Je, haya ndiyo yanaweza kuwa maswali magumu na majibu mepesi?

Je, haya ndiyo yanaweza kuwa maswali magumu na majibu mepesi?

Walker Water

JF-Expert Member
Joined
Aug 23, 2022
Posts
842
Reaction score
3,357
Leo naomba tuangalie na kujiuliza na kujijibu baadhi ya maswali yanayoonekana kuwatatiza watu wengi.

1. Mimi ni nani?; Mimi ni nafsi, mwili na roho.

2. Nimetoka wapi?; Nimetoka kwa Mungu Mkuu.

3. Amenileta kufanya nini hapa duniani?; Kufanya kazi yake ya kipekee ambayo hakuna mwingine ataweza kuifanya hapa duniani.

4. Nitaijuaje hiyo kazi?; Nitamuuliza yeye aliyenileta.

5. Nitamuulizaje?; Natafuta sehemu tulivu ya peke yangu na yeye nikiwa na kalamu na daftari kisha namwambia rohoni kuwa ninakikao na wewe na ninaomba unijibu haya maswali yangu, hakika ananijibu.

6. Kwa mimi nisiyeamini habari za Mungu na shetani nafanikiwaje?; Nimeumbwa kamili, hivyo najiwekea malengo yangu na ninatumia hekima yangu ya kibinadamu na nguvu zangu na ninafanikiwa kama nilivyopanga. Niwe mwaminifu tu.

7. Kwa nini Mungu asimuue shetani kabisa ili niishi kwa raha?; Hiyo kazi yote ameniachia mimi, yeye ananipa tu nguvu, hivyo mimi ndiye mwamuzi wa mwisho wa nini nimfanye shetani ( nikimwonea huruma sawa!).

8. Kwa nini Mungu aniumbe bila makubaliano yangu; Hapana, aliponiumba aliniuliza kwanza nikutume duniani ukafanye hichi na hichi, nikakubali mwenyewe, nikatolewa ufahamu nikazaliwa duniani na siku nazaliwa Mungu nilimwona akinipokea na siku ya kufa pia nitamwona dakika za mwisho ndipo nife. ( Sitapona nikishamwona ili nisije nikasimulia anafananaje).

9. Kwa nini nikifanya dhambi atanichoma pamoja na shetani?; Kwa sababu nimeumbwa kamili na nilivyofika duniani nikaacha kufanya kilichonileta nikaungana na shetani na kupendana naye na nimpaka nikiri mwenyewe kuwa nipo tayari kuchomwa naye na Mungu yeye ndiye mwonevu na hana haki.

10. Nifanyeje nitekeleze mambo yangu hapa duniani ili niishi kwa raha na kufa?; Nachagua kutekeleza mipango ya Mungu au yangu binafsi au ya shetani,yoyote kwa bidii. Mungu na shetani mipango yao ili ifanikiwe hapa duniani lazima wamtumie binadamu kwa sababu ana mwili. Mimi na vyote na hivyo naweza kutekeleza ya kati yao au yangu binafsi.

Karibuni wadau kwa maswali mengine, maswali na majibu au kuuliza swali na jibu lenye utata kati ya haya niliyo yaorodhesha
 
Leo naomba tuangalie na kujiuliza na kujijibu baadhi ya maswali yanayoonekana kuwatatiza watu wengi.

1. Mimi ni nani?; Mimi ni nafsi, mwili na roho.

2. Nimetoka wapi?; Nimetoka kwa Mungu Mkuu.

3. Amenileta kufanya nini hapa duniani?; Kufanya kazi yake ya kipekee ambayo hakuna mwingine ataweza kuifanya hapa duniani.

4. Nitaijuaje hiyo kazi?; Nitamuuliza yeye aliyenileta.

5. Nitamuulizaje?; Natafuta sehemu tulivu ya peke yangu na yeye nikiwa na kalamu na daftari kisha namwambia rohoni kuwa ninakikao na wewe na ninaomba unijibu haya maswali yangu, hakika ananijibu.

6. Kwa mimi nisiyeamini habari za Mungu na shetani nafanikiwaje?; Nimeumbwa kamili, hivyo najiwekea malengo yangu na ninatumia hekima yangu ya kibinadamu na nguvu zangu na ninafanikiwa kama nilivyopanga. Niwe mwaminifu tu.

