Je, Katiba Mpya ni Kipaumbele cha Mtanzania Kweli?

Je, Katiba Mpya ni Kipaumbele cha Mtanzania Kweli?

Ngaliwe

Senior Member
Joined
Dec 30, 2015
Posts
164
Reaction score
374
HOJA ya Katiba mpya imeanza tena kuibuka kwa kasi kidogo, kwa maelezo kwamba hiki ni kipaumbele cha taifa kwa sasa. Kwamba baadhi yetu wanaamini kwamba bila Katiba mpya hatuwezi kupiga hatua za maendeleo kama ambavyo tunatarajia.

Hakuna ubishi juu ya umuhimu wa Katiba kwa nchi yoyote, kwa kuwa Katiba ndiyo sheria mama na hiyo ndiyo mhimili wa sheria zingine zote, ni muhimu sana kwa taifa kuwa na katiba yake ambayo itaisaidia kufikia malengo ambayo watu wake wamejiwekea.

Pamoja na umuhimu huu, ni kweli kwamba Tanzania kama taifa kwa sasa tunahitaji kuwa na katiba mpya kama kipaumbele muhimu kuliko masuala mengine yanayolikabili taifa letu? Hili ni suala la mjadala lakini katika kujenga msingi wa hoja yangu ninaomba niongozwe na hekima hii ya Baba wa Taifa Mwalimu Kambarage Nyerere kuhusu umuhimu wa Katiba.

Haijalishi mtakuwa na Katiba ya namna gani, kama nchi haina maadili ya Taifa yatakayomwezesha Rais kusema ingawa katiba inaniniruhusu kufanya hili, siwezi kulifanya kwa kuwa si Utanzania, au wananchi kusema hatuwezi kufanya hili kwa sababu siyo utanzania liwe limetoka kwa rais au rais kipeuo cha pili, vinginevyo wananchi watabaki kuwa waathirika wa udikteta.

Mwalimu anasema nini, pamoja na umuhimu wa katiba lakini kwa yenyewe siyo kila kitu na kwamba kuwa na Katiba nzuri hakumaanishi ndiyo mwisho wa changamoto zote. Tukitaka kuwa wakweli tutatambua kwamba hatimaye bila maadili yanayowezesha utekelezaji makini wa katiba, haijalishi katiba hiyo inaandika na kutamka mambo mazuri kiasi gani, yanaweza kubaki kuwa maandishi tu bila kuwa na dhamira ya dhati ya utekelezaji.

Hii ndiyo kusema kwamba, kama tunayo dhamira na maadili mema yanayoliwezesha taifa letu kutekeleza mahitaji yake ya msingi kama vipaumbele vya kuwaletea watu maendeleo, hatuhitaji udharura wa kukimbilia katiba mpya kwa sasa, wakati maadili ya kitaifa hayohayo yanawezesha katiba iliyopo sasa kutekelezwa kwa manufaa makubwa ya taifa huku tukisukuma mbele vipaumbele vya kweli vya taifa na kuwaondolea wananchi umasikini.

Ni kweli kwamba wananchi walio wengi kipaumbele chao cha kwanza ni kupata barabara nzuri kwenye vijiji, mitaa na vitongoji vyao, wakulima wapate pembejeo kwa bei nafuu na uhakika wa masoko ya bidhaa za kilimo, vijana wapate ajira, mazingira mazuri ya uwekezaji na uanzishaji wa biashara, kuboresha huduma za afya, elimu na miundombinu mingine wezeshi kwa ajili ya kuweka mazingira mazuri ya kuendeleza taifa letu, haya hayategemei Katiba mpya.

Kama taifa lazima tujitafakari na kuona tunahitaji nini hasa kwa sasa, ni lazima ifike mahali tukubali kwamba pamoja na umuhimu wa harakati za masuala ya siasa katika nchi, lakini lazima yawe kwa kipimo na kiasi, nchi zote ambazo zimeendelea zilipiga hatua kubwa ya maendeleo walifika mahali wakitambua wanahitaji nini na kwa sababu gani bila kujali dunia ya nje inashinikiza nini.

Nchi nyingi hata za Ulaya zilifanya mapinduzi makubwa ya maendeleo kwa watu wao katika nyakati ambazo waliamua kuchagua kuelekeza nguvu zao kwenye mahitaji na vipaumbele vyao vya kweli bila kupelekwa pelekwa na mahitaji ya mataifa wengine, yenye maslahi zaidi na mashinikizo hayo kuliko tunaoshinikizwa.

Lipo kosa moja ambalo dunia inafanya, inashinikiza sisi nchi zinazoendelea turuke hatua ambayo mataifa makubwa walipitia wakiongozwa na mila na tamaduni zao lakini sisi wanataka turuke hatua hizo wakati wanajua fika kwamba kwa kufanya hivyo hawatusaidii kufikia kufikia malengo yetu, na kutufanya tuvurugikiwe na kuchanganyikiwa tu kama anavyokiri Mwanadiplomasia nguli wa Marekani, Dk. Henry Kissinger.

West have fallen prey to the temptation of ignoring history and judging every new state by criteria of their own civilization. It is often overlooked that the institutions of the west did not spring full blown from the brow of contemporaries but evolved over centuries which shaped frontiers and defined legitimacy, constitutional provisions, and basic values.”

