication skills' nisome shahada ya udhamil nje? Tutafute ufumbuzi Aksante sana Aksante saaana
 
Ni vyema sie tumeliona tatizo, wenye ufumbuzi karibuni sana
Kuna Prof mmoja wa UDSM( sitaki kumtaja lkn ni mzee mmoja anafundisha hadi hivi vyuo vya Ardhi na MUCHs) siku anatoa intro kwa first year ya commucation skills alisema anafundisha english kwa sababu waliona english bado ni shida sana kwa wanafunzi nyuooni.

By cZg from ETU: Mnania nzur saana wadau wa elimu Tanzania lakini hamuongelei mikakati ya uboreshaji elmu zaidi ya ukosoaji sasa ndo kusema ili nami mtoto wa mkulima nifahamu hiyo 'communication skills' nisome shahada ya udhamil nje? Tutafute ufumbuzi Aksante sana Aksante saaana
 
Back
Top Bottom