7. Kwa nini Mungu asimuue shetani kabisa ili niishi kwa raha?; Hiyo kazi yote ameniachia mimi, yeye ananipa tu nguvu, hivyo mimi ndiye mwamuzi wa mwisho wa nini nimfanye shetani ( nikimwonea huruma sawa!).

8. Kwa nini Mungu aniumbe bila makubaliano yangu; Hapana, aliponiumba aliniuliza kwanza nikutume duniani ukafanye hichi na hichi, nikakubali mwenyewe, nikatolewa ufahamu nikazaliwa duniani na siku nazaliwa Mungu nilimwona akinipokea na siku ya kufa pia nitamwona dakika za mwisho ndipo nife. ( Sitapona nikishamwona ili nisije nikasimulia anafananaje).

9. Kwa nini nikifanya dhambi atanichoma pamoja na shetani?; Kwa sababu nimeumbwa kamili na nilivyofika duniani nikaacha kufanya kilichonileta nikaungana na shetani na kupendana naye na nimpaka nikiri mwenyewe kuwa nipo tayari kuchomwa naye na Mungu yeye ndiye mwonevu na hana haki.

10. Nifanyeje nitekeleze mambo yangu hapa duniani ili niishi kwa raha na kufa?; Nachagua kutekeleza mipango ya Mungu au yangu binafsi au ya shetani,yoyote kwa bidii. Mungu na shetani mipango yao ili ifanikiwe hapa duniani lazima wamtumie binadamu kwa sababu ana mwili. Mimi na vyote na hivyo naweza kutekeleza ya kati yao au yangu binafsi.

Karibuni wadau kwa maswali mengine, maswali na majibu au kuuliza swali na jibu lenye utata kati ya haya niliyo yaorodhesha
Ndio huu upupu wa teolojia eti zile mbuzi askofu zikisoma wanaitwa ni wasomi
 
Haujasoma vizuri,rejea swali namba sita.
Unathibitishaje hizo habari za uwepo wa Mungu ni kweli?

Au unafosi kwamba habari za uwepo wa Mungu ni ukweli ila huna uthibitisho?

Thibitisha kwanza huyo Mungu na shetani wapo.

Vinginevyo unafanya, Logical non sequitur.

Unaleta dhana ya kufikirika na kuiita mungu na kusema kwamba ndio iliumba binadamu na dunia, ilhali huna uthibitisho wa ukisemacho na wala huna uthibitisho wa uwepo wa huyo mungu.
 
Kwanza eleza ulijuaje na unathibitishaje Mungu na shetani wapo?
Law of physics. In every action there is equal and opposite reaction.
Kama mtu anaamini Mungu anatenda mema basi lazima shetani mtenda mabaya atakuwepo.

Kuna wanao amini shetani amewapa mafanikio sio ajabu wakiamini Mungu ndio adui wao.
 
Unathibitishaje hizo habari za uwepo wa Mungu ni kweli?

Au unafosi kwamba habari za uwepo wa Mungu ni ukweli ila huna uthibitisho?

Thibitisha kwanza huyo Mungu na shetani wapo.

Vinginevyo unafanya, Logical non sequitur.

Unaleta dhana ya kufikirika na kuiita mungu na kusema kwamba ndio iliumba binadamu na dunia, ilhali huna uthibitisho wa ukisemacho na wala huna uthibitisho wa uwepo wa huyo mungu.
Mungu wangu amekataa kujithibitisha kwako. Ushauri wangu kaa kimya tu au fanya lolote unaloweza na majibu utakayopata utakuja hapa kushuhudia wengine.
 
Law of physics. In every action there is equal and opposite reaction.
Kama mtu anaamini Mungu anatenda mema basi lazima shetani mtenda mabaya atakuwepo.

Kuna wanao amini shetani amewapa mafanikio sio ajabu wakiamini Mungu ndio adui wao.
Nawajua vizuri hawa.
 
Mungu wangu amekataa kujithibitisha kwako. Ushauri wangu kaa kimya tu au fanya lolote unaloweza na majibu utakayopata utakuja hapa kushuhudia wengine.
Huyo Mungu wako kama yupo basi ni Mdhaifu sana ndio maana Kashindwa kuja hapa kujidhihirisha mwenyewe.