Kwa tafsiri isiyo rasmi anasema “Mataifa ya Magaharibi yameangukia katika mtengo wa kupuuza historia na kuyapima mataifa mapya kwa vigezo vya ustaarabu wao (wa Kimagharibi). Yanapuuza ukweli kwamba taasisi za kimagharibi hazikukua ghafla tu, isipokuwa zilijiimarisha tarataibu kwa karne kadhaa ili kujenga uhalali, katiba na msingi ya maadili.”

Sisi pia tunataka kuingia katika mtego huu, tunataka kujipima kwa viwango vya mataifa ambayo, Marekani kwa mfano, ina umri wa miaka 245 ya uhuru. Tangu ilipopata uhuru toka kwa Waingereza Julai 04, 1776 Taifa hilo limepita katika hatua nyingi mno za hovyo na za maana, mpaka kufika hapa lilipofika, lakini likiongozwa na mila, utamaduni na historia yake.

Tanzania katika umri wake wa miaka 60 ya Uhuru, haimaanishi tupite kila aina ya madhira waliyopitia, hilo haliwezekani kutokana na tofauti za mazingira, utamaduni na nyakati. Lakini ni muhimu sana kutambua kwamba pia hatuwezi kupiga hatua za maana kwa kuiga kila kitu chao kwa sababu zile zile za historia, utamaduni na nyakati, tunachotakiwa kufanya ni kujiruhusu sisi kama taifa kukua na kujiimarisha katika misingi ya maadili na mfumo wa utawala unaozingatia misingi ya historia yetu, mila na utamaduni wetu.

Na kwa hili la katiba, tunafanya haraka isiyokuwa na sababu, kwanza kwa sababu siyo kweli kwamba hiki ni kipaumbele cha taifa, lakini pia kama alivyosema Baba wa Taifa hapo juu, maadili ya utaifa wetu kwa sasa yanatosha kabisa kuendelea kulijenga taifa letu kwa katiba iliyopo.

Wapo watu wanalinganisha na nchi jirani, Kenya kwa Katiba yao mpya, lakini liko jambo hawalioni wala hawataki kulijadili jinsi katiba hiyo inavyowaingiza kwenye migogoro kila uchao hali inayoliweka pia kwenye hatari ya kutumbukia kwenye migogoro isiyokoma (tutalijadili kwa upana hili wakati mwingine).

Itoshe tu kuhitimisha hapa kwamba, tukiamua kuwa wakweli kwa dhati za utambuzi wetu na kwa kuzingatia hali halisi nchini, utaona kwamba vipaumbele halisi vya taifa letu kwa sasa ni huduma za maji, umeme wa uhakika, huduma za afya na dawa, miundombinu, viwanda na miradi ya kimkakati inayoweza kuiweka Tanzania katika ramani ya ushindani katika uwekezaji kwenye ukanda huu wa Afrika na siyo katiba mpya.

ASANTE SAMIA
 
... pia kauli hii ya Mwl. Nyerere ikuongoze kutafakari ulichoandika, "... Katiba (hii) inanifanya dikteta kwa kigezo chochote kile cha kidemokrasia,” alisema Mwalimu Nyerere. Je, tunahitaji kuongozwa na dikteta? Kama ndio, hatuhitaji Katiba Mpya. Katiba hii ina matobo kiasi kwamba wanasiasa wanaichezea wapendavyo.

Hushangai leo hii hadi VP, PM, Speaker, NS, na JM nao wana kinga ya kutoshtakiwa wakiwa na hata baada ya kutoka madarakani? Jibu ni moja tu, Katiba hii imeacha mianya mingi mno ya kuchezewa. Kama hadi Uchaguzi Mkuu unaweza kuchezewa kwa "kiwango kile" unataka nini kitokee ili uamini kwamba Katiba Mpya ilihitajika tangu juzi wala sio leo?

Mifumo imara, demokrasia imara, uwazi, na uwajibikaji katika kila ngazi ni nguzo muhimu za maendeleo. Na hayo, kwa hali iliyopo, hayawawezakani bila Katiba Mpya!
 
Kwa hiyo huoni umuhimu wa Katiba Mpya na ambayo mapendekezo/maoni yake kwa asilimia kubwa yametokana na Wananchi wenyewe!

Unataka tuendelee kuikumbatia Katiba ya mwaka 1977 (Katiba ya Ccm) mpaka leo! Katiba ambayo inamfanya Rais na chama chake cha Ccm kutuendesha kama magari mabovu kupitia vyombo vya dola!

Hili halikubaliki hata kidogo! Katiba Mpya ni muhimu zaidi ya hizo barabara! Watanzania tunataka Katiba ambayo itamfanya Rais kuwa mtumishi wa Wananchi! Na siyo hii ya sasa inayomfanya kuwa mungu mtu!
 
..Je, katiba ya mwaka 1977 ilipoandikwa kuna shughuli zozote za maendeleo ambazo zilisimama au ziliathirika?

..siamini kama kuandika katiba mpya kutazuia au kusimamisha utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

..Ni BUSARA kuandika katiba mpya kipindi hiki taifa lina amani na mshikamano kuliko kusubiri machafuko yatokee ndipo tuanze zoezi hilo.

..Kenya mnayoitolea mfano walisubiri mpaka wakafarakana ndio maana wanaonekana kutokufaidika na uandishi wa katiba ya mpya.
 
Ukweli mchungu, Wananchi walio wengi, wanaona ni kama makelele tu kwa habari ya katiba...., kwa maana hiyo, kwa sasa,Suala la Katiba katika nchi yetu, ni hitaji la wanaoitaka Ikulu na hasa kupitia vyama mbalimbali

Kwa waliowengi, hitaji lao kubwa, Ni kupatikana Raisi atakayebeba maswali yao na kuyatatua tokea chini kabisa!!

