Je, hii ndiyo sababu ya mtoto kufanana sura na mzazi wake?

Je, hii ndiyo sababu ya mtoto kufanana sura na mzazi wake?

Ubumuntu

JF-Expert Member
Joined
Oct 21, 2010
Posts
14,345
Reaction score
10,885
Salaam,

Wakati mamsapu alipokuwa mjamzito, nilikuwa nikienda nae kliniki mara kwa mara. Sasa siku moja, katika mazungumzo, nikamsikia dada mmoja aliyekuwa ana mtoto mchanga hapo kliniki, akisema daktari wake alimwambia sababu ya mtoto kufanana sura na wazazi wake.

Alisema kwamba, daktari alimwambia kwamba: mtoto anapofanana sura na baba, ina maana wakati wa tendo la ndoa (na muendelezo wa mbegu ya kiume kukutana na ya kike), mama aliridhika, kwamba, mama alifurahia tendo na kuridhika kabisa. Na pale mtoto anapofanana na mama ina maana mama hakuridhika kabisa, kwamba, baba alimwacha mama njiani.

Nilibaki na butwaa!! Dah! Ikabidi niwe nasubiria kwa hamu kufahamu mtoto wetu atafanana na nani. Ile kuzaliwa tu, kulalaleki, kidume kikawa kinafanana na mimi kama copy and paste!

Sasa, ninaandika haya, ili kuweza kupata ujuzi wa JF Doctors.
Hili suala la ukweli wa kisayansi ama yule daktari alimchengua tu yule dada?

Maana najiuliza, iwapo mtoto anafanana na wazazi wote, hapo inakuaje?

Wasalaam.
 
Salaam,

Wakati mamsapu alipokuwa mjamzito, nilikuwa nikienda nae kliniki mara kwa mara. Sasa siku moja, katika mazungumzo, nikamsikia dada mmoja aliyekuwa ana mtoto mchanga hapo kliniki, akisema daktari wake alimwambia sababu ya mtoto kufanana sura na wazazi wake.

Alisema kwamba, daktari alimwambia kwamba: mtoto anapofanana sura na baba, ina maana wakati wa tendo la ndoa (na muendelezo wa mbegu ya kiume kukutana na ya kike), mama aliridhika, kwamba, mama alifurahia tendo na kuridhika kabisa. Na pale mtoto anapofanana na mama ina maana mama hakuridhika kabisa, kwamba, baba alimwacha mama njiani.

Nilibaki na butwaa!! Dah! Ikabidi niwe nasubiria kwa hamu kufahamu mtoto wetu atafanana na nani. Ile kuzaliwa tu, kulalaleki, kidume kikawa kinafanana na mimi kama copy and paste!

Sasa, ninaandika haya, ili kuweza kupata ujuzi wa JF Doctors.
Hili suala la ukweli wa kisayansi ama yule daktari alimchengua tu yule dada?

Maana najiuliza, iwapo mtoto anafanana na wazazi wote, hapo inakuaje?

Wasalaam.

Wote baba na mama walifurahia mechi!!
 
Wote baba na mama walifurahia mechi!!

Baba siku zote uridhika kutokana na biolojia yake.

Kwa mujibu wa maelezo wa huyo daktari (kupitia yule dada), mwanamke ndiye kiashiria. Akifurahia, mtoto ufanana na baba. Hasipofurahia, basi mtoto atafanana naye.
 
Baba siku zote uridhika kutokana na biolojia yake.

Kwa mujibu wa maelezo wa huyo daktari (kupitia yule dada), mwanamke ndiye kiashiria. Akifurahia, mtoto ufanana na baba. Hasipofurahia, basi mtoto atafanana naye.

Haya bana! Mama kazaa mtoto anafanana na njemba jirani, minong'ono ilipoanza mama kadai mtoto kafanana na jirani kwa vile kipindi cha ujauzito wake alikuwa anamchukia sana huyo jirani yao!!!
 
