Je, inawezekana kuchaji battery za solar kwa umeme wa Tanesco?

Kwa nini ununue betri la solar ilhali huchaji kwa solar panel.

Ya solar mengi ni Chinese tu sokoni,fekifeki.
 
TANESCO mnafanya watu wanakua wabunifu, kuna mdau alibuni umeme wa biogas akapigwa pin anaeuliza nini shida anaambiwa anazalisha umeme bila kibari na hii ya mabetrii vipi mtawaambia wanazalisha umeme bila kibari au itakuaje?
 
Kwann unasema hiv mkuu ...
Ni mdogo sana tumia ujionee umeme wa biogas ndio mwingi Ila hatuna wataalamu wa umeme huo umejaa kwenye madampo yote makubwa nchini ukianza na Dampo la PUGU
 
Backup ya kuwasha taa 10 inaweza kuwa bei gani complete? Kuna jamaa akasema 2m, kweli?
 
Kuna kifaa kinaitwa inverter kinaweza kukusaidia. Kuna chenye mfumo wa hybrid na ambacho hakina.

Hybrid inverter ni gharama ila iko vizuri, kwanza ina njia ya umeme na solar. Pia kama tanesco watakata umeme wewe hautajua maana itabadilisha mfumo kutoka tanesco kuja kwenye mfumo wa solar kama kuna jua au kwenye beteri kama hakuna jua bila ya kukatika umeme.

Pili ina mfumo wa kulinda overload, overcharge, short na tahadhari nyinginyezo.

Ila hizo zingine bei ni ndogo na nyingi zina kelele wakati wa matumizi. Ila zinaoperate manually.
 
Battery ni Storage...,

Kwahio sababu hio battery yako ambayo inatunza DC (Direct Current) kutoka kwenye Solar ni sawa tu na Battery yako kwenye Simu ambayo inatunza Direct Current (ambayo imekuwa coverted na hio adapter yako kutoka umeme wa Grid / Tanesco ambao ni AC...

Kwa ufupi ndio unaweza ukatunza umeme wa grid (AC) kwenye battery ambayo inatunza DC kwa kutumia kifaa ambacho kina convert AC to DC
 
kwa hiyo kwa mfumo huu itahitajika both rectifier na inverter, Rectifier itumike kwenye kuchaji DC battery from AC power source then ili kutumia battery kwenye vifaa vyangu vya AC inabidi kuwe na inverter si ndio
 
kwa hiyo kwa mfumo huu itahitajika both rectifier na inverter, Rectifier itumike kwenye kuchaji DC battery from AC power source then ili kutumia battery kwenye vifaa vyangu vya AC inabidi kuwe na inverter si ndio
Naam utahitaji rectifier kubadilisha AC to DC ambayo ndio inaweza kutunzwa kwenye battery... Ila kumbuka hivi conversion unapoteza nishati...; Kwa ushauri kama ni Taa n.k. nunua Taa zinazotumia DC kama back-up umeme ukirudi utaendelea na vifaa vyako vingine....
 
Tv je unatumia dc?
 
Tv je unatumia dc?
Naam kuna TV za DC; ingawa TV nyingi zinachukua umeme wa AC (sababu ndio umeme kutoka kwenye GRID) ila umeme huu unakuwa converted to DC sababu componets nyingi kwe TV zinatumia DC; Kwa ufupi anaweza pia kununua TV ya DC
 
Mkuu inatumia muda gani kujaa

Mkuu huwa naweka chaji pindi umeme ukiwepo tu maana huku huwa unashinda jioni unakatika,ila inajaza kabisa mpaka 14.5V..wakat mwingine tunashinda bila umeme so huwa natumia jion umeme ukirudi nawasha inachajiwa had asubuhi,ni kitendo cha kuwasha switch tu
 
Nimepata Somo hapa kidogo mkuu,, hebu basi nikuulize.. Ninavyojua charger ya PC/Laptop huwa inachukuwa umeme from AC to DC kupeleka kwenye bettery ya laptop, Je, ninaweza kutumia hii Adopter ya PC kuchaji Betri yangu ya N100 na ikaweza kujaza bettery hiyo na nitajuaje kama Bettery imekaa full..?

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…