Je, huu Utamaduni 'Unaoboa' huwa ni takwa la Kikatiba, la Kiserikali, la Kichama ( CCM ) au ni la Kujipendekeza tu?

Je, huu Utamaduni 'Unaoboa' huwa ni takwa la Kikatiba, la Kiserikali, la Kichama ( CCM ) au ni la Kujipendekeza tu?

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2013
Posts
60,660
Reaction score
121,325
Utamkuta Waziri, Mkuu wa Mkoa na Wilaya pamoja na Watendaji wengine kila wakiwa wanatolea Ufafanuzi wa Jambo fulani wakiwa Wanahojiwa na Waandishi wa Habari ni lazima tu Watalazimisha kumtaja Rais wa Nchi (mfano wa sasa Samia) na hata kwa Wengine waliotuongoza Watanzania huko nyuma.

Hivi kwani Sisi Watanzania hatujui kuwa Rais wa Tanzania ni Samia Suluhu Hassan?

Na mnavyomtaja kila mara mkizungumza hata maeneo ambayo hamtakiwi Kumtaja ili Kuokoa muda huwa mnataka Kutuaminisha nini labda?

Kama kawaida yangu GENTAMYCINE ya kupenda Kutafiti na Kudadisi Jambo / Tukio nimejaribu kufuatilia Watendaji wa nchi za Ulaya, Marekani, South Africa, Uganda, Rwanda na Kenya wakiwa Wanaongea na Kutolea Ufafanuzi fulani wa Kiutendaji katika Serikali zao na hakuna mahala nimewasikia wakiwataja Marais wao na wala hawachukiwi na hao Marais kwa kutofanya Kwao hivyo.

Nikija kuwa Rais wa Tanzania nikiwa namsikia Mtendaji yoyote kila akiwa anaongea ananisifia au ananitajataja nitamuita Ikulu na Kumuwamba (Kumzaba) Vibao kwani nitajua huo ni Unafiki na Kujikomba kunakopitiliza Kwangu ili labda nami Nilewe Sifa na nisiwaze Kuwatumbua pale nikigundua Wameharibu mahala.

I hope Message Sent and Delivered!
 
Kweli kabisa mkuu. Hata mm huwa najiuliza ni kwa nn.

Ila acha na mm nimshukuru raisi wangu nimeamka salama leo na nimeingia hapa jf na kazi zinaendelea
 
Upumbavu huu sasa umevuka mpaka katika taasisi nyingine ambazo si za kiserikali. Angalia kwenye Derby ya jana mabango ya picha ya Samia yalikuwa mengi kuliko ambavyo huwepo wakati wa mikutano ya CCM!
 
Utamkuta Waziri, Mkuu wa Mkoa na Wilaya pamoja na Watendaji wengine kila wakiwa wanatolea Ufafanuzi wa Jambo fulani wakiwa Wanahojiwa na Waandishi wa Habari ni lazima tu Watalazimisha kumtaja Rais wa Nchi ( mfano wa sasa Samia ) na hata kwa Wengine waliotuongoza Watanzania huko nyuma.

Hivi kwani Sisi Watanzania hatujui kuwa Rais wa Tanzania ni Samia Suluhu Hassan?

Na mnavyomtaja kila mara mkizungumza hata maeneo ambayo hamtakiwi Kumtaja ili Kuokoa muda huwa mnataka Kutuaminisha nini labda?

Kama kawaida yangu GENTAMYCINE ya kupenda Kutafiti na Kudadisi Jambo / Tukio nimejaribu kufuatilia Watendaji wa nchi za Ulaya, Marekani, South Africa, Uganda, Rwanda na Kenya wakiwa Wanaongea na Kutolea Ufafanuzi fulani wa Kiutendaji katika Serikali zao na hakuna mahala nimewasikia wakiwataja Marais wao na wala hawachukiwi na hao Marais kwa kutofanya Kwao hivyo.

Nikija kuwa Rais wa Tanzania nikiwa namsikia Mtendaji yoyote kila akiwa anaongea ananisifia au ananitajataja nitamuita Ikulu na Kumuwamba ( Kumzaba ) Vibao kwani nitajua huo ni Unafiki na Kujikomba kunakopitiliza Kwangu ili labda nami Nilewe Sifa na nisiwaze Kuwatumbua pale nikigundua Wameharibu mahala.

I hope Message Sent and Delivered!!
Kama Yeye anaye tajwa hasemi jamani nimeambiwa nawaletea pesa ila kiukweli pesa hizi ni jasho lenu wala sio mm naleta au sheria ina taka nilete pesa hizi. Sasa anaye tajwa hasemi na ndio anafurahi sasa sio kwamba ni katabia kakujikomba kwa Rais ambako ni kabaya sana.
 
Low IQ. Watanzania wengi sana hasa viongozi wana kiwango duni mno cha kufikiri sawa sawa.
Hata wewe una nafasi ya kuwa kiongozi ukiona unao uwezo wa kiuongozi waweza kugombea ,lakini usiwatukane na kututukana watanzania kiujumla jumla bila hoja, TUMEFIKA hapa tulipo kwa kuwa tulipata na tuna viongozi wenye uchungu na nchi hii Kama ilivyo kwa mama Samia ambaye unamuona akipambana kizalendo kuhakikisha kuwa walau kila Siku tunapunguza kiwango Cha umaskini katika Kaya zetu

Kila siku unamuona mh Rais akiwa yupo kazini kuwatumikia watanzania wanyonge, akiwa kazini kutoa majibu kwa maswali ,akiwa kazini kutoa matumaini kwa waliokata Tamaa,akiwa kazini kuleta nuru mahali penye Giza, akiwa kazini kuonyesha njia mahali ambapo watu wamepotea njia
 
Siku za karibuni kulikuwa na zuio la kutumia bidhaa za kitimoto cha kushangaza ni pale zuio linaondolewa halafu anae tangaza anazisifu juhudi za muheshimiwa mama kufanikisha hili😀
 
Back
Top Bottom