Je Kigezo cha Elimu katika ndoa, uchmba na Urafiki ni cha msingi au ni ubaguzi

Je Kigezo cha Elimu katika ndoa, uchmba na Urafiki ni cha msingi au ni ubaguzi

mwanalumango

JF-Expert Member
Joined
Dec 13, 2010
Posts
232
Reaction score
279
Nachokoza tu kwa weledi wangu mdogo kuwa kutafuta rafiki wa kimahaba kwa minajiri ya kuwa mchumba na hatimaye my wife/husband ni kigezo kisichokuwa na msingi na ni cha kibaguzi na unyanyapaa wa wasiosoma. Si lazima iwe sahihi sana ila kuna sababu zinazojitokeza kwenye maisha halisi ya Kitanzania inayoonesha kuwa Elimu si kipimo kizuri sana cha mtu kuwa mume/mke bora na kuwa na ndoa iliyotengemaa.

Angalia matokeo ya tafiti za kienyeji katika maisha ya kawaida ya Kitanzania:


- Mahusiano mengi ya Aliyesoma hususani mwanaume na asiyesoma mwanamke yamekuwa ya kudumu sana. Itilafu inatokea pale mmoja anapoona kuwa yeye ni bora zaidi ya mwenza wake kwa ajili ya elimu aliyonayo, lakini kama hilo halipo mahusiano huwa ni ya kudumu zaidi
-Unapolala na mwenza hulali na degree wala udaktari bali unalala na mpenzi, raha na starehe zinazopatikanika hazinamahusiano kabisa na elimu ya mtu.
- Heshima katika mahusiano haitokani na elimu bali malezi bora toka kwa wazazi. Mwenza anaweza asiwe na elimu bali akashehena mambo muhimu katika mahusiano pamoja na mapenzi ya kweli, uadilifu, uchapakazi, hutuma, upenda kwa mwenzake na familia yake kwa jumla na kupelekea kuwa muhimili wa mahusiano
- Sioni sababu kwanini wasio na elimu fulani wa baguliwe, kwa mimi hakuna sababu ya kufanya hivyo kwakuwa kuna wengi wasionaelimu wamefanikiwa sana kimaisha na kiuchumi, wamekuwa wafanyabiashara wakubwa, wamekuwa na vipaji vikubwa.
- Mahusiano mengi ya wasomi yana migogoro sana, jipime wewe au unaowafahamu

Kwahiyo elimu bado sio kigezo katika kutafuta mahusiano bora na ya kudumu, wengine watasema exposure, lakini wewe uliyesoma unaweza kumfanya uliyenaye awe vyovyote unavyotaka wewe kama kweli unampenda. tusiogope sana ugumu wa maisha kwakutafuta mpenzi msomi unayetaka msaidiane naye na ukapoteza raha ya mapenzi katika maisha yako yote.

NAOMBA NIFAHAMISHENI KWANINI TWATUMIA KIGEZO CHA ELIMU? Nataka mtu anieleze objectively nini hasa. Mwisho natoa siri, mimi ni msomi wa kiwango cha juu kabisa na niko well exposed, nimefanyakazi nchi mbalimbali katika mabara yote karibuni na watu wa mataifa mbalimbali, na mke wangu hakusoma kabisa lakini we have been in a wonderful relationship, she is everything to me, sijaona kushindwa kufanyakitu kwakuwa hana elimu kubwa na sijaona kushindwa kutimiza majukumu yake kama mama wa familia na mzalishaji kiuchumi anapowezeshwa eti kwakuwa hana elimu. Naomba nielezeni nini kigezo hasa cha kubagua wenza kutokana na elimu.
 
nakubaliana na ww kwamba elimu sio kigezo cha msingi kwako, il kwangu nisingependa gap iwe kubwa mno. mke wangu natarajia awerafiki yangu wa karibu tuwe na uwezo wa kukaa na kuzungumza mambo mengi mbali ya mapenzi, kureason out mambo tofauti. sasa gap inapokuwa kubwa hata fikra hutofautiana sana hivyo kutakuwqa na vijiwelement vya utengano kwenye mambo flani. co wife anapewa nafasi ya kusema chochote ww huku unaanza kuhofia atasemama nini mama nanii ehee! ni hilo t na mentality niliyo jijengea, ni mtazamo wangu binafsi msijenge chuki.
 
Kweli mi naona nikaoe darasa la saba au form six
 
Post nimeshindwa kuimalizia.......ndefu sana.......hivi kuna mahali umezungumzia pesa......? Nataka nianzie hapo......
 
Pesa na uchumi ni sababu. Nahisi, pamoja na ugumu wa maisha, wanaume tumekuwa hatujiamini katika kutekeleza majukumu yetu ya uanaume na kutaka kugawana majukumu haya na wanawake. Mimi nadhani kama the head of the family ninajukumu la kuitunza familia yangu akiwemo mke na watoto kuanzia malazi, chakula, mavazi, afya, elimu na mengineyo regardles kama mke anafanyakazi au la, kama mke anafanyakazi basi hiyo ni added advantage lakini si kigezo cha kuacha majukumu ya kimsingi kama mwanaume, and I am so proud of fulfilling my responsibilities as a man and the head of the family. Tukilijua hili nyumba zetu zitakuwa na amani sana.

Post nimeshindwa kuimalizia.......ndefu sana.......hivi kuna mahali umezungumzia pesa......? Nataka nianzie hapo......
 
