Je, ilikuwa na ulazima wa Simba kumsajili Niyonzima? Usajili usiokuwa na maana kabisa ni huu

py thon

JF-Expert Member
Joined
Sep 11, 2016
Posts
2,476
Reaction score
4,448
Katika usajili walioufanya Simba pasi na shaka usajili wa Niyonzima walikurupuka. Simba haikuwa na tatizo na kiungo na idara ambayo Simba ilikuwa vizuri mno basi ni idara ya kiungo ndio maana wakicheza na yanga au Azam tokea msimu uliopita walikuwa wakitawala sana mpira hata Yanga yenye Kamusoko na Niyonzima na simba iliyokuwa pungufu lakini simba iliyokuwa pungufu waliwapoteza yanga huku Ndemla, Mkude Mzamiru wakipasiana pasi kwa ustadi mkubwa

Niyonzima amekuwa akilaumiwa na mashabiki wa yanga kuwa amekuwa akicheza chini ya kiwango kila akikutana na Simba. Niyonzima sio alikuwa anapenda tatizo uwezo wa Mkude, Ndemla, Mzamiru na Mo katika uchezeshaji ulikuwa mkubwa

Je, kulikuwa na ulazima wa simba kumsajili Nio?

Niyonzima sio goal scoring midfielder sasa kama sio kiungo anayefunga basi atakuwa mzuri kwenye uchezeshaji. Swali: Je, Simba walikuwa na shida ya aina ya kiungo huyo?

Saizi Simba ina idadi kubwa ya viungo karibu 7, na wanaokuwa wanaanza msimu huu ni Kotey, Mzamiru na Niyonzima

Ndemla, Mkude, Mo wamekuwa wakisugua sana benchi.

Binafsi sijaona umuhimu wa Niyonzima ndani ya kikosi cha Simba, Ndemla na Mo walikuwa wakitekeleza ipasavyo na saizi wamekuwa wahanga.

Simba udhaifu wao ulikuwa ni eneo la ushambuliaji na ni sehemu iliyokuwa ikiinyima maksi Simba.

Ninamshauri Mkude dirisha dogo aondoke simba huyu jamaa ni mtaalamu sana ni nadra kumuona akipoteza pasi na ana akili, na pia Mo namshauri asepe zake aende Azam au hata Yanga wanashida na type yake.

Ndemla ni play maker mzuri na sio wa kukaa benchi kabisa namshauri atafute timu south Africa au Africa kaskazini aidha Etoil du sahel au Al ahl.

Kubaki simba watajipoteza na watabaki historia wakati ilibidi watambe nyakati hizi.
 
Unajua kwanini FIFA waliweka idadi ya wachezaji katika timu wawe 30 au 28 ilhali wanaocheza uwanjani ni 11?
Haya mambo si kuvamia vamia tu tafakari hilo kwanza ndo utapata jibu.
 
Kakwambia anataka kulogwa?
Kamati ya ufundi siyo timu ya walozi.
Ni jopo la wanataaluma wa mpira linaloshugulika na kuhakikisha wachezaji, makocha na wadau wa timu wanashirikiana kwa usahihi kuhakikisha timu inapata matokeo mazuri katika mechi zote.
Sio ushirikina.
 
Unajua kwanini FIFA waliweka idadi ya wachezaji katika timu wawe 30 au 28 ilhali wanaocheza uwanjani ni 11?
Haya mambo si kuvamia vamia tu tafakari hilo kwanza ndo utapata jibu.
Jaribu kufanya hesabu ndogo tu ndipo uchangie vinginevyo utakuwa unapost ujinga kila siku...nikupe hesabu ndogo tu 7×7 ngapi?
 
Inauma sana kuona vipaji vya wazawa kama Ndemla, Mkude na Mo vikipotea kwa sababu ya tamaa zisizo na maana!
 
Mkuu si unajua usajili wa bongo ni undavaundava..kukomoana na kutaka sifa tu?
 
[emoji28][emoji28][emoji28][emoji28] Soka la Tanzania bado haliwapi Wazawa nafasi kwa ajiri ya kuonekana zaidi .......

Tusilalamike na timu ya taifa tulalamike na clubs zetu.. unakuta timu imejaa wageni kwenye ile first 11 unawakuta wa 4 [emoji28][emoji28]

Hawa tunao waona wakuna Samatta na Msuva jitihada zao zimewafikisha pale walipo ila kiujumla muundao wa soka la Tanzania ni mbovu kuanzia chini hadi juu....

Tuwaache wakuna NIYONZIMA, OKWI,TAMBWE,NGOMA NA PAPI watese tulisha jiaminisha ya kuwa kwa wageni na sio wazawa
 
Haya ndio madhara ya kukomoana ktk soka la bongo.
 
Akili zinaanza kuwarudi sasa baada ya kuzuzuliwa na vuvuzela, kikosi cha bilioni 1.3 kinapoteza matumaini sasa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…