Je kocha Antonio Conte kumaliza zama za Juventus kutamba Italia?

Je kocha Antonio Conte kumaliza zama za Juventus kutamba Italia?

uzeebusara

JF-Expert Member
Joined
Apr 15, 2013
Posts
657
Reaction score
514
Habari zenu!
Baada ya kukaa nje kwa muda toka alivyopishana na bodi na wachezaji wa klabu ya Chelsea Fc hatimaye kocha mwenye mzuka wa kushangilia na mbinu nyingi amerejea tena lakini katika ligi ya Italia. Na kwa sasa katika klabu ya Inter milan!
Wachambuzi na wajuzi wa soka mnalionaje hili kwa soka la Italia lililotawaliwa sana na klabu ya Juventus. Je Antonio Conte atamaliza ufalme wa Juventus katka ligi hii kwa msimu ujayo au itachukua muda sana?
Njooni tujadili hili!
 
Antonio Conte ni kocha mzuri sana ila ana tatizo la kugombana na wachezaji Sana. Mfano saiv kasema amtaki Icard ndo maana anamtaka Lukaku
 
Ila hy Icardi si kuna wakati alitaka kuweka mgomo kushinikiza auzwe? Anyway, jamaa ni muumini wa nidhamu ya juu sana labda hii inachangia kutofautiana na wachezaji. Ila swali linabaki je atakomesha ufalme wa Juve?
Antonio Conte ni kocha mzuri sana ila ana tatizo la kugombana na wachezaji Sana. Mfano saiv kasema amtaki Icard ndo maana anamtaka Lukaku
 
Teknikali jamaa ni mzuri sana, lkn je pale Inter Milan pana watu sahihi kwake kufit ktk mfumo wake jp hata mie naona kama uzoefu wa ile ligi pia utambeba sana
Anaanza na recruitment ya watu anaodhani watamfaa. Lukaku wa kwanza😄. Harafu ana uzoefu huko. Misimu mitatu Juve alitwaa ndoo mfululizo
 
Ila hy Icardi si kuna wakati alitaka kuweka mgomo kushinikiza auzwe? Anyway, jamaa ni muumini wa nidhamu ya juu sana labda hii inachangia kutofautiana na wachezaji. Ila swali linabaki je atakomesha ufalme wa Juve?
Anaeza kwa maana ni kocha mwenye mbinu nyingi ..yani anaweza kutumia mifumo miwili tofauti ndani ya mechi moja na zikafanikiwa.
 
Ni sababu zipo hasa zinazochangia Juventus kutawala soka la Italia ukiachana na uwekezaji wake kwa wachezaji? Je klabu kama As Roma, Ac, Inter Milan et al zilikosa makocha sahihi au pesa? Au wachezaji wasio viwango?
 
Utawala wa Juventus atauondosha pale Intermilan itakapotanua Budget na kulingana au kuizidi Juventus ili isajili World Class and Talented players kama Juve.
Venginevyo kwa Budget ya Kusajili average players kutoka Torino na Bologna basi Conte asitegemee kumtoa Juve kwenye Mstari.
 
Back
Top Bottom