Unahangaika sana kumuongelea huyo Mungu kwa vile Hayupo kujiongelea mwenyewe.

Mungu hajawahi kuwepo, hayupo na hata uwezekano wa kuwepo kwake Haupo.
 
Law of physics. In every action there is equal and opposite reaction.
Kama mtu anaamini Mungu anatenda mema basi lazima shetani mtenda mabaya atakuwepo.

Kuna wanao amini shetani amewapa mafanikio sio ajabu wakiamini Mungu ndio adui wao.
Logical non sequitur.

Unachanganya sayansi na imani kuunda hitimisho potofu lenye Contradiction.
 
Law of physics. In every action there is equal and opposite reaction.
Kama mtu anaamini Mungu anatenda mema basi lazima shetani mtenda mabaya atakuwepo.

Kuna wanao amini shetani amewapa mafanikio sio ajabu wakiamini Mungu ndio adui wao.
Naomba kujua chanzo cha shetani,iblisi n.k

Yaani nini ajili ya uwepo wa kiumbe hicho??
 
Hivi ni kwann Sisi binadamu tunajiona viumbe Wa ajabu hadi kufikiri tuna mahali tunakwenda baada ya kufa na siyo Wanyama wengine km Sokwe, Ng'ombe, Kuku nk? Tunachowazidi wanyama wengine(mana na Sisi binadamu ni wanyama pia) ni uwezo mkubwa wa ubongo tulio nao. Hivi ni ubongo huu ndio unatupeleka huko mnakoita mbinguni au ni sura zetu? Mana kama ni uwezo mkubwa bongo zetu wapo binadamu wanaozaliwa na ubongo wenye uwezo mdogo(IQ) km wa Mbwa(wenye mtindio Wa ubongo), Je, nao wakifa watakwenda kunakosemwa ni Mbinguni? Kama nao watakwenda kwann Wanyama wengine nao wasiende huko baada ya kufa? Hakuna Mbingu Wala Moto. Ni fikra tu za watu Wa Dini.
Kwamba Mungu alimuumba Malaika ambaye baadaye akamuasi. Inavyoelezwa ni km vile Mungu ni mzazi tu anayezaa mtoto bila kujua baadaye atakuwa na tabia ganu. Hapo hapo Mungu anapewa Sifa zote kuwa anajua mwisho kabla ya mwanzo, kwa sifa hizo alitakiwa kujua kuwa huyo Malaika atamuasi kabla hajamuumba. Vinginevyo hana hizo sifa. Kama alijua na akamuumba tu anyway, kosa ni la nani? Kama huyo Malaika, ambaye sasa anajulikana km Shetani akimdanganya mtu, km wanavyosema, na mtu akadanganyika, wakati Mungu alishajua wewe utadanganyika tu mana anajua mwanzo kabla ya mwisho, hiyo adhabu ni ya nn?
Kwenye vitabu vya hizi Dini kuu wanasema Adam aliumbwa na kuwekwa katika Bustan na kuonyeshwa miti yenye matunda atakayokula, lakini akakatazwa Kula matunda ya Mti mmoja tu wa Kati Kati ya Bustani. Halafu akaumbiwa Mke aitwaye Hawa au Eva. Halafu Shetani akaja akamdanganya ale matunda ya ule Mti. Mungu akakasirika akawafukuza na kuwalaani. Sasa laana za nn kama alijua mwisho kabla ya mwanzo. Maana yake alijua Adam atakula tunda na atawafukuza kabla hata hajamuumba. Vinginevyo, ili lawama zake ziwe halali, aondolewe hizo sifa. Abaki tu km Muumba asiyejua yatakayompata kiumbe chake baadaye. Hapo laana zake na lawama kwa Adam vinakuwa halali.
Haya Mambo kwenye hivi vitabu ni hekaya tu kama za Sindbad kwenye Alfu Lela ulela.
Nmefuatilia sana haya yanayoelezwa kwenye hivi vitabu vya hizi Dini zetu kuu. Nmepata ufahamu mkubwa sana kuwa hivi vitabu viliandikwa na watu wajanja Fulani wakitaka kutoa majibu ya maswali magumu yaliyokuwepo wakati huo kwa kuyatengenezea majibu yasiyo na ukweli wowote. Walifikiri hakutakuwa na maarifa Zaidi ya kujua Mambo tofauti na wakati wao.
Kwa Waislaam wanaambiwa, wakati Wa mfungo Wa mwezi Wa Ramadhan, jua linapotaka kutoka, wafunge na jua linapozama wafungue. Hii ni kwa sababu mtunzi Wa hicho kitabu alikuwa anaishi maeneo ya Karibu na Tropiki hivyo saa 12 ilikuwa inapatikana bila shida. Mfungo huo Wa kutoka na kuzama kwa jua hauwezekani kwa Nchi za juu kabisa za Dunia ambapo Kuna majira ambayo jua halionekani kabisa kwa Zaidi ya wiki na Kuna majira ambayo ucku hakuna kabisa. Mtunzi Wa hicho kitabu anadai alipewa maagizo hayo na Mungu aliyeumba Dunia. Km ni kweli, huyo Mungu hakujua majira ya Dunia aliyoiumba? Ni dhahiri haya yalikuwa maagizo ya mtunga kitabu au mtoa wahay na siyo Mungu kwani hakuwa ametembelea maeneo hayo ya Dunia hivyo hakujua chochote juu ya tofauti za majira Kati ya eneo analoishi na Maeneo mengine ya Dunia.
Tukaambiwa wafu Wa hiyo Imani ya kiislaam, wanapofika kaburini tu ni vipigo kwa kwenda mbele. Unaambiwa kichwa kinapigwa rungu hadi kinatawanyika na kujikusanya tena na kinapigwa tena na tena. Adhabu humo haisemeki, yaan mtu unakuwa nyaka nyaka. Lkn ukifukua kaburi la muislaam, labda kwa ajili ya postmoterm, kwa waliokufa kwa utata, huwez kuwakuta na hayo majeraha. Ss kinachopigwa n nn, ni hiyo roho km wanavyosema? Je, roho ina kichwa au kiwiliwili?
Mambo ni mengi ndugu zangu. Tafuta mwenyewe maarifa utajiuliza maswali mengi sana katika hizi Imani.
 
