Mbwa dume
JF-Expert Member
- Jan 15, 2014
- 5,934
- 10,206
Habari zenu wandugu,
Ni muda mrefu nilikuwa kimya lakini yote ni katika harakati za utafutaji ukizingatia utawala huu hakuna tena zile dili za upigaji.
Niende kwenye mada,
Nina mdada ambaye niliwahi kuwa na mahusiano naye kipindi flani hivi then tukapotezana ikapelekea kila mtu kushika hamsini zake, kwani wazazi wake walihamia mkoa mwingine kikazi then polepole mawasiliano yakakatika.
Sasa tatizo ni kwamba mdada huyu alinijulisha kuwa kipindi naachana naye alikuwa na ujauzito japo hakujua, na hivi tunavyoongea tayari kajifungua mtoto wa kiume sasa hofu yangu inakuja hivi, nakumbuka tumeachana tarehe 16 January mwaka huu akiwa hana dalili za mimba.
Nakumbuka mara yake ya mwisho kuona damu ilikuwa December mwishoni na mpaka hiyo January tunaachana, nakumbuka kwenye tarehe 14 nilimpeleka hospital alikuwa akiumwa akapimwa vipimo vyote mpaka mimba hakuwa nayo isipokuwa walikuta tatizo la UTI ambapo alipewa dawa za kutumia na kufikia tarehe 16 January tukaagana akasafiri na wazazi wake na ndio ikawa mwisho kuonana kwetu zaidi ya mawasiliano kidogo kwa simu.
Mpaka hapa sina nia mbaya ya kumkataa mtoto ila hofu yangu ni kwamba, ikiwa mimba imeingia tarehe hizo alizoondoka yaani kati ya tarehe 15 na 16 January je inawezekana kweli ajifungue tarehe 5. Septemba?
Mbona ukihesabu miezi kuanzia ameondoka yaani tarehe 16.January mpaka tarehe 5. Septemba mbona miezi tisa haifiki? Ina maana huyu mtoto kazaliwa na miezi 8?na ikiwa ni hivyo je inawezekana mtoto kuzaliwa na miezi 8 akawa na hafya njema kama ilivyo kwa huyu?
Naamini humu jukwaani kuna wajuzi wa haya mambo pengine mimi sijui kuhesabu vizuri miezi.
Naomba kueleweshwa.
NB: Tarehe yake ya mwisho period =25/12/2016
Siku ya niliyompeleka hospital =14/01/2017 (vipimo vilionyesha hakuwa na mimba)
Siku aliyosafiri na ndio mwisho wetu kuonana 16/01/2017
Lakini amejifungua tarehe = 05/09/2017
Wadau naomba sana ushauri wenu kuhusu hesabu hizi maana mie naona miezi ya hiyo mimba haifiki 9!
Ni muda mrefu nilikuwa kimya lakini yote ni katika harakati za utafutaji ukizingatia utawala huu hakuna tena zile dili za upigaji.
Niende kwenye mada,
Nina mdada ambaye niliwahi kuwa na mahusiano naye kipindi flani hivi then tukapotezana ikapelekea kila mtu kushika hamsini zake, kwani wazazi wake walihamia mkoa mwingine kikazi then polepole mawasiliano yakakatika.
Sasa tatizo ni kwamba mdada huyu alinijulisha kuwa kipindi naachana naye alikuwa na ujauzito japo hakujua, na hivi tunavyoongea tayari kajifungua mtoto wa kiume sasa hofu yangu inakuja hivi, nakumbuka tumeachana tarehe 16 January mwaka huu akiwa hana dalili za mimba.
Nakumbuka mara yake ya mwisho kuona damu ilikuwa December mwishoni na mpaka hiyo January tunaachana, nakumbuka kwenye tarehe 14 nilimpeleka hospital alikuwa akiumwa akapimwa vipimo vyote mpaka mimba hakuwa nayo isipokuwa walikuta tatizo la UTI ambapo alipewa dawa za kutumia na kufikia tarehe 16 January tukaagana akasafiri na wazazi wake na ndio ikawa mwisho kuonana kwetu zaidi ya mawasiliano kidogo kwa simu.
Mpaka hapa sina nia mbaya ya kumkataa mtoto ila hofu yangu ni kwamba, ikiwa mimba imeingia tarehe hizo alizoondoka yaani kati ya tarehe 15 na 16 January je inawezekana kweli ajifungue tarehe 5. Septemba?
Mbona ukihesabu miezi kuanzia ameondoka yaani tarehe 16.January mpaka tarehe 5. Septemba mbona miezi tisa haifiki? Ina maana huyu mtoto kazaliwa na miezi 8?na ikiwa ni hivyo je inawezekana mtoto kuzaliwa na miezi 8 akawa na hafya njema kama ilivyo kwa huyu?
Naamini humu jukwaani kuna wajuzi wa haya mambo pengine mimi sijui kuhesabu vizuri miezi.
Naomba kueleweshwa.
NB: Tarehe yake ya mwisho period =25/12/2016
Siku ya niliyompeleka hospital =14/01/2017 (vipimo vilionyesha hakuwa na mimba)
Siku aliyosafiri na ndio mwisho wetu kuonana 16/01/2017
Lakini amejifungua tarehe = 05/09/2017
Wadau naomba sana ushauri wenu kuhusu hesabu hizi maana mie naona miezi ya hiyo mimba haifiki 9!