Ijapokuwa katiba, ndio msingi bora wa ulinzi na usalama pia uhakika wa kuwafanya viongozi wawe bora hata kama hawataki
 
HOJA ya Katiba mpya imeanza tena kuibuka kwa kasi kidogo, kwa maelezo kwamba hiki ni kipaumbele cha taifa kwa sasa. Kwamba baadhi yetu wanaamini kwamba bila Katiba mpya hatuwezi kupiga hatua za maendeleo kama ambavyo tunatarajia.

Hakuna ubishi juu ya umuhimu wa Katiba kwa nchi yoyote, kwa kuwa Katiba ndiyo sheria mama na hiyo ndiyo mhimili wa sheria zingine zote, ni muhimu sana kwa taifa kuwa na katiba yake ambayo itaisaidia kufikia malengo ambayo watu wake wamejiwekea.

Pamoja na umuhimu huu, ni kweli kwamba Tanzania kama taifa kwa sasa tunahitaji kuwa na katiba mpya kama kipaumbele muhimu kuliko masuala mengine yanayolikabili taifa letu? Hili ni suala la mjadala lakini katika kujenga msingi wa hoja yangu ninaomba niongozwe na hekima hii ya Baba wa Taifa Mwalimu Kambarage Nyerere kuhusu umuhimu wa Katiba.

Haijalishi mtakuwa na Katiba ya namna gani, kama nchi haina maadili ya Taifa yatakayomwezesha Rais kusema ingawa katiba inaniniruhusu kufanya hili, siwezi kulifanya kwa kuwa si Utanzania, au wananchi kusema hatuwezi kufanya hili kwa sababu siyo utanzania liwe limetoka kwa rais au rais kipeuo cha pili, vinginevyo wananchi watabaki kuwa waathirika wa udikteta.

Mwalimu anasema nini, pamoja na umuhimu wa katiba lakini kwa yenyewe siyo kila kitu na kwamba kuwa na Katiba nzuri hakumaanishi ndiyo mwisho wa changamoto zote. Tukitaka kuwa wakweli tutatambua kwamba hatimaye bila maadili yanayowezesha utekelezaji makini wa katiba, haijalishi katiba hiyo inaandika na kutamka mambo mazuri kiasi gani, yanaweza kubaki kuwa maandishi tu bila kuwa na dhamira ya dhati ya utekelezaji.

Hii ndiyo kusema kwamba, kama tunayo dhamira na maadili mema yanayoliwezesha taifa letu kutekeleza mahitaji yake ya msingi kama vipaumbele vya kuwaletea watu maendeleo, hatuhitaji udharura wa kukimbilia katiba mpya kwa sasa, wakati maadili ya kitaifa hayohayo yanawezesha katiba iliyopo sasa kutekelezwa kwa manufaa makubwa ya taifa huku tukisukuma mbele vipaumbele vya kweli vya taifa na kuwaondolea wananchi umaskini.

Ni kweli kwamba wananchi walio wengi kipaumbele chao cha kwanza ni kupata barabara nzuri kwenye vijiji, mitaa na vitongoji vyao, wakulima wapate pembejeo kwa bei nafuu na uhakika wa masoko ya bidhaa za kilimo, vijana wapate ajira, mazingira mazuri ya uwekezaji na uanzishaji wa biashara, kuboresha huduma za afya, elimu na miundombinu mingine wezeshi kwa ajili ya kuweka mazingira mazuri ya kuendeleza taifa letu, haya hayategemei Katiba mpya.

Kama taifa lazima tujitafakari na kuona tunahitaji nini hasa kwa sasa, ni lazima ifike mahali tukubali kwamba pamoja na umuhimu wa harakati za masuala ya siasa katika nchi, lakini lazima yawe kwa kipimo na kiasi, nchi zote ambazo zimeendelea zilipiga hatua kubwa ya maendeleo walifika mahali wakitambua wanahitaji nini na kwa sababu gani bila kujali dunia ya nje inashinikiza nini.

Nchi nyingi hata za Ulaya zilifanya mapinduzi makubwa ya maendeleo kwa watu wao katika nyakati ambazo waliamua kuchagua kuelekeza nguvu zao kwenye mahitaji na vipaumbele vyao vya kweli bila kupelekwa pelekwa na mahitaji ya mataifa wengine, yenye maslahi zaidi na mashinikizo hayo kuliko tunaoshinikizwa.

Lipo kosa moja ambalo dunia inafanya, inashinikiza sisi nchi zinazoendelea turuke hatua ambayo mataifa makubwa walipitia wakiongozwa na mila na tamaduni zao lakini sisi wanataka turuke hatua hizo wakati wanajua fika kwamba kwa kufanya hivyo hawatusaidii kufikia kufikia malengo yetu, na kutufanya tuvurugikiwe na kuchanganyikiwa tu kama anavyokiri Mwanadiplomasia nguli wa Marekani, Dk. Henry Kissinger.

West have fallen prey to the temptation of ignoring history and judging every new state by criteria of their own civilization. It is often overlooked that the institutions of the west did not spring full blown from the brow of contemporaries but evolved over centuries which shaped frontiers and defined legitimacy, constitutional provisions, and basic values.”

