Je, kujaladia madaftari lilikuwa jambo muhimu kiasi gani enzi za uanafunzi wako?

Je, kujaladia madaftari lilikuwa jambo muhimu kiasi gani enzi za uanafunzi wako?

The Sheriff

JF-Expert Member
Joined
Oct 10, 2019
Posts
747
Reaction score
2,112
Kuna jambo nimelikumbuka wakati nafanya mazungumzo na wafanyakazi wenzangu leo. Tulikuwa tukijikumbusha visanga na mambo mbalimbali ya miaka ya nyuma wakati tukisoma.

Ni kuhusu kujaladia madaftari. Hii kwa walimu wengi ilikuwa ni sharti muhimu; yaani akiingia darasani anaweza kuamua tu kukagua madaftari kama yamejaladiwa na yeyote anayepatikana na hatia anaambulia mikwaju kadhaa ya kumkumbusha kuwa “msafi”.

Wakati mwingine ilikuwa kwamba tukikusanya madaftari kwa ajili ya mwalimu kufanya usahihishaji, yalikuwa yanaweza kurudi yakiwa katika makundi mawili – yaliyojaladiwa na yasiyojaladiwa. Hapo sasa wenye madaftari yaliyo “uchi” wanaadhibiwa ili “kuwakumbusha” umuhimu wa kuwa “wasafi”.

Haikujalisha daftari lako lilikuwa safi kiasi gani, jalada ilikuwa ndiyo kipimo cha usafi kwa mujibu wa walimu wa enzi hizo. Sina hakika sana kama bado huu utaratibu bado unaishi.

Mimi nilikuwa natumia zaidi kalenda zilizopitwa na wakati. Upande mweupe usio na picha ndiyo nilikuwa napendelea zaidi utazamane na walimu ili kuthibibitisha “usafi” wangu. Wakati mwingine nilitumia magazeti.

Mpaka sasa sijajua kwanini kulikuwa na ulazima wa kujaladia; tena vikiambatana na kulazimishwa kwa bakora.

Hebu na wewe tupatie experience yako kuhusu hili. Karibu.
 
Kila baada ya siku mbili nilikuwa napewa adhabu kwa kosa la kuibia watu majaladio yao halafu naligeuza jalada, nje kuwa ndani na ndani kunakuwa nje, basi hapo daftari langu linakua jipya nishaepuka msala wa kulambwa stiki na ticha wa hesabu na upuuzi mkubwa nilikua Wala sikai na jalada kwa mda mrefu tayari nishakamatwa na kusemewa kwa mwalimu na kifuatacho ni kipigo.

Basi ile shule ule ndo ukawa wizi kila siku wa kuibiana majalada. Sasa nikikaa nikifikiria naona kua kumbe WIZI hapa TANZANIA una mizizi ya muda mrefu na ulianza zamani sana.
 
Niliacha kujaladia baada ya kujaladia na gazeti la kipuuzi bila kujua yan sabab ya utoto yani kurasa ya mbele lile gazeti liliandika habari ina jina Kama la mwalim alaf inasema" George mkumbo gerezani kwa kubaka" halafu yuma kun katuni ya watu wanabinuana Mara kifo Cha mende mim na utoto wangu sijui chchte Dadek lile ticha lilitaka kuniua siku ile plus adhabu Kali kinoma.
 
Niliacha kujaladia baada ya kujaladia na gazeti la kipuuzi bila kujua yan sabab ya utoto yan kurasa ya mbele lile gazeti liliandika habari ina jina Kama la mwalim alaf inasema" George mkumbo gerezani kwa kubaka" alaf nyuma kun katuni ya watu wanabinuana Mara kifo Cha mende mim na utoto wangu sijui chchte Dadek lile ticha lilitaka kuniua siku ile plus adhabu Kali kinoma.
Hahahaha
 
Kuna jambo nimelikumbuka wakati nafanya mazungumzo na wafanyakazi wenzangu leo. Tulikuwa tukijikumbusha visanga na mambo mbalimbali ya miaka ya nyuma wakati tukisoma.

