KERO Je, Dar kuna Mgao wa Maji? Wizara ya Maji tupeni majibu. Eneo ulilopo hali ya upatikanaji wa huduma hii ukoje?

KERO Je, Dar kuna Mgao wa Maji? Wizara ya Maji tupeni majibu. Eneo ulilopo hali ya upatikanaji wa huduma hii ukoje?

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

Precious Diamond

JF-Expert Member
Joined
Jun 9, 2023
Posts
593
Reaction score
1,376
Salam Wakuu,

Kama kawaida msemaji kujiteua kwenye masuala ya maji Mbezi Beach nimekuja na update.

Kwa majibu tuliyopewa na Meneja wa DAWASA Kawe inaonekana kuna mgao. Maana maji yanazuiliwa kwa baadhi ya masaa ili wengine wapate jambo linalofanya baadhi ya maeneo kupata maji kwa presha ndogo sana na wengine ndio tunakosa kabisa. Wizara ya Maji

Kwa maneno haya ni dhahiri kuwa kuna mgao. Waziri Wizara ya Maji toka hadharani utuambie nini kinaendelea, hayo maji unayosema yapo hatuyaoni, na hizo bilioni unazotaja kila siku zinatumika kuboresha miondombinu na matengenezo ya mara kwa mara hatuoni matunda yake.

Wakuu huko mliko hali ikoje? Wekeni hapa na kuwatag Wizara ya Maji wapate notifications za kutosha watupe majibu ya kueleweka.

Hii hapa convo kutoka group la DAWASA Mbezi Beach, hii ilikuwa jana, mtaani kwetu maji yalirejea kwa masaa kadhaa tukarudi kule kule, yamekatwa jana ile ile mpaka sasa naweka uzi huu hayajarudi.

Screenshot_20241117_102705_WhatsApp.jpg
Screenshot_20241117_102722_WhatsApp.jpg
HILI JIBU LA MENEJA HAPA CHINI NI KWAMBA AMETUAMBIA TUPO KWENYE MGAO!
Screenshot_20241117_102741_WhatsApp.jpg

Kwamba ni miezi hii miwili hapa ndio matumizi yamekuwa makubwa ila kabla yalikua hayatumiki sana wakati wa asubuhi? Tumechoka majibu yenu ya kisiasa.
Screenshot_20241117_102825_WhatsApp.jpg
Screenshot_20241117_102851_WhatsApp.jpg

Screenshot_20241117_131617_WhatsApp.jpg


Maji yalijaa mpaka yanamwagika sasa mgao huu umetoka wapi? Wizara ya Maji

====

Majibu ya wadau kuhusu maeneo mengine

Mkuu hiyo sio huko kwenu tu hata Sinza hali ni hiyo hiyo.

Ikishafika tu saa 3 usiku wanakata hadi 6 usiku ndo wanarudisha.

Yaani mtu umetoka kwenye mizunguko yako unataka utulie na familia maji hamna na tangazo hawatoi.

Wizara ya Maji naomba uliangalie hili
 
CCM hata wakae miaka 100 zaidi mgao utakua palepale.
 
Tatizo la Maji linasolviwa kwa njia mbili tu:

1. Kuongeza vyanzo
2. Kucontrol matumizi

DAWASA wenyewe wanatumia njia yao ya tatu.

3. Siasa
 
Mkuu hiyo sio huko kwenu tu hata Sinza hali ni hiyo hiyo.

Ikishafika tu saa 3 usiku wanakata hadi 6 usiku ndo wanarudisha.

Yaani mtu umetoka kwenye mizunguko yako unataka utulie na familia maji hamna na tangazo hawatoi.

Wizara ya Maji naomba uliangalie hili
 
Sahivi ukipata maji jaza hadi vijiko, usitumue kwa majigambo.
 
Huku kimara mwisho maji hayajatoka toka juzii(ijumaa),
Yaani kwa sasa hyapiti masaa 24, maji yanakuwa yamekatika.
Na hakuna taarifa yoyote.
 
Wewe ukiona hayatoki full time jua ni mgao tayari, hivi na hilo ni la kuuliza? Punguza deko.
 
Back
Top Bottom