Kwa tafsiri isiyo rasmi anasema “Mataifa ya Magaharibi yameangukia katika mtengo wa kupuuza historia na kuyapima mataifa mapya kwa vigezo vya ustaarabu wao (wa Kimagharibi). Yanapuuza ukweli kwamba taasisi za kimagharibi hazikukua ghafla tu, isipokuwa zilijiimarisha tarataibu kwa karne kadhaa ili kujenga uhalali, katiba na msingi ya maadili.”

Sisi pia tunataka kuingia katika mtego huu, tunataka kujipima kwa viwango vya mataifa ambayo, Marekani kwa mfano, ina umri wa miaka 245 ya uhuru. Tangu ilipopata uhuru toka kwa Waingereza Julai 04, 1776 Taifa hilo limepita katika hatua nyingi mno za hovyo na za maana, mpaka kufika hapa lilipofika, lakini likiongozwa na mila, utamaduni na historia yake.

Tanzania katika umri wake wa miaka 60 ya Uhuru, haimaanishi tupite kila aina ya madhira waliyopitia, hilo haliwezekani kutokana na tofauti za mazingira, utamaduni na nyakati. Lakini ni muhimu sana kutambua kwamba pia hatuwezi kupiga hatua za maana kwa kuiga kila kitu chao kwa sababu zile zile za historia, utamaduni na nyakati, tunachotakiwa kufanya ni kujiruhusu sisi kama taifa kukua na kujiimarisha katika misingi ya maadili na mfumo wa utawala unaozingatia misingi ya historia yetu, mila na utamaduni wetu.

Na kwa hili la katiba, tunafanya haraka isiyokuwa na sababu, kwanza kwa sababu siyo kweli kwamba hiki ni kipaumbele cha taifa, lakini pia kama alivyosema Baba wa Taifa hapo juu, maadili ya utaifa wetu kwa sasa yanatosha kabisa kuendelea kulijenga taifa letu kwa katiba iliyopo.

Wapo watu wanalinganisha na nchi jirani, Kenya kwa Katiba yao mpya, lakini liko jambo hawalioni wala hawataki kulijadili jinsi katiba hiyo inavyowaingiza kwenye migogoro kila uchao hali inayoliweka pia kwenye hatari ya kutumbukia kwenye migogoro isiyokoma (tutalijadili kwa upana hili wakati mwingine).

Itoshe tu kuhitimisha hapa kwamba, tukiamua kuwa wakweli kwa dhati za utambuzi wetu na kwa kuzingatia hali halisi nchini, utaona kwamba vipaumbele halisi vya taifa letu kwa sasa ni huduma za maji, umeme wa uhakika, huduma za afya na dawa, miundombinu, viwanda na miradi ya kimkakati inayoweza kuiweka Tanzania katika ramani ya ushindani katika uwekezaji kwenye ukanda huu wa Afrika na siyo katiba mpya.

ASANTE SAMIA
Unajipa moyo ili muendelee kuila nchi hii kiulani.
Kizazi cha sasa kimeshastuka, katiba nzuri ndio kila kitu.
Sijawahi kuona katiba mbovu kama ya Tanzania, na hii yote ni makusudi ya ccm wakidhani watatawala milele.
Kuwa na maadili na uwajibikaji kutatoka wapi wakati watu wengine wanajiamulia kufanya mambo yao wanavyotaka hata kuvunja katiba wakijua hawawezi kuwajibishwa na chochote?
Nchi hii haina katiba inayoweka mwelekeo au sera ya nchi, sera ya nchi inategemea na nani yuko madarakani kama raisi.
Kukiingia chama kingine madarakani kwa katiba hii hii, mbona ccm watalia na kusaga meno, na itakuwa ndio mwisho wake kuingia madarakani unless kuwe na katiba inayoweka usawa kwa wananchi wote katka shughuli zao na hasa katika kuendesha siasa katika nchi yao.
Tangu tumepata uhuru nchi hii imepitia vipindi mbalimbali ambavyo nchi haikuweza kutulia na kujenga uchumi ulio imara. Haya yote yalisababishwa na kutokuwa na katiba imara inayoweza kusimamia maendeleo ya uchumi wa nchi, badala yake nchi imetegemea sera za raisi aliyeko madarakani, kwa mfano;
1. Awamu ya kwanza ya mwl Nyerere na hata kabla ya uhuru, kulikuwa na wazungu na waasia wengi waliowekeza hapa nchini na kujenga hapa nchini.
Nyerere aliwaita mabepari, makabaila na mabeberu, mali zao zote zilitaifishwa na kukabidhiwa wananchi kisa ujamaa.
unakabidhi mtu kuendesha kitu asichokijua wala kukianzisha, unategemea nini?
Swala lilikuwa ni nchi kuangalia kwamba hawa matajiri wanachangiaje katika uchumi wa nchi?
kama hawachangii nchi ifanyeje waweze kuchangia?
Tangu azimio la Arusha, wawekezaji wengi mpaka leo hawana imani na nchi hii.
Wenzetu majirani zetu kama Kenya wamekuwa na wawekezaji wa nje tangu kabla ya uhuru, ndio maana viwanda vya kenya na bidhaa zao zina compete duniani na uchumi wao uko imara.
2. Awamu ya pili, ya tatu na ya nne wote walijitahidi kukuza uchumi na ku encourage uwekezaji, lakini mafanikio hayakuwa makubwa.
3. Awamu ya tano ndio kabisaa ikafukuza wawekezaji na wafanyabiashara hadi wa ndani, na wananchi wengine waliikimbia nchi kwa kuhofia usalama wa maisha yao, ndani ya katiba hii hii inayosema inalinda wananchi na mali zao. wakusimamia hilo ni nani?
Mama yetu Samia anayo kazi kubwa na ngumu. Sio rahisi mwekezaji alio serious kuwekeza billions au trillions nchi hii, kwa vile hawajui kesho kitatokea nini. wanaowekeza wanajaribu jaribu tu.
Katiba nzuri, yenye sera za kuendeleza uchumi wa nchi ndiyo itakayotuvusha hapa tulipo.
Haiwezekani nchi ikaendeshwa kwa siasa, raisi ndio anaamua kila kitu kutoka juu hadi chini, utaalamu umewekwa pembeni.
 