Ni kuhusu kujaladia madaftari. Hii kwa walimu wengi ilikuwa ni sharti muhimu; yaani akiingia darasani anaweza kuamua tu kukagua madaftari kama yamejaladiwa na yeyote anayepatikana na hatia anaambulia mikwaju kadhaa ya kumkumbusha kuwa “msafi”.

Wakati mwingine ilikuwa kwamba tukikusanya madaftari kwa ajili ya mwalimu kufanya usahihishaji, yalikuwa yanaweza kurudi yakiwa katika makundi mawili – yaliyojaladiwa na yasiyojaladiwa. Hapo sasa wenye madaftari yaliyo “uchi” wanaadhibiwa ili “kuwakumbusha” umuhimu wa kuwa “wasafi”.

Haikujalisha daftari lako lilikuwa safi kiasi gani, jalada ilikuwa ndiyo kipimo cha usafi kwa mujibu wa walimu wa enzi hizo. Sina hakika sana kama bado huu utaratibu bado unaishi.

Mimi nilikuwa natumia zaidi kalenda zilizopitwa na wakati. Upande mweupe usio na picha ndiyo nilikuwa napendelea zaidi utazamane na walimu ili kuthibibitisha “usafi” wangu. Wakati mwingine nilitumia magazeti.

Mpaka sasa sijajua kwanini kulikuwa na ulazima wa kujaladia; tena vikiambatana na kulazimishwa kwa bakora.

Hebu na wewe tupatie experience yako kuhusu hili. Karibu.
Nakumbuka toka darasa la TATU daftari langu la hesabu nilikuwa nashonea Uzi, daftari likawa kubwa nilipofika la sita Uzi ikawa ngumu nikashonea waya
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]

Yaani daftari Moja najazia Tu mpaka darasa la Saba mwanzoni . Akaja mwalimu mmoja akaniboa fundisha yake yaani simwelewi kabisa nikaamua kuliacha nikaanzisha mengine

Tulikuwa tukikaa tunaanza kulingishiana Una vema ngap ( zilizoandukwa kabisa vema) na Una vizuri ngapi [emoji13][emoji13][emoji13][emoji13][emoji13]

Ila hesabu nilikuwa naipenda Sana

Daaah

Nkaja kuambulia PCB

AKI YA NANI
 
Nakumbuka toka darasa la TATU daftari langu la hesabu nilikuwa nashonea Uzi, daftari likawa kubwa nilipofika la sita Uzi ikawa ngumu nikashonea waya
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]

Yaani daftari Moja najazia Tu mpaka darasa la Saba mwanzoni . Akaja mwalimu mmoja akaniboa fundisha yake yaani simwelewi kabisa nikaamua kuliacha nikaanzisha mengine

Tulikuwa tukikaa tunaanza kulingishiana Una vema ngap ( zilizoandukwa kabisa vema) na Una vizuri ngapi [emoji13][emoji13][emoji13][emoji13][emoji13]

Ila hesabu nilikuwa naipenda Sana

Daaah

Nkaja kuambulia PCB

AKI YA NANI
😂😂😂😂😂 Tumetoka mbali sana, jamaa yangu.
 
Niliacha kujaladia baada ya kujaladia na gazeti la kipuuzi bila kujua yan sabab ya utoto yani kurasa ya mbele lile gazeti liliandika habari ina jina Kama la mwalim alaf inasema" George mkumbo gerezani kwa kubaka" halafu yuma kun katuni ya watu wanabinuana Mara kifo Cha mende mim na utoto wangu sijui chchte Dadek lile ticha lilitaka kuniua siku ile plus adhabu Kali kinoma.
Tumekuzwa kibabe sana aisee 😂
 
Back
Top Bottom