Je kibubu kitanisaidia?

mkuu kutapeliwa sio kazi ndogo....


mkuu ntaku PM
 
Nakumbuka zamaaani sana kulikuwa na kawimbo kamoja hivi kanaimbwa '...moto,mwizi,maji na majanga mbalimbali...' hahahahahahahahaha!
tehehehe kwa maana hayo majanga ni kikwazo kwa kibubu mkuu au nimekuelewa vibaya
 
Mimi nimejaribu hii hapa chini toka mwezi wa mwanza..ila sasa vyuma vimekaza nilipofika mwezi wa saba nikaanza kupumulia mashine, kwa hiyo nina deni la mwezi wa nane na wa tisa..du.. ila i hope nitafanikiwa lazma nikamilishe kila mwezi na december ikifika niwe na hiyo amount.. nimetengeneza kibubu cha chuma kabisa ambacho siwez kukifungua hadi kupeleka kwa fundi welding. Ukiangalia hapo kila wiki inaongezeka 3000..
 
kiongozi hii sijakusoma vizuri ni kitu gani kiongozi??
 
Aweke bank ni best option

Sent from my itel S11 using JamiiForums mobile app
 

kama unaweza save laki mbili ni bora ukafungua kibubu account kwa maana unaweza weka iyo laki mbili kila mwezi kweny account yako ya kibubu(hii ni kama fixed account tofauti ni kwamba fixed unaweka at lump sum lakini hii unaweka kiasi kile kile kila mwezi kama ni laki kwa miezi 12 utakatwa laki kila mwezi kwa miezi yote iyo)

note: rate the fixed sasa hivi sio rafiki sana hivo huwezi pata faida kwa kiasi icho kidogo cha fedha, na hata iyo kibubu hakina rate nzuri sana lakini itakusaidia fikia malengo yako kwa iyo kipindi ulichokipanga.......................

nakutakia kila la heri mkuu
 
nashkuru sana ila kama umeniacha kimtindo hivi hyo kibubu account yapatikana benki huko ama vipi kiongozi?
 
mkuu maneno yako yapo kikubwa zaidi ebu nieleze kwa uwazi kabisa mkuu ili tupate mafaida kem kem
Boss uyo jamaa kasema ukiweka fixed kuna kushika kwa hisa sasa bora uchonge kibubu chako ili mradi usiwe na tamaa
 
Ungekuwa na access na Saccos nzuri ungejiunga hapo. Unaweka ila pia inazaa.
 
nashkuru sana ila kama umeniacha kimtindo hivi hyo kibubu account yapatikana benki huko ama vipi kiongozi?

tembelea DTB bank niliona wanatangaza iyo huduma nikaipenda nilifanya calculation nikagundua ile rate ni hakuna kitu ila kwa security ni bora kuweka pesa yako bank kuliko kibubu cha nyumban kwa maana nyumbani kuna mengi likitoka la kutokea hutoenda claim popote
 
Boss uyo jamaa kasema ukiweka fixed kuna kushika kwa hisa sasa bora uchonge kibubu chako ili mradi usiwe na tamaa
kiongozi nashkuru kwa mawazo yako na ufafanuzi hapo juu...

unajua hata ukiweka benki kisha ukawa na tamaa basi utazitoa tu hata kama kadi uliacha mbagala basi utaifuata mbona...

ila hichi kibubu yataka kusahau hasa...
pia mtu ukifuzu kuweka kwenye kibubu basi ni mafunzo tosha ya kuicontrol nafsi yako mana nafsi itataka uchomoe kumi kumi tu
 
Mpigaji
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…