Naamini kuna ambao hawajui chochote kuhusu hiyo katiba mpya
 
Ukweli mchungu, Wananchi walio wengi, wanaona ni kama makelele tu kwa habari ya katiba...., kwa maana hiyo, kwa sasa,Suala la Katiba katika nchi yetu, ni hitaji la wanaoitaka Ikulu na hasa kupitia vyama mbalimbali

Kwa waliowengi, hitaji lao kubwa, Ni kupatikana Raisi atakayebeba maswali yao na kuyatatua tokea chini kabisa!!

Ijapokuwa katiba, ndio msingi bora wa ulinzi na usalama pia uhakika wa kuwafanya viongozi wawe bora hata kama hawataki

..katiba mpya ili waingie ikulu?

..au katiba mbovu ya zamani ili wasitoke ikulu?

..au katiba mpya bora yenye kutoa HAKI SAWA kwa kila Mtanzania?

..Katiba ya sasa imeanza kutuletea malalamiko toka kwa baadhi ya Watz. Je, tusubiri mpaka kutokee machafuko ndipo tuandike katiba mpya?

..I think we need to be proactive kwa kuandika katiba mpya sasa ili kuepukana na hatari zinazoweza kutukuta mbele ya safari.

..Tukisubiri katiba mpya iwe " kipaumbele " , sawa na walivyo Sudan, tutakuwa tumekosea na tumechelewa.
 
Itoshe tu kuhitimisha hapa kwamba, tukiamua kuwa wakweli kwa dhati za utambuzi wetu na kwa kuzingatia hali halisi nchini, utaona kwamba vipaumbele halisi vya taifa letu kwa sasa ni huduma za maji, umeme wa uhakika, huduma za afya na dawa, miundombinu, viwanda na miradi ya kimkakati inayoweza kuiweka Tanzania katika ramani ya ushindani katika uwekezaji kwenye ukanda huu wa Afrika na siyo katiba mpya.

ASANTE SAMIA
Ni kweli hivi ndo vipaumbele. Ila katika mpya ni means (nyenzo) ya kuleta hivi vipaumbele.

Iko hivi, ili kupata hivyo vipaumbele kwa haraka tunahitaji uongozi bora na matumizi sahihi ya rasilimali. Nahitaji muundo na mifumo mipya ya uendeshaji wa nchi. Ndo maana tunahitaji katiba mpya sasa hivi.

Ukipesha pori sasa hivi ili ulime. Vipaumbele vyako vitakuwa kufyeka shamba, kukwatua, kulima, kupanda etc. Ila unahitaji mashoka, mapanga, majembe etc. Huwezi kumwambia mkulima achana na kununua mapanga kwa sasa kwa sababu kipaumbele chako ni kufyeka.

Sisi tunasema tununue mapanga na mashoka kwanza. Nyie mnasema hapana kipaumbele chetu ni kufyeka..
 
HOJA ya Katiba mpya imeanza tena kuibuka kwa kasi kidogo, kwa maelezo kwamba hiki ni kipaumbele cha taifa kwa sasa. Kwamba baadhi yetu wanaamini kwamba bila Katiba mpya hatuwezi kupiga hatua za maendeleo kama ambavyo tunatarajia.

Hakuna ubishi juu ya umuhimu wa Katiba kwa nchi yoyote, kwa kuwa Katiba ndiyo sheria mama na hiyo ndiyo mhimili wa sheria zingine zote, ni muhimu sana kwa taifa kuwa na katiba yake ambayo itaisaidia kufikia malengo ambayo watu wake wamejiwekea.

Pamoja na umuhimu huu, ni kweli kwamba Tanzania kama taifa kwa sasa tunahitaji kuwa na katiba mpya kama kipaumbele muhimu kuliko masuala mengine yanayolikabili taifa letu? Hili ni suala la mjadala lakini katika kujenga msingi wa hoja yangu ninaomba niongozwe na hekima hii ya Baba wa Taifa Mwalimu Kambarage Nyerere kuhusu umuhimu wa Katiba.

Haijalishi mtakuwa na Katiba ya namna gani, kama nchi haina maadili ya Taifa yatakayomwezesha Rais kusema ingawa katiba inaniniruhusu kufanya hili, siwezi kulifanya kwa kuwa si Utanzania, au wananchi kusema hatuwezi kufanya hili kwa sababu siyo utanzania liwe limetoka kwa rais au rais kipeuo cha pili, vinginevyo wananchi watabaki kuwa waathirika wa udikteta.