Haya bana! Mama kazaa mtoto anafanana na njemba jirani, minong'ono ilipoanza mama kadai mtoto kafanana na jirani kwa vile kipindi cha ujauzito wake alikuwa anamchukia sana huyo jirani yao!!!

Duh! Hii mbona haipo kisayansi kabisa?!?

Hili naona JF doctors wanakimbia kutoa maelezeo yao ya kitaalamu.

Riwa ZeMarcopolo Mr Kiroboto drphone na wengineo majibu tafadhali.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu, hakuna uwiano wa kisayansi hapo!.....Hizo ni ngano za kufurahisha baraza tu!
 
Mkuu, hakuna uwiano wa kisayansi hapo!.....Hizo ni ngano za kufurahisha baraza tu!

Oh! Hujajibu swali la msingi lililomo ndani ya swali hili. Ni zipi sababu za mtoto kufanana sura na mzazi wake?
 
Oh! Hujajibu swali la msingi lililomo ndani ya swali hili. Ni zipi sababu za mtoto kufanana sura na mzazi wake?

Rejea maelezo yako mkuu baada ya kichwa cha habari!....nimejibu kulingana na maelezo yako ya msingi!

Sababu ya mtoto kufanana sura na na wazazi wake ni VINASABA. Nikipata wasaa mzuri nitakuja na nondo za kutosha hapa kutoa lecture kuhusu vinasaba kwa faida ya wana jamvi.
 
Rejea maelezo yako mkuu baada ya kichwa cha habari!....nimejibu kulingana na maelezo yako ya msingi!

Sababu ya mtoto kufanana sura na na wazazi wake ni VINASABA. Nikipata wasaa mzuri nitakuja na nondo za kutosha hapa kutoa lecture kuhusu vinasaba kwa faida ya wana jamvi.

Shukrani chifu. Nasubiria lecture.
 
Nzi, mtoto anaundwa na mbegu ya baba na mama ambazo zibabeba pair moja ya vinasaba. Vinasaba hivi ni printout ya jinsi mtoto atakavyokuwa kutokana na muungano wa pairs. Sasa katika kila moja kwenye pair hii kuna vitu 23 kila upande na kila kimoja kina nguvu tofauti. Na hivyo ndo vimemfanya obama asiwe shombeshombe kama wengine kwa sababu kinasaba husika cha baba kimekuwa strong kuliko mama.

Kimtaani tunasema ana damu kali, haidanganyi. Maskio, pua, macho, nywele etx zitaonekana kwenye kinasaba kilicho strong zaidi. Ndio maana zeru zeru anaweza kuzaa mtoto wa kawaida endapo anazaa na mtu asie na hata dalili iliyojificha ya uzeruzeru(japo kuna exception ambayo nikikupa nitakuchanganya zaidi)

kama issue ni kuridhishwa kwa mama mbona dunia ingekuwa ya ajabu? Wanawake wachache sana wanaridhishwa kingono aisee, truth be told!

Kama hujaelewa nialike nije kunywa mtori wa mzazi niwaeleweshe kwa kituo.
 
Nzi, mtoto anaundwa na mbegu ya baba na mama ambazo zibabeba pair moja ya vinasaba. Vinasaba hivi ni printout ya jinsi mtoto atakavyokuwa kutokana na muungano wa pairs. Sasa katika kila moja kwenye pair hii kuna vitu 23 kila upande na kila kimoja kina nguvu tofauti. Na hivyo ndo vimemfanya obama asiwe shombeshombe kama wengine kwa sababu kinasaba husika cha baba kimekuwa strong kuliko mama.