Nyerere alisema usimchague mtu kuwa kiongozi kwa sababu ya kabila/dini/ukanda na chagueni watu kwa kufuata sifa zao na wala si kabila/dini/ukanda. Mimi nasema usioe/usiolewe kwa sababu ya elimu ya mwenza, oone/oleweni kutoka na sifa za anayefaa kuwa mwenza bila kujali elimu yake. Kama elimu pekee ingekuwa kigezo basi waliooana na elimu tofauti wote wasingekuwa na mafanikio katika maisha ya kawaida ya ndoa na kiuchumi pia. Oa darasa la saba, oa shahada na daktari lakini elimu isiwe ni kigezo cha msingi cha mwanandoa atakayekuwa bora na mwema kwako, kumbuka hutafuta girlfriend wa kwenda nae disco, unatafuta mwanamke atakayeitwa mkeo na mama wa watoto wako kunakomajaaliwa.

Kweli mi naona nikaoe darasa la saba au form six
 
Nakubaliana na wewe na ninaheshimu fikra zako. Ila nakufahamisha kuwa elimu ya kuzaliwa ni more powerful than elimu ya darasani. Mimi ni typically village boy. Mama yangu mzazi hakusoma hata darasa moja lakini alikuwa na akili ya zaidi ya mwanamke aliyesoma chuo kikuku, alikuwa powerful woman hata wanaume hawakuweza kugusa nyumbani kwetu alitulea watoto watano as a single mamy na hautetereka eti kwakuwa hakusoma. Katika utoto wangu alikuwa mwenyekiti wa kijiji na chama kwa muda wa zaidi ya miaka 15 na aliacha mwenyewe na kuwa mshauri, alikuwa mzee wa baraza la mahakama ya mwanzo akitoa mchango mkubwa sana katika masuala ya kisheria, alikuwa mjumbe kayika board ya shule ya sekondari. Ninachotaka kesema ni kwamba omba upate mwanamke mwenye elimu ya kuzaliwa, nimeona wanawake wengi wamemaliza chuo hata kujieleza juongea mambo muhimu hawawezi, ukiwaintaview kwenye masuala ya kazi unaona huruma shule gani amesoma huyu maana hawezi kabisa. Kwahiyo kuwa mwangalifu, ila naheshimu mawazo yako na mtazamo wako kwakuwa si wote wasioenda shule wako kama my proud mamy.

nakubaliana na ww kwamba elimu sio kigezo cha msingi kwako, il kwangu nisingependa gap iwe kubwa mno. mke wangu natarajia awerafiki yangu wa karibu tuwe na uwezo wa kukaa na kuzungumza mambo mengi mbali ya mapenzi, kureason out mambo tofauti. sasa gap inapokuwa kubwa hata fikra hutofautiana sana hivyo kutakuwqa na vijiwelement vya utengano kwenye mambo flani. co wife anapewa nafasi ya kusema chochote ww huku unaanza kuhofia atasemama nini mama nanii ehee! ni hilo t na mentality niliyo jijengea, ni mtazamo wangu binafsi msijenge chuki.
 
Wanaume wa siku hizi hawataki kubeba majukumu yao hivyo huwa wanatafuta aliesoma wakiamini kuwa watasaidiana nusu kwa nusu kubeba mzigo wa familia. Fungu lingine liende kule kibanda hasara. Unadhani akioa asiesoma si atakuwa na mzigo mkubwa??
 
Nakubalina nawe ila Wanaume twapasa kuwa wanaume kamili pale tu tunapotimiza majukumu ya lazima na ya msingi katika familia zetu kama wanaume. Kunatofauti kati ya kuwa na elimu ya darasani na kuwa na akili hata kama huna elimu ya darasani. Unaweza ukakosa elimu ya darasani lakini unaweza ukafundishika katika masuala muhimu ya maisha likiwemo la kujitegemea kiuchumi unapowezeshwa. Mke asiyesoma lakini ana akili za kuzaliwa anaweza akawa empowered economically na akawa economically self-sustained. Nakupa mifano hai kabisa, kakangu ni darasa la saba ila mkewe amesoma lakini jamaa anarun business of more than 1 million usd. Mimi nimesoma na mke wangu hakusoma, bahati mbaya au nzuri mimi nimekuwa nikifanyakazi na mashirika makubwa ya Kimataifa kwa takribani miaka 10 sasa nikiwa nje ya nchi na miradi yetu yote ya kifamilia nyumbani ukianzia kwenye ujenzi wa makazi yetu na ya kibiashara na kilimo cha kisasa cha mashamba makubwa vinasimamiwa na mke wangu ambaye hata hata diploma ila ana akili ya kuzaliwa na anafundishika na kuelewa nini familia inahitaji na nini mchango wake kwenye maendeleo ya familia yetu. Tukiwawezesha na kuwaamini mnaweza. Tatizo tukishakuwa na elimu za juu tunadhani mke mzuri na mwema ni yule aliyesoma tu si kweli kabisa.


Wanaume wa siku hizi hawataki kubeba majukumu yao hivyo huwa wanatafuta aliesoma wakiamini kuwa watasaidiana nusu kwa nusu kubeba mzigo wa familia. Fungu lingine liende kule kibanda hasara. Unadhani akioa asiesoma si atakuwa na mzigo mkubwa??
 
Back
Top Bottom