Mwalimu anasema nini, pamoja na umuhimu wa katiba lakini kwa yenyewe siyo kila kitu na kwamba kuwa na Katiba nzuri hakumaanishi ndiyo mwisho wa changamoto zote. Tukitaka kuwa wakweli tutatambua kwamba hatimaye bila maadili yanayowezesha utekelezaji makini wa katiba, haijalishi katiba hiyo inaandika na kutamka mambo mazuri kiasi gani, yanaweza kubaki kuwa maandishi tu bila kuwa na dhamira ya dhati ya utekelezaji.

Hii ndiyo kusema kwamba, kama tunayo dhamira na maadili mema yanayoliwezesha taifa letu kutekeleza mahitaji yake ya msingi kama vipaumbele vya kuwaletea watu maendeleo, hatuhitaji udharura wa kukimbilia katiba mpya kwa sasa, wakati maadili ya kitaifa hayohayo yanawezesha katiba iliyopo sasa kutekelezwa kwa manufaa makubwa ya taifa huku tukisukuma mbele vipaumbele vya kweli vya taifa na kuwaondolea wananchi umasikini.

Ni kweli kwamba wananchi walio wengi kipaumbele chao cha kwanza ni kupata barabara nzuri kwenye vijiji, mitaa na vitongoji vyao, wakulima wapate pembejeo kwa bei nafuu na uhakika wa masoko ya bidhaa za kilimo, vijana wapate ajira, mazingira mazuri ya uwekezaji na uanzishaji wa biashara, kuboresha huduma za afya, elimu na miundombinu mingine wezeshi kwa ajili ya kuweka mazingira mazuri ya kuendeleza taifa letu, haya hayategemei Katiba mpya.

Kama taifa lazima tujitafakari na kuona tunahitaji nini hasa kwa sasa, ni lazima ifike mahali tukubali kwamba pamoja na umuhimu wa harakati za masuala ya siasa katika nchi, lakini lazima yawe kwa kipimo na kiasi, nchi zote ambazo zimeendelea zilipiga hatua kubwa ya maendeleo walifika mahali wakitambua wanahitaji nini na kwa sababu gani bila kujali dunia ya nje inashinikiza nini.

Nchi nyingi hata za Ulaya zilifanya mapinduzi makubwa ya maendeleo kwa watu wao katika nyakati ambazo waliamua kuchagua kuelekeza nguvu zao kwenye mahitaji na vipaumbele vyao vya kweli bila kupelekwa pelekwa na mahitaji ya mataifa wengine, yenye maslahi zaidi na mashinikizo hayo kuliko tunaoshinikizwa.

Lipo kosa moja ambalo dunia inafanya, inashinikiza sisi nchi zinazoendelea turuke hatua ambayo mataifa makubwa walipitia wakiongozwa na mila na tamaduni zao lakini sisi wanataka turuke hatua hizo wakati wanajua fika kwamba kwa kufanya hivyo hawatusaidii kufikia kufikia malengo yetu, na kutufanya tuvurugikiwe na kuchanganyikiwa tu kama anavyokiri Mwanadiplomasia nguli wa Marekani, Dk. Henry Kissinger.

West have fallen prey to the temptation of ignoring history and judging every new state by criteria of their own civilization. It is often overlooked that the institutions of the west did not spring full blown from the brow of contemporaries but evolved over centuries which shaped frontiers and defined legitimacy, constitutional provisions, and basic values.”

Kwa tafsiri isiyo rasmi anasema “Mataifa ya Magaharibi yameangukia katika mtengo wa kupuuza historia na kuyapima mataifa mapya kwa vigezo vya ustaarabu wao (wa Kimagharibi). Yanapuuza ukweli kwamba taasisi za kimagharibi hazikukua ghafla tu, isipokuwa zilijiimarisha tarataibu kwa karne kadhaa ili kujenga uhalali, katiba na msingi ya maadili.”

Sisi pia tunataka kuingia katika mtego huu, tunataka kujipima kwa viwango vya mataifa ambayo, Marekani kwa mfano, ina umri wa miaka 245 ya uhuru. Tangu ilipopata uhuru toka kwa Waingereza Julai 04, 1776 Taifa hilo limepita katika hatua nyingi mno za hovyo na za maana, mpaka kufika hapa lilipofika, lakini likiongozwa na mila, utamaduni na historia yake.

Tanzania katika umri wake wa miaka 60 ya Uhuru, haimaanishi tupite kila aina ya madhira waliyopitia, hilo haliwezekani kutokana na tofauti za mazingira, utamaduni na nyakati. Lakini ni muhimu sana kutambua kwamba pia hatuwezi kupiga hatua za maana kwa kuiga kila kitu chao kwa sababu zile zile za historia, utamaduni na nyakati, tunachotakiwa kufanya ni kujiruhusu sisi kama taifa kukua na kujiimarisha katika misingi ya maadili na mfumo wa utawala unaozingatia misingi ya historia yetu, mila na utamaduni wetu.

Na kwa hili la katiba, tunafanya haraka isiyokuwa na sababu, kwanza kwa sababu siyo kweli kwamba hiki ni kipaumbele cha taifa, lakini pia kama alivyosema Baba wa Taifa hapo juu, maadili ya utaifa wetu kwa sasa yanatosha kabisa kuendelea kulijenga taifa letu kwa katiba iliyopo.

Wapo watu wanalinganisha na nchi jirani, Kenya kwa Katiba yao mpya, lakini liko jambo hawalioni wala hawataki kulijadili jinsi katiba hiyo inavyowaingiza kwenye migogoro kila uchao hali inayoliweka pia kwenye hatari ya kutumbukia kwenye migogoro isiyokoma (tutalijadili kwa upana hili wakati mwingine).