Asante sana.
Kumbe vinasaba ndiyo mwamuzi. Vinasaba siyo ndiyo genes kwa kiinglishi? Nilisoma mahali, eti inasemekana kwamba kwa mwanadamu kukua katika hali kamili anahitaji vinasaba 100,000 kutoka kwenye seli 1!!
Kwa muktadha huo, ina maana kwa mtoto kufanana na wazazi wote, itabidi mtoto achukue nusu ya vinasaba kutoka kwa kila mzazi? Na ili afanane na baba completely ina maana vinasaba hivyo vyote vitatoka kwa baba? Na ili afanane na mama, nayo itakuwa kama akifanana na baba?

Ndio maana zeru zeru anaweza kuzaa mtoto wa kawaida endapo anazaa na mtu asie na hata dalili iliyojificha ya uzeruzeru(japo kuna exception ambayo nikikupa nitakuchanganya zaidi)

Hadi hapa, ulishanichanganya kuhusu zeruzeru. Kwa nilivyoelewa, zeruzeru anaweza hata kuzaa na zeruzeru mwenzake na wakapata mtoto hasiye zeruzeru. Ama sivyo? Ni sawa tu na watu wawili wasio zeruzeru wanapoweza kuzaa mtoto zeruzeru. Sijui wataalamu wanasema hili ni heritable.

kama issue ni kuridhishwa kwa mama mbona dunia ingekuwa ya ajabu? Wanawake wachache sana wanaridhishwa kingono aisee, truth be told!

Aisee!!! Kutoka kwenye uzoefu ama utafiti? Sasa wanawake mmechukua hatua zipi ili muondoe dukuduku lenu katika kupata suluhisho la tatizo hilo.

Kama hujaelewa nialike nije kunywa mtori wa mzazi niwaeleweshe kwa kituo.

Asante.
Lakini, mh! Wewe na bunduki yako utamtisha baby.
 
Ninachokifaham hapa Sura ya Mtoto inatengenezwa Wakati wa Mama Mjamzito kulea Mimba Mama anapitia nyakati Gani ikiwa utamuacha peke Yake ukamtenga angalia atakaekuwa nae karibu akimfariji na kumtia moyo Hapa huenda Rafiki yako au ndugu Yako ambae atakua anaongea nae vizuri hapo ndipo sura ya mtoto inatengenezwa kumbuka Sura ya Mtoto inapatikana kutoka kwenye Ubongo wa Mbele Sasa kwenye Ubongo wa Mbele ukute uyo mama anamuaza huyu alie msaada wake Wewe utakumbukwa lini uwez kuumba kitu usichokijua
 
Mtoa mada,mpaka hii 2025 utakuwa umekua kiumri na kiakili,vp bado unaamini hili ulilo liandika?
 
Salaam,

Wakati mamsapu alipokuwa mjamzito, nilikuwa nikienda nae kliniki mara kwa mara. Sasa siku moja, katika mazungumzo, nikamsikia dada mmoja aliyekuwa ana mtoto mchanga hapo kliniki, akisema daktari wake alimwambia sababu ya mtoto kufanana sura na wazazi wake.

Alisema kwamba, daktari alimwambia kwamba: mtoto anapofanana sura na baba, ina maana wakati wa tendo la ndoa (na muendelezo wa mbegu ya kiume kukutana na ya kike), mama aliridhika, kwamba, mama alifurahia tendo na kuridhika kabisa. Na pale mtoto anapofanana na mama ina maana mama hakuridhika kabisa, kwamba, baba alimwacha mama njiani.

Nilibaki na butwaa!! Dah! Ikabidi niwe nasubiria kwa hamu kufahamu mtoto wetu atafanana na nani. Ile kuzaliwa tu, kulalaleki, kidume kikawa kinafanana na mimi kama copy and paste!

Sasa, ninaandika haya, ili kuweza kupata ujuzi wa JF Doctors.
Hili suala la ukweli wa kisayansi ama yule daktari alimchengua tu yule dada?

Maana najiuliza, iwapo mtoto anafanana na wazazi wote, hapo inakuaje?

Wasalaam.
Sayans ya hisia kal
 
Back
Top Bottom