Hivi ni kwann Sisi binadamu tunajiona viumbe Wa ajabu hadi kufikiri tuna mahali tunakwenda baada ya kufa na siyo Wanyama wengine km Sokwe, Ng'ombe, Kuku nk? Tunachowazidi wanyama wengine(mana na Sisi binadamu ni wanyama pia) ni uwezo mkubwa wa ubongo tulio nao. Hivi ni ubongo huu ndio unatupeleka huko mnakoita mbinguni au ni sura zetu? Mana kama ni uwezo mkubwa bongo zetu wapo binadamu wanaozaliwa na ubongo wenye uwezo mdogo(IQ) km wa Mbwa(wenye mtindio Wa ubongo), Je, nao wakifa watakwenda kunakosemwa ni Mbinguni? Kama nao watakwenda kwann Wanyama wengine nao wasiende huko baada ya kufa? Hakuna Mbingu Wala Moto. Ni fikra tu za watu Wa Dini.
Kwamba Mungu alimuumba Malaika ambaye baadaye akamuasi. Inavyoelezwa ni km vile Mungu ni mzazi tu anayezaa mtoto bila kujua baadaye atakuwa na tabia ganu. Hapo hapo Mungu anapewa Sifa zote kuwa anajua mwisho kabla ya mwanzo, kwa sifa hizo alitakiwa kujua kuwa huyo Malaika atamuasi kabla hajamuumba. Vinginevyo hana hizo sifa. Kama alijua na akamuumba tu anyway, kosa ni la nani? Kama huyo Malaika, ambaye sasa anajulikana km Shetani akimdanganya mtu, km wanavyosema, na mtu akadanganyika, wakati Mungu alishajua wewe utadanganyika tu mana anajua mwanzo kabla ya mwisho, hiyo adhabu ni ya nn?
Kwenye vitabu vya hizi Dini kuu wanasema Adam aliumbwa na kuwekwa katika Bustan na kuonyeshwa miti yenye matunda atakayokula, lakini akakatazwa Kula matunda ya Mti mmoja tu wa Kati Kati ya Bustani. Halafu akaumbiwa Mke aitwaye Hawa au Eva. Halafu Shetani akaja akamdanganya ale matunda ya ule Mti. Mungu akakasirika akawafukuza na kuwalaani. Sasa laana za nn kama alijua mwisho kabla ya mwanzo. Maana yake alijua Adam atakula tunda na atawafukuza kabla hata hajamuumba. Vinginevyo, ili lawama zake ziwe halali, aondolewe hizo sifa. Abaki tu km Muumba asiyejua yatakayompata kiumbe chake baadaye. Hapo laana zake na lawama kwa Adam vinakuwa halali.
Haya Mambo kwenye hivi vitabu ni hekaya tu kama za Sindbad kwenye Alfu Lela ulela.
Nmefuatilia sana haya yanayoelezwa kwenye hivi vitabu vya hizi Dini zetu kuu. Nmepata ufahamu mkubwa sana kuwa hivi vitabu viliandikwa na watu wajanja Fulani wakitaka kutoa majibu ya maswali magumu yaliyokuwepo wakati huo kwa kuyatengenezea majibu yasiyo na ukweli wowote. Walifikiri hakutakuwa na maarifa Zaidi ya kujua Mambo tofauti na wakati wao.