Itoshe tu kuhitimisha hapa kwamba, tukiamua kuwa wakweli kwa dhati za utambuzi wetu na kwa kuzingatia hali halisi nchini, utaona kwamba vipaumbele halisi vya taifa letu kwa sasa ni huduma za maji, umeme wa uhakika, huduma za afya na dawa, miundombinu, viwanda na miradi ya kimkakati inayoweza kuiweka Tanzania katika ramani ya ushindani katika uwekezaji kwenye ukanda huu wa Afrika na siyo katiba mpya.

ASANTE SAMIA
Katiba mpya ni mhimu sana na ni juu ya mambo yote. Bila kuwa na muundo wa uongozi unaokidhi mazingira ya kijamii na kiuchumi ya sasa, hali ya maendeleo kiujumla itabaki ndoto itakayoambatana na matumizi makubwa ya "state power". Wasomi wanaamini: "It is the superstructure (how you govern yourself) that shapes socio-economic direction of a country".
 
Unafiki ndio unakwamisha katiba mpya.
Ila nina imani Raisi SSH,atatupa katiba mpya.
 
HOJA ya Katiba mpya imeanza tena kuibuka kwa kasi kidogo, kwa maelezo kwamba hiki ni kipaumbele cha taifa kwa sasa. Kwamba baadhi yetu wanaamini kwamba bila Katiba mpya hatuwezi kupiga hatua za maendeleo kama ambavyo tunatarajia.

Hakuna ubishi juu ya umuhimu wa Katiba kwa nchi yoyote, kwa kuwa Katiba ndiyo sheria mama na hiyo ndiyo mhimili wa sheria zingine zote, ni muhimu sana kwa taifa kuwa na katiba yake ambayo itaisaidia kufikia malengo ambayo watu wake wamejiwekea.

Pamoja na umuhimu huu, ni kweli kwamba Tanzania kama taifa kwa sasa tunahitaji kuwa na katiba mpya kama kipaumbele muhimu kuliko masuala mengine yanayolikabili taifa letu? Hili ni suala la mjadala lakini katika kujenga msingi wa hoja yangu ninaomba niongozwe na hekima hii ya Baba wa Taifa Mwalimu Kambarage Nyerere kuhusu umuhimu wa Katiba.

Haijalishi mtakuwa na Katiba ya namna gani, kama nchi haina maadili ya Taifa yatakayomwezesha Rais kusema ingawa katiba inaniniruhusu kufanya hili, siwezi kulifanya kwa kuwa si Utanzania, au wananchi kusema hatuwezi kufanya hili kwa sababu siyo utanzania liwe limetoka kwa rais au rais kipeuo cha pili, vinginevyo wananchi watabaki kuwa waathirika wa udikteta.

Mwalimu anasema nini, pamoja na umuhimu wa katiba lakini kwa yenyewe siyo kila kitu na kwamba kuwa na Katiba nzuri hakumaanishi ndiyo mwisho wa changamoto zote. Tukitaka kuwa wakweli tutatambua kwamba hatimaye bila maadili yanayowezesha utekelezaji makini wa katiba, haijalishi katiba hiyo inaandika na kutamka mambo mazuri kiasi gani, yanaweza kubaki kuwa maandishi tu bila kuwa na dhamira ya dhati ya utekelezaji.

Hii ndiyo kusema kwamba, kama tunayo dhamira na maadili mema yanayoliwezesha taifa letu kutekeleza mahitaji yake ya msingi kama vipaumbele vya kuwaletea watu maendeleo, hatuhitaji udharura wa kukimbilia katiba mpya kwa sasa, wakati maadili ya kitaifa hayohayo yanawezesha katiba iliyopo sasa kutekelezwa kwa manufaa makubwa ya taifa huku tukisukuma mbele vipaumbele vya kweli vya taifa na kuwaondolea wananchi umasikini.

Ni kweli kwamba wananchi walio wengi kipaumbele chao cha kwanza ni kupata barabara nzuri kwenye vijiji, mitaa na vitongoji vyao, wakulima wapate pembejeo kwa bei nafuu na uhakika wa masoko ya bidhaa za kilimo, vijana wapate ajira, mazingira mazuri ya uwekezaji na uanzishaji wa biashara, kuboresha huduma za afya, elimu na miundombinu mingine wezeshi kwa ajili ya kuweka mazingira mazuri ya kuendeleza taifa letu, haya hayategemei Katiba mpya.

Kama taifa lazima tujitafakari na kuona tunahitaji nini hasa kwa sasa, ni lazima ifike mahali tukubali kwamba pamoja na umuhimu wa harakati za masuala ya siasa katika nchi, lakini lazima yawe kwa kipimo na kiasi, nchi zote ambazo zimeendelea zilipiga hatua kubwa ya maendeleo walifika mahali wakitambua wanahitaji nini na kwa sababu gani bila kujali dunia ya nje inashinikiza nini.

Nchi nyingi hata za Ulaya zilifanya mapinduzi makubwa ya maendeleo kwa watu wao katika nyakati ambazo waliamua kuchagua kuelekeza nguvu zao kwenye mahitaji na vipaumbele vyao vya kweli bila kupelekwa pelekwa na mahitaji ya mataifa wengine, yenye maslahi zaidi na mashinikizo hayo kuliko tunaoshinikizwa.

