Je KIKWETE alikurupuka kwa maagizo yake Wizara ya Elimu??

JokaKuu

Platinum Member
Joined
Jul 31, 2006
Posts
34,188
Reaction score
62,952
wana jamvi,

..nadhani mnakumbuka kwamba Raisi aliagiza shule zote sasa zitumie kitabu cha aina moja kufundishia somo husika.

..nilidhani Raisi alipaswa kusisitiza kuhusu waalimu na watunga mitihani kuzingatia syllabuss.

..masuala ya vitabu nadhani kila mtu anachagua kitabu kile ambacho anaona kinamsaidia kuelewa vizuri somo husika.

..halafu hivi katika dunia ya leo tunapaswa kweli kutegemea source/kitabu moja/kimoja katika kujifunza?

..JE RAISI ALIKURUPUKA???


kusoma makala nzima bonyeza hapa.
 


Hapo kweli alichemsha. Lakini hata hapa mtoni, unakuta kitabu kimoja tu kinatumika mpaka university level.

Mwalimu akicha-adapt kitabu kimoja vingine vinachapia tu.
 
Zakumi,

..inawezekana kukawa na kitabu kimoja wanaita reference book. halafu kuna vingine recommended.

..lakini hata mimi na wewe ukitupa kazi ya kufundisha, say O-level Biology, wewe unaweza kuchagua kufundisha kwa kutumia kitabu cha Modern Biology, mimi nikaamua kutumia Introduction to Biology.

..kuna mazingira mengine vitabu vinatofautiana uzuri topic by topic. mazingira hayo yanamlazimisha mwalimu/mwanafunzi kutumia kitabu zaidi ya kimoja.
 
JK alifikiri kuwa shule binafsi na Seminary zinafaulisha sana kutokana na kutumia vitabu tofauti, hivyo alitaka kiwe kimoja na kila shule itaweza kufaulu........
 

Katika level za chini kama shule za msingi na sekondari mara nyingi vitabu vinafuata mitaala na sioni sababu kwanini kitabu kimoja kisitumike. Tatizo linalokuja ni kuwa waalimu wenyewe sio wazuri au vitabu vyenyewe havitoshelezi kiu ya wanafunzi.

Kwenye vyuo kwa sababu mwanafunzi anatakiwa kufanya kazi zingine pekee yake kuna umuhimu wa kuwa na vitabu vingi. Lakini kwa waalimu wa Tanzania, kile kitabu kizuri anakificha hili wanafunzi wasijue maswali yatatoka wapi.
 
Kama Mungai aliweza kuanzisha somo jipya Tanzania kwa kuunganisha masomo ya Fizikia,Biolojia, na kemia na kuwa somo moja ,nini kitashindikana Bongo?
 
Mbona enzi zetu tulitumia abbot na lambert tu na mambo yalikuwa shwari!
 
JK alifikiri kuwa shule binafsi na Seminary zinafaulisha sana kutokana na kutumia vitabu tofauti, hivyo alitaka kiwe kimoja na kila shule itaweza kufaulu........

If that's was his logic behind his statement then is an Idiot thinking, he could have learned the private school 0r seminaries style rather than insisting on primitive style of looking at thinks like a fish
 
Mpita Njia said:
Mbona enzi zetu tulitumia abbot na lambert tu na mambo yalikuwa shwari!

Mpita Njia,

..enzi zetu kulikuwa na Complete Junior Physics, na kingine cha Chemistry. vitabu hivi vilikuwa kwa ajili ya form 1 na 2.

..vitabu vya Abbot[physics] na Lambert[chemistry] vilikuwa a little advanced kwa hiyo tulivitumia kuanzia form 3.

..mwanafunzi mdadisi aliyetaka kuchomoza zaidi ya wenzake ilibidi atafute references nyingine zaidi ya hizo zilizokuwepo mashuleni.

..umri ambao vijana wetu wanajiunga sekondari ni wakati ambapo wanapaswa kuwa wadadisi wenye kupenda kuuliza maswali, kujisomea, na kufanya utafiti. nadhani tutakuwa tunawadumaza kwa huu utamaduni wa kutegemea reference moja maalumu ktk masomo yao.

..kwa mtizamo wangu msisitizo uwekwe kwenye SYLLABUSS. kwamba waalimu wafundishe na kutunga mitihani kwa kufuata SYLLABUSS. wakaguzi wa elimu wazingatie hilo. suala la kitabu gani kitatumika waachiwe waalimu.
 
Yupo Prof. Maghembe pale....ndio mshauri wake mkuu....najua JK hakukurupuka kwenye hili....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…