Pre GE2025 Je, jeshi la Polisi litatekeleza maelekezo ya Dkt. Nchimbi ya kuwaachia viongozi wa CHADEMA? Haiwezekani akawa yeye pia ana mamlaka ya kusema kamata?

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Resilience

JF-Expert Member
Joined
Jan 4, 2023
Posts
1,096
Reaction score
4,948
Kama Karibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi anaweza akaelekeza waliokamatwa waachiwe na Vyombo vikatii, upo uwezekano huyu ndiye aliyeagiza wakamatwe.

Tukumbuke Juzi alimtaka Lissu ajiunge CCM then Lissu akamjibu shit, yawezekana kabisa mzee Nchimbi alichukia akaamua kutoa maelekezo kuonyesha kwamba ana nguvu.

Je, kuna haki ya siasa? Kama CCM wanaweza wanatuhumu, wakakamata na bila hata kutoa sababu wakasema achia; upo umuhimu wa sheria nchini?

PIA SOMA

- Kuelekea 2025 - Katibu Mkuu wa CCM, Dkt. Nchimbi aiagiza Serikali kuwaachia Viongozi wa CHADEMA
 
Tuachane na ccm watanzania.
 
Old school politics.

Kuna watu bado wako gizani, wanawaza kizamani saaana, kipo kile kizazi kinaamini chenyewe kikisema ndio alpha na omega, hutakiwi kupinga maana wao ndio wenye akili sana lakini pia ndio wameshikilia dola.
Watu hawa mara nyingi hawajui athari za maendeleo ya Dunia na uelekeo wake matokeo yake huishia kuleta maafa.

Sasa hivi tuko kwenye free world, free thinking, free minds, hupaswi kuwa rigid baadala yake unapaswa sana kuwa flexible.
 
Kuna kaukweli
 
Hakukuwa na ulazima wowote wa Nchombi kutoa maelekezo hayo hadharani, angeweza kuongea tu na Waziri husika au Mkuu wa Jeshi la Polisi kuhusu kuwaachia huru Viongozi hao wa CHADEMA.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…