Lipo kosa moja ambalo dunia inafanya, inashinikiza sisi nchi zinazoendelea turuke hatua ambayo mataifa makubwa walipitia wakiongozwa na mila na tamaduni zao lakini sisi wanataka turuke hatua hizo wakati wanajua fika kwamba kwa kufanya hivyo hawatusaidii kufikia kufikia malengo yetu, na kutufanya tuvurugikiwe na kuchanganyikiwa tu kama anavyokiri Mwanadiplomasia nguli wa Marekani, Dk. Henry Kissinger.

West have fallen prey to the temptation of ignoring history and judging every new state by criteria of their own civilization. It is often overlooked that the institutions of the west did not spring full blown from the brow of contemporaries but evolved over centuries which shaped frontiers and defined legitimacy, constitutional provisions, and basic values.”

Kwa tafsiri isiyo rasmi anasema “Mataifa ya Magaharibi yameangukia katika mtengo wa kupuuza historia na kuyapima mataifa mapya kwa vigezo vya ustaarabu wao (wa Kimagharibi). Yanapuuza ukweli kwamba taasisi za kimagharibi hazikukua ghafla tu, isipokuwa zilijiimarisha tarataibu kwa karne kadhaa ili kujenga uhalali, katiba na msingi ya maadili.”

Sisi pia tunataka kuingia katika mtego huu, tunataka kujipima kwa viwango vya mataifa ambayo, Marekani kwa mfano, ina umri wa miaka 245 ya uhuru. Tangu ilipopata uhuru toka kwa Waingereza Julai 04, 1776 Taifa hilo limepita katika hatua nyingi mno za hovyo na za maana, mpaka kufika hapa lilipofika, lakini likiongozwa na mila, utamaduni na historia yake.

Tanzania katika umri wake wa miaka 60 ya Uhuru, haimaanishi tupite kila aina ya madhira waliyopitia, hilo haliwezekani kutokana na tofauti za mazingira, utamaduni na nyakati. Lakini ni muhimu sana kutambua kwamba pia hatuwezi kupiga hatua za maana kwa kuiga kila kitu chao kwa sababu zile zile za historia, utamaduni na nyakati, tunachotakiwa kufanya ni kujiruhusu sisi kama taifa kukua na kujiimarisha katika misingi ya maadili na mfumo wa utawala unaozingatia misingi ya historia yetu, mila na utamaduni wetu.

Na kwa hili la katiba, tunafanya haraka isiyokuwa na sababu, kwanza kwa sababu siyo kweli kwamba hiki ni kipaumbele cha taifa, lakini pia kama alivyosema Baba wa Taifa hapo juu, maadili ya utaifa wetu kwa sasa yanatosha kabisa kuendelea kulijenga taifa letu kwa katiba iliyopo.

Wapo watu wanalinganisha na nchi jirani, Kenya kwa Katiba yao mpya, lakini liko jambo hawalioni wala hawataki kulijadili jinsi katiba hiyo inavyowaingiza kwenye migogoro kila uchao hali inayoliweka pia kwenye hatari ya kutumbukia kwenye migogoro isiyokoma (tutalijadili kwa upana hili wakati mwingine).

Itoshe tu kuhitimisha hapa kwamba, tukiamua kuwa wakweli kwa dhati za utambuzi wetu na kwa kuzingatia hali halisi nchini, utaona kwamba vipaumbele halisi vya taifa letu kwa sasa ni huduma za maji, umeme wa uhakika, huduma za afya na dawa, miundombinu, viwanda na miradi ya kimkakati inayoweza kuiweka Tanzania katika ramani ya ushindani katika uwekezaji kwenye ukanda huu wa Afrika na siyo katiba mpya.

ASANTE SAMIA
Kenya ambao wana katiba mpya kwa sasa kuna mzozo wa kiutendaji kati ya mahakama na Executive branch.
Tume ya utumishi ya mahakama imependekeza majaji na kumtaka Rais aidhinishe uteuzi, Rais amegoma.

Majuma machache yaliyopita Mahakama ilitengua move ya kura za maoni ya BBI; ukiangali Kenya katiba mpya haikuwa na maslahi ya wananchi per se;ila namna gani wanagawana mkate wa taifa.

hata hapa kwetu, majority wanaodai katiba mpya hawana lengo hasa la uwajibikaji kwa serikali ili kukabiliana na maadui wakubwa wa taifa ambao ni umasikini, ujinga na maradhi; isipokuwa tume ya uchaguzi ambayo itawahakikishia ugali kwa ajili yao na familia zao na sio namna gani tunatumia advantage ya Tanzania kulifikia soko la nchi zilizotuzunguka kwa kuuza bidhaa na huduma.

Tunatumai Mhe. Rais na wasaidizi wake watakuwa na mkakati jumuishi kwa kuijenga sekta binafsi ya Tanzania ambayo utalenga hasa kutengeneza ajira za vijana kwa kuanzia soko la ndani kwa bidhaa ambazo zaweza kuzalishwa ndani na ikiwekezekana muazo yafikia masoko ya Kenya, Uganda, Rwanda, Congo, Zambia, Malawi, Mozambique, Madagascar, Comoro na Seychelles.

Nimesikia Mhe. Rais analenga kuanzia benki ya ujasiliamali, bila shaka itajengewa mifumo jumuishi yenye watu wanaofikiri nje ya box ili kuifanya Tanzania ya sasa iwe na neema kwa kizazi cha sasa na vijavyo.
 
Back
Top Bottom