takribani waandishi 40 mbalimbali wa binadamu walichangia kuandika Biblia, ambayo iliandikwa katika kipindi cha miaka 1500. Waandishi walikuwa wafalme, wavuvi, makuhani, viongozi wa serikali, wakulima, wachungaji, na madaktari. Kutoka tofauti hii yote inakuwa umoja wa ajabu, na ndhamira moja kuunganishwa pamoja.

Umoja wa Biblia ni kutokana na ukweli kwamba, hatimaye, ina Mwandishi mmoja - Mungu mwenyewe. Biblia ni "pumzi ya Mungu" (2 Timotheo 3:16). Waandishi wanadamu waliandika kile hasa Mungu alitaka waandike, na matokeo yake ilikuwa kamilifu na takatifu ya neno la Mungu (Zaburi 12:6, 2 Petro 1:21).
Kwa Waislaam wanaambiwa, wakati Wa mfungo Wa mwezi Wa Ramadhan, jua linapotaka kutoka, wafunge na jua linapozama wafungue. Hii ni kwa sababu mtunzi Wa hicho kitabu alikuwa anaishi maeneo ya Karibu na Tropiki hivyo saa 12 ilikuwa inapatikana bila shida. Mfungo huo Wa kutoka na kuzama kwa jua hauwezekani kwa Nchi za juu kabisa za Dunia ambapo Kuna majira ambayo jua halionekani kabisa kwa Zaidi ya wiki na Kuna majira ambayo ucku hakuna kabisa. Mtunzi Wa hicho kitabu anadai alipewa maagizo hayo na Mungu aliyeumba Dunia. Km ni kweli, huyo Mungu hakujua majira ya Dunia aliyoiumba? Ni dhahiri haya yalikuwa maagizo ya mtunga kitabu au mtoa wahay na siyo Mungu kwani hakuwa ametembelea maeneo hayo ya Dunia hivyo hakujua chochote juu ya tofauti za majira Kati ya eneo analoishi na Maeneo mengine ya Dunia.
Tukaambiwa wafu Wa hiyo Imani ya kiislaam, wanapofika kaburini tu ni vipigo kwa kwenda mbele. Unaambiwa kichwa kinapigwa rungu hadi kinatawanyika na kujikusanya tena na kinapigwa tena na tena. Adhabu humo haisemeki, yaan mtu unakuwa nyaka nyaka. Lkn ukifukua kaburi la muislaam, labda kwa ajili ya postmoterm, kwa waliokufa kwa utata, huwez kuwakuta na hayo majeraha. Ss kinachopigwa n nn, ni hiyo roho km wanavyosema? Je, roho ina kichwa au kiwiliwili?
Mambo ni mengi ndugu zangu. Tafuta mwenyewe maarifa utajiuliza maswali mengi sana katika hizi Imani.
 
Back
Top Bottom